Tuesday 4 March 2014

Mamilioni ya Airtel ‘Mimi ni Bingwa’ yaenda Bukoba

Dar es Salaam. Promosheni ya ‘Mimi ni Bingwa’ imemtangaza Rashid Jacob Kagombola, mkazi wa Bukoba mkoani Kagera kuwa mshindi wa Sh50 milioni katika droo kubwa ya bahati nasibu iliyochezeshwa na Kampuni ya Mawasiliano ya Airtel Tanzania mwishoni mwa wiki Dar es Salaam.
Akimtangaza mshindi huyo, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema: “Leo hii tumefikia mwisho wa Promosheni yetu ya ‘Mimi ni Bingwa’ ambayo imewanufaisha Watanzania wengi. Limekuwa ni zoezi la mafanikio likishirikisha idadi kubwa ya wateja waliojiunga katika promosheni hii iliyokuwa na vipengele tofauti.”
“Ningependa kuwashukuru wateja wetu kwa kushiriki promosheni hii tangu ilipoanza mwishoni mwa Novemba mwaka jana. Airtel bado ina mipango mingine mingi inakuja, tukilenga kuendelea kurudisha kile tulichonacho kwa wateja wetu na kuisaidia jamii inayotuzunguka kukuza viwango vyao vya maisha.”
Alisisitiza kuwa mbali na zawadi hiyo ya Sh50 milioni kutolewa, washindi wa awamu ya pili na ya tatu wa safari iliyogharimiwa kila kitu ya kwenda kuangalia mechi ya Klabu ya Manchester United wataondoka nchini mwezi huu pale klabu hiyo itakapocheza tena kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Naye mshindi wa Promosheni hiyo, Rashid Jacob, akizungumza kwa njia ya simu kutoka Bukoba, aliipongeza Airtel Tanzania kwa kuanzisha promosheni hiyo ambayo amedai imesaidia kubadili maisha ya wateja wake na kuwa na mabadiliko chanya katika jamii na nchi nzima kwa jumla.
“Hii ni miujiza inayotokea maishani mwangu. Siwezi kuamini nami nimeingia katika orodha ya mamilionea Tanzania. Kwangu ni kama kutimia kwa ndoto kwa sababu ya Airtel. Naishukuru Airtel Tanzania. Hakika hizi milioni 50 zitabadilisha maisha yangu kabisa na zawadi nitakayoipatia Airtel ni kubaki kuwa mteja wao mwaminifu wakati wote,” alisema Kagombola.
Wakati wa promosheni hiyo, washiriki wawili wa Mimi ni Bingwa wa kila siku walizawadiwa Sh2 milioni , wawili wa Sh5 milioni katika droo za kila wiki na mmoja tiketi mbili za safari iliyogharimiwa kila kitu kwenda jiji la Manchester.

 

Kardinali Pengo aweka wazi msimamo wa Kanisa

 Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo akiwaonesha waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, nakala ya gazeti la Mwanachi lililoandika habari kuhusu msimamo wa Kanisa juu ya suala la serikali tatu. Picha na Venance Nestory  

