Wana-CCM Dodoma waonya wajumbe
Dodoma. Chama cha Mapinduzi, Kata ya Chang’ombe katika Manispaa
ya Dodoma kimeonya kuwa Katiba mpya isipotoa matumaini ya wananchi
kupimiwa ardhi, hawataitambua na hawatakuwa tayari kupiga kura ya
kuchagua kiongozi yeyote katika maeneo yao.
Wanachama wa chama hicho walitoa kauli hiyo katika kikao chao kilichofanyika Tawi la Mji Mwema.
Walisema Serikali kupitia Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) imewahadaa na kwamba matumaini yao sasa yako ndani ya Katiba.
Wananchi hao pia waliushutumu uongozi wa CCM wa Mkoa wa Dodoma kwa madai ya kushirikiana na CDAkuwanyima haki zao.
Hata hivyo, Katibu wa CCM wa Mkoa wa Dodoma,
Albert Mgumba alikanusha madai hayo na kueleza kwamba chama hicho
kinafanya kila njia kupigania haki za wananchi hao.
Mgumba alisema mfumo wa CDA ndiyo tatizo kubwa na kwamba hiyo inachangiwa na muundo wake.
Mwenyekiti wa CCM wa Tawi la Mji Mwema, Hussein
Binde alisema wamekuwa wakidanganywa kuwa watapimiwa ardhi yao lakini
hakuna kilichofanyika.
No comments:
Post a Comment