Tuesday 25 March 2014

Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Home » General News » Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Screen Shot 2014-03-25 at 8.53.23 AM
Idadi ya waliofariki kutokana na shambulizi la Kanisa Mombasa Kenya March 23 2014 imefikia sita ambapo wote hao vifo vyao vimetokana na majereha ya risasi huku wengine tisa waliokua wakipata matibabu hospitali wakiruhusiwa kwenda nyumbani.
Mkuu wa Polisi Kenya amesema bado hawajafutilia mbali kwamba lilikua shambulio la kigaidi ambapo kwa mujibu wa Erick Ponda ambae ni mwandishi wa habari wa DW Mombasa alieongea na millardayo.com akisema mpaka March 24 2014 jioni watu 59 walikua wamekamatwa na Polisi kwenye msako wakituhumiwa kuhusika na shambulio hilo.
Wakati huohuo, mtoto ambae bado kichwani kwake kuna risasi aliyopigwa kwenye shambulio hilo amepelekwa kwenye hospitali ya binafsi kwa matibabu maalum kwa sababu anahitaji kufanyiwa upasuaji ili kuokoa maisha yake.
Mama mzazi wa mtoto huyu alifariki kwenye hili shambulio hivyo kwa sasa mtoto yuko na ndugu wa mama yake ambae namkariri akisema ‘haendelei vizuri manake amekua akinisumbua hawezi kulala, ana maumivu makali sana kichwani kutokana na hiyo risasi ndani ya kichwa’
Viongozi wa kidini wakiongozwa na Askofu Julius Atsango wamewataka wenzao wa dini ya kiislamu kuisaidia serikali kuwakamata wanaosingizia dini kutekeleza mashambulizi