Dar es Salaam/Iringa. Siku mbili baada ya Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kutoa waraka wa kulitaka Bunge Maalumu la Katiba kutopuuza mapendekezo ya muundo wa serikali tatu, Askofu Mkuu wa Jimbo Mkuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka na kusema msimamo huo siyo wa Kanisa Katoliki nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kardinali Pengo pamoja na kukiri kuwa tume ilitoa maoni hayo, alikanusha kuwa taarifa zilizotolewa na moja ya magazeti kuwa msimamo wa Kanisa Katoliki ni serikali tatu.
“Maoni ya Tume hayawezi kuwa ni msimamo wa kanisa. Kanisa Katoliki lina utaratibu wa kutoa misimamo yake na huwa inatolewa na Mwenyekiti wa TEC,” alisema.
Hata hivyo, Rais wa TEC, Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa kutoka Jimbo la Iringa, alisema jana kuwa alikuwa na shughuli nyingi, hivyo asingeweza kuzungumzia suala hilo, labda wiki ijayo.
Akizungumza katika makazi yake mjini Iringa, Askofu Ngalalekumtwa alisema: “Mniache, nina shughuli nyingi…labda mnitafute wiki ijayo,” alisema.
Vilevile, Pengo ambaye alirejea msimamo wake binafsi wa kuunga mkono Muungano wa serikali mbili, alisema kwa namna Rasimu ya Katiba ilivyo, hakuna kigezo cha kulazimisha Kanisa Katoliki litoe msimamo.
Alisema Kanisa Katoliki lingeweza kutoa msimamo iwapo Rasimu ya Katiba ingekuwa na dosari zinazohusu imani au maadili.
“Kwa mfano, (Rasimu) ingekuwa inasema, hakuna Mungu lazima tungekuja juu kwa sababu inaingilia imani yetu,” alisema Kardinali Pengo na kufafanua:
“Vilevile tungeweza kusema inakwenda kinyume na maadili iwapo inaruhusu kuua wazee au inaunga mkono ndoa za jinsi moja.”
Tamko la Tume
Tamko la tume hiyo inayoongozwa na Askofu Mkuu wa Tabora, Paulo Ruzoka liliweka bayana kuwa muundo wa serikali mbili haukutatua matatizo ya msingi na badala yake ulilimbikiza kero zilizosababisha Zanzibar kujiundia katiba yake mwaka 2010 bila kushauriana na Tanzania Bara.
Tamko hilo la kurasa 15 lililosambazwa kwa baadhi ya Wajumbe wa Bunge la Katiba, lilitolewa baada ya mkutano wa kitaifa wa Wajumbe wa Kamati za Majimbo za Haki na Amani za Kanisa hilo na Chama cha Wanataaluma Wakatoliki Tanzania (CPT), uliofanyika jijini Dar es Salaam Februari 5 na 6 mwaka huu.

 

Sitta apiga jaramba kuongoza Bunge

 

Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Ameir Kificho, akizungumza na mjumbe wa Bunge hilo, Samuel Sitta (kushoto), ndani ya Ukumbi wa Bunge, Dodoma jana. Picha na Emmanuel Herman   

Dodoma. Siku moja baada ya kuteuliwa na CCM kuwania uenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema ameanza kupitia sheria na kanuni zitakazomwezesha kuliongoza huku akiahidi kutenda haki kwa wajumbe wote iwapo atachaguliwa.
Akizungumza mjini Dodoma jana, Sitta alisema: “Nawashukuru wote waliokuwa wakiniunga mkono na niseme wazi kuwa nitatenda haki kwa wajumbe wote wa Bunge Maalumu la Katiba.”
Alisema kazi kubwa aliyonayo baada ya uteuzi huo ni kuhakikisha kuwa anazipitia sheria na kanuni zinazoongoza bunge hilo na sheria nyingine kwa kuwa ndizo nyenzo zake za utendaji kazi.
Akizungumzia mchakato wa uteuzi ndani ya chama hicho na mchuano uliokuwapo kati yake na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge alisema: “Hii ni hatua ya awali na ya kawaida tu ndani ya CCM. Mara nyingi chama changu kikiona kuna mambo yanayoleta msuguano, basi huamua kuteua jina moja kwa ajili ya kugombea. Wameteua majina mawili kwa demokrasia kabisa. Ninakishukuru chama changu kwa kuniteua na kwa sasa najiandaa na uchaguzi.”
Suluhu: Nitafanya maajabu
Kwa upande wake, Mjumbe wa bunge hilo aliyeteuliwa na CCM kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu Hassan aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba ana uwezo mkubwa wa kuliongoza Bunge Maalumu la Katiba na hana shaka katika uteuzi wake.
Samia ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), alijisifu akisema ana rekodi nzuri ambayo haitiliwi shaka kwa weledi wake na haoni tatizo kwa yeye kupewa nafasi hiyo.
“Nina rekodi nzuri ya kuongoza Serikali kwa muda mrefu na sijapata doa lolote, kwa hiyo sioni ugumu wowote,” alisema.
Samia aliwahi pia kuwa Waziri wa Ajira na Wanawake na baadaye, Waziri wa Utalii katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kabla ya kuwa Waziri wa Nchi, katika Ofisi ya Makamu wa Rais.
Kinana na mchakato
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alizungumzia mchakato uliompitisha Sitta kuwania nafasi hiyo na kusema ulilenga kuzuia mgawanyiko ndani ya chama.
Hata hivyo, alisema Chenge aliamua kwa hiari yake kujitoa baada ya kukubaliana na Sitta walipoitwa na uongozi wa chama kwa ushauri. Akizungumza katika mahojiano maalumu mjini Dodoma, Kinana alisema: “Kiutaratibu, yeyote ilimradi awe mjumbe wa Bunge la Katiba, angeweza kujitokeza kugombea uenyekiti. CCM, walijitokeza wawili walionyesha nia; Sitta na Chenge.






