Saturday, 12 April 2014
Raia wa Guinea Bissau kuchagua rais mpya
Uchaguzi wa urais na maeneo bunge unafanyika katika taifa dogo la afrika magharibi Guinea Bissau.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Antonio Indjai aliikabidhi mamlaka serikali ya raia mnamo mwaka 2012 iliopewa wajibu wa kuandaa Uchaguzi huo.
Indjai alifunguliwa mashtaka nchini marekani kwa madai ya kufanya biashara ya mihadarati pamoja na kuwauzia silaha waasi wa Colombia.Wagombea 13 wanawania wadhfa wa urais.
Iwapo mmoja wao hatashinda kwa wingi wa kura basi uchaguzi huo utaenda kwa awamu ya pili mnamo mwezi May.
Boko Haram ladaiwa kuwaua watu laki moja
Sasa imebainika kuwa wanamgambo wa kiislamu kazkazini
mwa Nigeria wamewaua zaidi ya watu laki moja na arubaini na tano katika
misururu ya mashambulizi juma lililopita.
Sineta wa jimbo la kazkazini mashariki la Borno
Ahmed Zannah ameiambia BBC kwamba mauaji hayo yalifanyika katika maeneo
matatu tofauti yaliopo mashambani.Amesema kuwa taassi moja ya kutoa mafunzo ya elimu ndio iliokuwa ya kwanza kulengwa ambapo wanamgambo hao waliwaua walimu watano kabla ya kuwatekanyara wake zao kadhaa.
Wapiganaji hao wanaoshukiwa kutoka katika kundi la wanamgambo wa Boko haram baadaye walivamia vijiji viwili katika eneo la mashambani karibu na mpaka na Cameroon.
Iran haitabadili balozi wake katika UN
Makamo wa waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Iran
amesema nchi yake haifikirii kumteua mtu mwengine kuiwakilisha nchi
katika Umoja wa Mataifa.
Taarifa iliyotolewa na Abbas Araqchi imesema
Iran itatumia sheria kupinga uamuzi wa Marekani wa kumkatalia visa Hamid
Abutalebi kuingia Marekani, ili kuwa mwakilishi mpya wa Iran katika
Umoja wa Mataifa mjini New York.Bwana Abutalebi amehusishwa na kundi lilovamia ubalozi wa Marekani mjini Teheran mwaka wa 1979, na nchini Marekani baadhi ya wanasiasa wamepinga vikali uteuzi wa mwanabalozi huyo.
Marekani haikuwahi kumkatalia visa mwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wenye makao yake makuu mjini New York.
Subscribe to:
Posts (Atom)