Saturday 12 April 2014

JINSI MAFURIKO YANAVYOLITESA JIJI LA DAR..ANGALIA PICHA 

Raia wa Guinea Bissau kuchagua rais mpya


Uchaguzi wa urais na maeneo bunge unafanyika katika taifa dogo la afrika magharibi Guinea Bissau.
Ni uchaguzi wa Kwanza tangu kufanyika kwa mapinduzi miaka miwili iliopita -ikiwa ni hatua ya hivi karibuni ya kijeshi ambayo imesaidia kuhakikisha kwamba hakuna raisi aliyechaguliwa ambaye amefanikiwa kuiongoza Guinea Bissau kwa kipindi chote alichochaguliwa tangu taifa hilo lijipatie Uhuru wake kutoka kwa Ureno mnamo mwaka 1974.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Antonio Indjai aliikabidhi mamlaka serikali ya raia mnamo mwaka 2012 iliopewa wajibu wa kuandaa Uchaguzi huo.
Indjai alifunguliwa mashtaka nchini marekani kwa madai ya kufanya biashara ya mihadarati pamoja na kuwauzia silaha waasi wa Colombia.Wagombea 13 wanawania wadhfa wa urais.
Iwapo mmoja wao hatashinda kwa wingi wa kura basi uchaguzi huo utaenda kwa awamu ya pili mnamo mwezi May.

Boko Haram ladaiwa kuwaua watu laki moja

Sasa imebainika kuwa wanamgambo wa kiislamu kazkazini mwa Nigeria wamewaua zaidi ya watu laki moja na arubaini na tano katika misururu ya mashambulizi juma lililopita.
Sineta wa jimbo la kazkazini mashariki la Borno Ahmed Zannah ameiambia BBC kwamba mauaji hayo yalifanyika katika maeneo matatu tofauti yaliopo mashambani.
Amesema kuwa taassi moja ya kutoa mafunzo ya elimu ndio iliokuwa ya kwanza kulengwa ambapo wanamgambo hao waliwaua walimu watano kabla ya kuwatekanyara wake zao kadhaa.
Wapiganaji hao wanaoshukiwa kutoka katika kundi la wanamgambo wa Boko haram baadaye walivamia vijiji viwili katika eneo la mashambani karibu na mpaka na Cameroon.

Iran haitabadili balozi wake katika UN

Abutalebi

Makamo wa waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Iran amesema nchi yake haifikirii kumteua mtu mwengine kuiwakilisha nchi katika Umoja wa Mataifa.
Taarifa iliyotolewa na Abbas Araqchi imesema Iran itatumia sheria kupinga uamuzi wa Marekani wa kumkatalia visa Hamid Abutalebi kuingia Marekani, ili kuwa mwakilishi mpya wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York.
Bwana Abutalebi amehusishwa na kundi lilovamia ubalozi wa Marekani mjini Teheran mwaka wa 1979, na nchini Marekani baadhi ya wanasiasa wamepinga vikali uteuzi wa mwanabalozi huyo.
Marekani haikuwahi kumkatalia visa mwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wenye makao yake makuu mjini New York.