Mauaji zaidi yatokea Nigeria



Ghasia zaidi zimetokea Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambapo watu 13 wameuawa.
Mkaazi wa kijiji cha Jakana karibu na mji wa Maiduguri jimbo la Borno amesema takriban watu 40 wameuawa katika shambulio lililofanywa na kundi la Boko Haram JUmatatu usiku.
Kaskazini mwa Nigeria imeshuhudia mashambulio ya kundi la Boko Haram licha ya operesheni ya jeshi inayoendelea.
Hapo Jumapili usiku watu 30 waliuawa katika shambulio mji wa Mafa na watu wengine 90 waliuawa katika siku ya Jumamosi katika shambulio la bomu mjini Maiduguri.

Keqiang asema mageuzi ni sharti China 


Li Keqiang akihutubia bunge la Uchina.
Waziri mkuu wa China, Li Keqiang, ameuambia mkutano wa kila mwaka, wa bunge la taifa hilo mjini Beijing, kwamba maendeleo ya kiuchumi yanasalia kuwa jukumu kubwa zaidi la serikali, lakini marekebisho ya kimsingi ni sharti yatekelezwa japo ni machungu.
Bwana Li amewaambia maelfu ya wajumbe katika bunge la taifa hilo, Great Hall of the People, kwamba shabaha ya kila mwaka ya ukuaji wa kiuchumi itasalia kuwa asilimia saba nukta tano.
Akizungumzia tatizo la uchafuzi, amesema kuwa moshi mkubwa unaondelea kutanda katika miji mikubwa ya China, ni onyo la kiasili dhidi ya maendeleo yasiokuwa na mpango.
Waziri huyo mkuu wa China kadhalika ametangaza marufuku dhidi ya majengo mapya ya serikali kama sehemu ya kile alichokitaja kuwa mapambano bila huruma dhidi ya ufisadi.

 

Obama ataka wachunguzi kutumwa Ukraine

 

Hali ya wasiwasi imekumba jimbo la Crimea.
Rais Obama ametangaza mapendekezo ambayo huenda yakatoa suluhu kwa mzozo wa Ukraine, ikiwemo kuwatuma wachunguzi wa kimataifa na kuanzishwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Moscow na serikali mpya mjini Kiev.
Bwana Obama amejadili swala hilo kwa njia ya simu na chanzela wa Ujerumani, Angela Merkel.
Wachunguzi hao watalenga kulinda haki za watu wa kabila la Urusi waliopo katika jimbo la Crimea; na kwa upande wake Urusi itahitajika kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo hilo. Pendekezo hilo huenda likajadiliwa pembezoni mwa mkutano utakaofanyika nchini Ufaransa (Jumatano) ambao utawaleta pamoja wajumbe kutoka Marekani, Urusi na kwingineko kwa ajili ya kuijadili Lebanon.
Hapo awali waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry, amelaani kile amekitaja kuwa kitendo cha uchukozi kutoka Urusi dhidi ya Ukraine. Wakati wa ziara yake mjini Kiev ambapo aliweka shada la maua kuwakumbuka waandamanaji waliouwawa mwezi uliopita, bwana Kerry ameshutumu Moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Mwandishi wa BBC Sarah Reinsford aliyepo mjini Kiev amesema kuwa wakati akiweka shada la maua katika maeneo walikouwawa mamia ya waandamanaji mjini humo, John Kerry alikaribishwa na umati wa watu waliokuwa wakiomba msaada wa marekani.
Na hilo ndilo lililomleta hapa; kutoa msaada wa hali na mali na pia wa kisiasa kwa serikali ya mpito ya Ukraine, na pia ahadi ya msaada wa kifedha na wa kiufundi kusaidia katika kuimarisha uchumi, amesema mwandishi wetu.

Rais Putin.

