Saturday 12 April 2014

Iran haitabadili balozi wake katika UN

Abutalebi

Makamo wa waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Iran amesema nchi yake haifikirii kumteua mtu mwengine kuiwakilisha nchi katika Umoja wa Mataifa.
Taarifa iliyotolewa na Abbas Araqchi imesema Iran itatumia sheria kupinga uamuzi wa Marekani wa kumkatalia visa Hamid Abutalebi kuingia Marekani, ili kuwa mwakilishi mpya wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York.
Bwana Abutalebi amehusishwa na kundi lilovamia ubalozi wa Marekani mjini Teheran mwaka wa 1979, na nchini Marekani baadhi ya wanasiasa wamepinga vikali uteuzi wa mwanabalozi huyo.
Marekani haikuwahi kumkatalia visa mwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wenye makao yake makuu mjini New York.

No comments:

Post a Comment