Lakini zaidi ya yote bwana Kerry ameleta ujumbe kwa Moscow.
" Nadhani ni bayana kwamba Urusi imekuwa ikifanya bidii kubuni dhana ya kuiwezesha kutekeleza uvamizi zaidi. Urusi imezungumzia raia wachache wanaozungumza kirusi ambao wamezingirwa. Ukweli ni kwamba hawajazingirwa! Ukweli ni kwamba serikali mpya ya Ukraine imewajibika ipasavyo kwa kuhimiza utulivu na kujiepusha na uchokozi," amesema Bwana Kerry.
Haukuna ushahidi, amesisitiza, kwa madai ya urusi kwamba wanajeshi wake wanalinda raia wanaozungumza lugha ya kirusi nchini Ukraine akiishutumu moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Katika karne ya ishirini na moja, bwana Kerry ameonya, haiwezekani kuvamia taifa jingine na kisha kuamrisha matakwa yako yatekelezwe kwa kutumia mtutu wa bunduki. Na kisha akamhimiza rais Putin kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea na kushughulikia malalamishi yake kupitia njia za kisheria na amani.
Lau sivyo, ameonya, kwamba Urusi itakabiliwa na vikwazo zaidi vya kiuchumi na kisiasa.

 

CHAMA KIPYA CHA SIASA ACT CHAIONDOA CHADEMA KIGOMA RASMI LEO SOMA HAPA LIVE!!


HATIMAYE CHADEMA YAFUTWA RASMI KIGOMA NA ACT-TANZANIA

CHAMA KIPYA CHA ACT CHASHUSHA BENDERA ZA CHADEMA KIGOMA

CHAMA cha Alliance For Change and Transparency Mkoa wa Kigoma,kimeshusha Bendera ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA tawi la Ujiji stendi ya zamani na kupandisha bendera ya (ACT) wakati wa uzinduzi rasmi wa matawi sita katika manispaa ya kigoma ujiji.


Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, Katibu wa ACT Mkoa Athuman Kabogo alidai lengo la kushusha bendera hiyo ni hatua ya kukataa kugeuzwa kuwa vibaraka wa watu wengine kwa kukosa haki ya kuhoji na kuwania nyadhifa za chama hicho na
hivyo kuanzisha ACT kama chama cha wanyonge kinachoweza kuwasikiliza na kutoa haki kwa kila mmoja.

Kabogo aliwataka wanachama wahitaji, wachukue kadi za ACT ili chama kipate usajili kamili kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu husika pamoja na kutoa michango endelevu ,ikiwa ni jitihada za makusudi kuhakikisha chama kinasonga mbele
kwa maslahi ya Taifa.

�Wananchi nyie ni chachu ya chama kuwepo kwenye mchakato wa uchaguzi mdogo wa wenyeviti wa serikali za mitaa kwa kukiamini na kukipatia ridhaa kiweze kuleta
mabadiliko ya kimaendeleo� alisema Juma Ramadhan aliyekuwa katibu kampeni wa CUF kigoma.

Kwa upande wa Katibu ACT Kanda Magharibi Wiston Moga alisema, lengo la chama ni kuleta mabadiliko kwenye ulingo wa siasa,ambapo wao wamedhamiria kutetea maslahi ya umma kwa lengo la kuondoa mfumo wa maslahi binafsi ambayo ni chachu ya vyama vya siasa kushindwa kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi.

Katika ziara hiyo ya uzinduzi wa matawi ya chama husika,ACT kimefanikiwa kufungua matawi kwenye kata sita kati ya kata 19 zilizopo katika manispaa ya kigoma ujiji,huku baadhi ya viongozi kutoka UPD,CHADEMA na CUF wakijiunga na chama hicho
kwa kudai wanahitaji chama chenye uchungu na kukabiliana na changamoto za wanyonge.

Hata hivyo wanachama 3500 wa chama cha Democrasia na Maendeleo Chadema katika tawi la Ujiji mkoani Kigoma wamehamia chama kipya cha Alliance For Change and Transparency (ACT).

 

Mauaji zaidi yatokea Nigeria 

Ghasia zaidi zimetokea Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambapo watu 13 wameuawa.

 

Mkaazi wa kijiji cha Jakana karibu na mji wa Maiduguri jimbo la Borno amesema takriban watu 40 wameuawa katika shambulio lililofanywa na kundi la Boko Haram JUmatatu usiku.
Kaskazini mwa Nigeria imeshuhudia mashambulio ya kundi la Boko Haram licha ya operesheni ya jeshi inayoendelea.
Hapo Jumapili usiku watu 30 waliuawa katika shambulio mji wa Mafa na watu wengine 90 waliuawa katika siku ya Jumamosi katika shambulio la bomu mjini Maiduguri.

 

GHOROFA LADAIWA LIMEPINDA

Upande mmoja wa jengo hilo.
Likionekana kwa mbele.
Likionekana kwa mbali.
JENGO la ghorofa tano linalojengwa pembezoni mwa barabara ya kwenda Tandale Sokoni maeneo ya Manzese limepigwa marufuku na mamlaka husika kuendelea kujengwa kutokana na kuonekana limepinda.

BREAKING NEWSSS!! LIZIWANI KIKWETE ASHINDA KURA ZA MAONI ZA UBUNGE CHALINZE

  

 
Ndg.Ridhiwani Kikwete Mgombea wa ubunge katika Kura za Maoni za CCM jimbo la Chalinze akijipigia Kura leo.
 
...akipanga mstari (katikati) katika uwakilishi wa Kata anayotoka ya Msoga.
Matokeo:
Ridhiwani Kikwete kashinda kwa kupata kura 758 kati ya kura 1321,
Ilikuwa hivi:_
1.Ridhiwani Kikwete kura 758
2.Shaban Iman Madega kura 335
3.Athuman Ramadhan Maneno kura 206
4.Changwa Mohamed mkwazu kura 12
Kura zilikuwa 1363 zilizo Haribika 5 na Halali ni kura 1316
Wagombea wa Ubunge Chalinze kwa tiketi ya ccm walikuwa ni:-
1.Ndg.Ridhiwani Kikwete,
2.Shaban Iman Madega,
3.Athuman Ramadhan Maneno
4.Changwa Mohamed mkwazu
Tarehe 9/3/2014 KUCHUKUA FOMU
Tarehe 11/3/2014 KURUDISHA
Tarehe 15/3/2014UZINDUZI RASMI WA KAMPENI ZA CCM

Tutatetea kwa nguvu uhuru wa habari-Mukajanga

 

Katibu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga amesema uwepo wa wanahabari na wadau wa habari kwenye Bunge la Katiba kutasaidia kutetea kwa nguvu zake zote vipengele vinavyotoa haki ya uhuru wa habari kwenye Rasimu ya Katiba.
Mukajanga, ambaye pia ni mmoja wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki kuwa kupendekezwa kwa uhuru huo ni jambo moja na kupitishwa kwa vifungu hivyo ni jambo jingine.
Kwa mujibu wa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Ibara ya 31 (1) inapendekeza haki ya kila mtu kuwa na uhuru wa kutafuta, kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa.
Pia Rasimu hiyo inatoa haki kwa mtu kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi na vitakuwa huru kupata, kutumia na kusambaza habari.
Kajubi, ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, alisema jambo kubwa ambalo tayari ameshalifanya ni kuwatambua wadau wa habari ndani ya Bunge hilo, ambao atashirikiana nao katika kusukuma agenda hiyo.
“Mapendekezo yetu karibu yote tuliyoyatoa mbele ya Tume ya Jaji Warioba (Joseph) yameingizwa kwenye hii Rasimu. Jukumu letu sisi (wajumbe) sasa ni kushawishi ili yaweze kupitishwa bungeni,” alisema.
Kajubi pia alisema wadau wote wa habari, likiwemo Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na waandishi wenyewe, wana wajibu mkubwa wa kushawishi kuhusu kupitishwa kwa ibara hizo.
Kwa mujibu wa rasimu hiyo, masuala mengine yaliyomo ni haki ya vyombo vya habari kuwa huru kusambaza taarifa kwa wananchi.
Pia kulinda utu, heshima na staha ya wananchi dhidi ya habari hizo.
Ibara ya 31(4) inaibana Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi kuwa na wajibu wa kikatiba wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.

 

Wana-CCM Dodoma waonya wajumbe

Dodoma. Chama cha Mapinduzi, Kata ya Chang’ombe katika Manispaa ya Dodoma kimeonya kuwa Katiba mpya isipotoa matumaini ya wananchi kupimiwa ardhi, hawataitambua na hawatakuwa tayari kupiga kura ya kuchagua kiongozi yeyote katika maeneo yao.
Wanachama wa chama hicho walitoa kauli hiyo katika kikao chao kilichofanyika Tawi la Mji Mwema.
Walisema Serikali kupitia Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) imewahadaa na kwamba matumaini yao sasa yako ndani ya Katiba.
Wananchi hao pia waliushutumu uongozi wa CCM wa Mkoa wa Dodoma kwa madai ya kushirikiana na CDAkuwanyima haki zao.
Hata hivyo, Katibu wa CCM wa Mkoa wa Dodoma, Albert Mgumba alikanusha madai hayo na kueleza kwamba chama hicho kinafanya kila njia kupigania haki za wananchi hao.
Mgumba alisema mfumo wa CDA ndiyo tatizo kubwa na kwamba hiyo inachangiwa na muundo wake.
Mwenyekiti wa CCM wa Tawi la Mji Mwema, Hussein Binde alisema wamekuwa wakidanganywa kuwa watapimiwa ardhi yao lakini hakuna kilichofanyika.

 

Wamisri wainyima ulaji Yanga 

Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu (jezi ya kijani) akiwania mpira na mabeki wa Al Ahly wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jumamosi iliyopita. Yanga ilishinda 1-0. Picha na Michael Matemanga.  

Dar es Salaam. Klabu ya Yanga imepoteza dola 70,000 za Kimarekani (Sh 111.2 milioni) baada ya kampuni ya MGB ya Misri kushindwa kurusha moja kwa moja ‘Live’ mechi kati ya timu hiyo na Al Ahly iliyochezwa Uwanja wa Taifa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Awali, Yanga iliingia mkataba wa Dola za Marekani 90,000 na kampuni hiyo kwa ajili ya kuonyesha mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kuwania kucheza raundi ya pili na ikapewa malipo ya awali dola 20,000.
Mwakilishi wa Kampuni ya MGB, Francis Gaitho aliuambia mtandao wa Al Ahly.com kuwa wanailaumu Yanga kwa kukwamisha zoezi la kurusha mechi hiyo, akidai waliwafukuza uwanjani wafanyakazi wa televisheni ya Star TV na kamera zao waliokwenda kurusha moja kwa moja pambano hilo.
Alisema baada ya kusaini mkataba na Yanga, waliwalipa fedha za awali kutoka kwenye akaunti yao nchini Misri kwenda kwenye akaunti ya klabu hiyo Tanzania.
Gaitho alisema timu ya watu wa utayarishaji waliotakiwa kuja Dar es Salaam kurekodi mchezo huo ilishindwa kufika kwa wakati kutoka Cairo, hivyo wakalazimika kutafuta kampuni ya Tanzania kufanya kazi hiyo na Star TV ya Tanzania ikabahatika kupata zabuni kutoka kwao.
Alisema kuwa licha wa ubalozi wa Misri nchini Tanzania kuiandikia barua klabu ya Yanga kwamba MGB italipa malipo yaliyobaki baada ya mechi na kudhaminiwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, uongozi wa Yanga iligoma kurekodiwa  kwa mechi hiyo.
“Wakati tulipofikia mwafaka na kukubaliana mechi irekodiwe, kwa bahati mbaya Star TV walikuwa tayari wamekwishaondoka uwanjani na muda ulikuwa umeenda,” alisema Gaitho.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Mussa Katabaro akizungumzia madai hayo katika mahojiano na mtandao wa Bin Zubery alikiri klabu hiyo kupokea malipo ya Dola 20,000 na kudai kuwa klabu yake ilipaswa kulipwa kiasi kingine cha Dola 35,000 kabla ya mechi na Dola 35,000 nyingine baada ya mechi, lakini MGB ilishindwa kutekeleza kipengele hicho cha mkataba. “Mbaya zaidi, katika mkataba wetu na wao tulikubaliana hakuna kupelekana mahakamani, sasa tulipoona wameshindwa kulipa zile fedha.
Katabaro alisema wateja wao hawakuwa wa kweli katika maelezo yao baada ya kudai kwamba kuna mtu alikuwa anakuja na fedha kutoka Misri akakamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cairo wakati si kweli.  
Alisema baadaye walidai ubalozi wa Misri hapa nchini utalipa hizo fedha, lakini ulipoulizwa ulikana na ndipo TFF ilipojitolea kuwaandikia Yanga SC hundi ya dola 35,000 na dola 10,000 kwa Stars TV ili mechi ionyeshwe.
“Sisi tulikubali kupokea hundi ya TFF mechi ionyeshwe, lakini Star TV wakagoma kupokea hundi ya TFF wakaondoka, sisi hatukuwafukuza kama wanavyodai hao jamaa, kimsingi hawa jamaa wametukosesha fedha dola 70,000.
“Kuna kampuni nyingine ya Misri ilijitokeza ikiwa tayari kutupatia dola 100,000 kununua haki za TV za hiyo mechi, lakini sisi tukaheshimu mkataba wetu na MGB, ila mwisho wa siku uungwana wetu umetuponza,”alisema Katabaro

 

Mwelekeo mpya bungeni, Pinda atoa hoja kutuliza hali ya hewa

Dodoma. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alifanikiwa kutuliza hali ya hewa bungeni baada ya kutoa mapendekezo yaliyoungwa mkono na pande zote zilizokuwa zinavutana kuhusu kupitisha baadhi ya vifungu vya Kanuni za Bunge la Katiba. 

 

Katika mapendekezo yake yaliyoungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa CCM -Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Pinda alisema: “Nataka kuwaomba wenzangu wote kwenye maeneo hayo (yenye malumbano) tukiwa tunayapitia kama hatutaelewana tuyaache kwa muda na kumwomba Mwenyekiti aunde timu ya watu wazima na wenye busara wajaribu kuyatazama. “Tujadiliane, tushindane kwa lugha za staha, tusitumie lugha inayoweza kukasirisha. Isiwe mimi nimesema, mimi nimesema...”
Waziri Mkuu, aliwataka wajumbe wajiepushe na lugha za kuudhi ambazo zinaweza kukwamisha upatikanaji wa Katiba Mpya.
Pinda alilazimika kuingilia kati baada ya kutokea mgawanyiko mkubwa wa namna ya kupiga kura kupitisha vifungu vya rasimu.
Akiunga mkono ushauri huo, Mbowe alisema Bunge limejaa hisia za hofu ndani na nje, jambo ambalo linatia wasiwasi wa kupatikana kwa Katiba Mpya. Alisema iwapo wajumbe watashirikiana na kuweka kando masilahi ya vyama, idadi yao katika makundi, Katiba inaweza kupatikana.
Vuai alionya kuhusu matumizi ya lugha za kuudhi huku Profesa Lipumba akiwataka wajumbe kuzingatia masilahi ya Taifa kama alivyoagiza Rais Jakaya Kikwete na kutengeneza Katiba ya Watanzania wote bila ya kujali masilahi binafsi.
Upigaji kura bungeni vita
Awali, mjadala wa utaratibu wa upigaji kura katika Bunge hilo ulichukua sura mpya baada ya kudaiwa kuwapo ushawishi unaohusisha utoaji wa bahasha ili kutaka kuungwa mkono katika misimamo inayokinzana.
Habari zilizopatikana zilidai kuwa watuhumiwa katika sakata hilo ni baadhi ya wajumbe ambao ni mawaziri na mbunge mmoja wa CCM. Vigogo hao wanadaiwa kuwashawishi wajumbe ambao hawatokani na vyama vya siasa ili kupitisha agenda ya kura ya wazi kirahisi.
Akiandika kwenye ukurasa wake wa Facebook, Mjumbe wa Bunge hilo, Julius Mtatiro ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF, alisema: “Jaribio la kuzuia kura ya siri limechukua njia za aibu, baada ya CCM kutumia fedha kushawishi wajumbe.”
Katika ujumbe huo ambao alikiri kuuandika, Mtatiro aliwataja wajumbe watatu ambao ni mawaziri kuwa waliwakaribisha wajumbe kwenye makazi yao na “kuwaandalia chakula cha kutosha, vinywaji vya kutosha na viburudisho vingine, huku wakipewa bahasha za nauli baada ya vikao hivyo vya siri.” Mmoja wa waliotajwa ni Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe aliyedaiwa kuwaalika wawakilishi wa wafugaji na kuwapa chakuka na bahasha.
Akijibu tuhuma hizo, pamoja na kukiri kuwakaribisha baadhi ya wajumbe na kula nao chakula, alikana tuhuma za kuwahonga ili waunge mkono msimamo wa chama hicho. Alisema Mtatiro amemdhalilisha, hivyo anawasiliana na mwanasheria wake ili kumfikisha mahakamani.

 

 

Wabunge wa Libya washambuliwa 

Wabunge wawili nchini Libya walipigwa risasi na kuumizwa baada ya kundi la waandamanaji kuwashambulia bungeni katika mji mkuu wa Tripoli.
Walioshuhudia tukio hilo, walisema kuwa wawili hao walipigwa risasi walipojaribu kutoroka kutoka katika eneo hilo.
 
Waandamanaji hao waliokuwa na ghadhabu walilishambulia bunge hilo, huku wakitaka bunge lifungwe na tarehe mpya ya uchaguzi wa mapema itangazwe.
Kumekuwa na wimbi la maandamano nchini humo kutokana na uamuzi wa bunge la nchi hiyo kuahirisha tarehe ya uchaguzi hadi baadaye mwakani.
Waliolishambulia bunge siku ya Jumapili walisema kuwa walighadhabishwa pia na “kutekwa nyara” kwa waandamanaji waliokuwa na kikao nje ya bunge.
Walisema kuwa waliohusika na utekaji nyara huo walikuwa chini ya uongozi wa waasi wanaotumikia amri ya bunge.
Waandamanaji hao ambao wengi wao ni vijana walijihami kwa visu na vijiti,wakalishambulia bunge huku wakiwa na ujumbe kwa wabunge kwa kuimba “jiuzulu,jiuzulu”, kwa mujibu wa taarifa ya ashirika la habari la AFP.
Bunge la nchi ya Libya limeshambuliwa mara kadhaa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Nuri Abu Sahmein ambaye ni spika wa bunge hilo aliambia kituo cha televisheni cha Al-Nabaa kuwa maandamano yaliyokuwa ya amani, yalivurugwa na watu waliojihami.
"Wabunge wawili walipigwa risasi pale walipojaribu kutoweka mahali hapo kwa kutumia magari yao,” alisema.
Haikuwezakana kubaini papo hapo idadi ya wabunge walioumia.
Picha zilizotumwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha waandamanaji wakivuta kile kilichokusudiwa kuwa kiti cha Spika wa bunge hilo nje ya bunge na kukichoma.
Mwandishi wa BBC Rana Jawad ambaye yuko Tripoli anasema kuwa bunge la Libya limeshambuliwa mara kadhaa na makundi tofauti, yakiwemo makundi ya waasi katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Uchaguzi uliokuwa wa amani ulifanywa na nchi ya Libya katika mwezi wa Julai mwaka jana, ila bado nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika ingali inang’ang’ana kupata utulivu, miaka mitatu baadaye tangu kufurushwa kutoka maamlakani kwa aliyekuwa rais, hayati Muammar Gaddafi.

 

Kirusi bwete chazinduka

Taarifa ya kirusi aina ya Pithovirus sibericum ambacho kimekuwa bwete kwa miaka zaidi ya 30,000 hadi kilipopelekwa tena kwenye mabara nchini Ufaransa imeendelea kuwa taarifa kuu.

kirusi cha Pithovirus sibericum 

Kirusi hicho cha kale kimerejesha uhai wake baada ya kukaa bwete kwa miaka zaidi ya elfu 30,000 , walieleza wanasayansi .
Kilipatikana kikiwa kimezama kwenye utando wa barafu katika eneo la Siberia, lakini baada ya kuzinduliwa kikawa tena na uwezo wa kusababisha maambukizi .
Wanasayansi wa Ufaransa wanasema hata hivyo kirusi hicho si hatari kwa maisha ya binadamu na wanyama , lakini hii inaonyesha kuwa virusi wengine wanaweza kuzinduka hata baada ya kuwa bwete kwa muda mrefu.
Taarifa ya utafiti huo ilichapishwa katika kituo cha kitaifa cha sayansi nchini Ufaransa (PNAS).
Professor Jean-Michel Claverie, wa kituo cha utafiti (CNRS) katika chuo kikuu cha Aix-Marseille nchini France, alisema: " Hii ni mara ya kwanza tumeona kirusi ambacho bado kina maambukizi baada ya kipindi kirefu kama hiki.
Kirusi hiki ambacho ni kikubwa kinaweza kuonekana kwa macho tofauti na virusi vingine vinavyoonekana tu kwa kutumia microscope, na kilipatikana kikiwa kimezikwa mita 30 chini kwenye barafu iliyoganda.
Wanasayansi wanasema kubainika kwa kirusi cha Pithovirus sibericum kunaonyesha hatari kwamba virusi vya maambukizi vinavyodhaniwa kuwa vimekufa vinaweza kuibuka tena baada ya miaka mingi na kusababisha maambukizi kutokana na shughuli za binadamu.