Tuesday 25 February 2014

Wasiwasi wa Ukraine kusambaratika

Rais wa mpito wa Ukraine, Olexander Turchynov, ameonya kuhusu tisho la kusambatarika kwa nchi hiyo kufuatia kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais,

 

 

 

 

 

 

 

Rais wa mpito Olexander Turchynov asema tangazo litatolewa Alhamisi

Viktor Yanukovych.
Matamshi yake yanakuja wakati ambapo upinzani ukitokota katika maeneo ya Ukraine ambapo Kirusi kinazungumzwa dhidi ya serikali ya mpito.
Bunge la Ukraine limechelewa kuiunda serikali ya mseto.
Tangazo lilitarajiwa siku ya Jumanne kufuatia kung'atuliwa mamlakani aliyekuwa Rais Viktor Yanukovych, lakini Rais wa mpito Olexander Turchynov, amesema kuwa litatolewa siku ya Alhamisi ili kuruhusu mashauriano kuendelea.
Turchynov ameelezea wasiwasi wake kwa kile alichokitaja kama hatari ya kugawanyika kwa baadhi ya maeneo nchini Ukraine.
Kumetolewa waranti ya kukamatwa Yanukovych kwa madai ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji, lakini hajulikani aliko.
Wanadiplomasia wakuu wa Umoja wa Ulaya wanakutana katika mji mkuu Kiev kujadili usaidizi wa kifedha kwa serikali ya mpito, huku nchi hiyo ikitishiwa na mdororo wa kiuchumi kufuatia maandamano ya miezi mitatu.
Jumuiya ya Kimataifa
Kumekuwa na wasiwasi katika jumuiya ya kimataifa kuwa huenda Ukraine ikagawanyika mara mbili; upande mmoja ukiwa karibu na Umoja wa Ulaya, na mwingine ukiegemea upande wa Urusi.
 
Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza, William Hague, anasafiri kwenda Washington-Marekani, kulijadili suala hili.
Katika taarifa aliyoitoa bungeni, alisema kuwa Ukraine inahitaji msaada wa dharura wa fedha wa kimataifa ili kuimarisha uchumi wake unaozorota.
Ingawa kumekuwa na msimamo mkali kutoka kwa Urusi, Hague, amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa Umoja wa Ulaya na Urusi kufanya kazi pamoja.
Hague alisema, 'Azimio letu kuu ni kuendeleza demokrasia, kutetea haki za kibinaadam, na kufuatwa kwa sheria nchini Ukraine.
Hii sio kuhusu uamuzi wa Ukraine kuchagua kati ya Umoja wa Ulaya ama Urusi. Ni kuhusu kuielekeza nchi hiyo katika njia ya kidemokrasia katika siku zijazo'.

Wanamgambo waua wanafunzi Nigeria

Wanamgambo wa Kiislam wa kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria wametuhumiwa kushambulia shule moja na kuwaua wanafunzi kadhaa.
Polisi nchini Nigeria wameliambia Shirika la Habari la Uingereza, Reuters kwamba wote waliouawa ni wavulana na kwamba baadhi ya miili ya wanafunzi hao imeungua na kubaki majivu.
\
Taarifa ya jeshi la Nigeria imesema shambulio hilo limefanyika katika jimbo la Yobe.
Wakaazi wa mji wa Buni Yadi katika jimbo hilo, wamesema washambuliaji hao walivamia usiku na kuwachinja baadhi ya wanafunzi.
Wamesema baadhi waliuawa kwa kupigwa risasi.
Walimu katika chuo cha serikali ya shirikisho katika mji wa Buni Yadi wameliambia shirika la habari la AP kwamba wanafunzi wapatao 40 waliuawa katika shambulio hilo ambalo lilianza mapema Jumanne asubuhi.
Jeshi limethibitisha kwamba shambulio hilo limetokea katika hosteli za wanafunzi lakini limesema haliwezi kutoa taarifa zaidi kwa sasa.
Kundi la Boko Haram limekuwa likishutumiwa kuendesha vitendo vya mauaji kaskazini mwa Nigeria, yakiwemo mauaji ya mapema mwezi huu katika jimbo la Yobe.
Boko Haram, lina maana ya"Elimu ya Magharibi ni dhambi" katika lugha ya Kihausa, mara kwa mara limekuwa likishambulia shule katika siku za nyuma.
Watu kadhaa wameuawa katika mashambulio mawili yaliyotokea wiki iliyopita. Katika tukio moja, wanamgambo hao wa Boko Haram, waliteketeza kijiji kizima na kuwapiga risasi wakaazi wa eneo hilo waliokuwa wakijaribu kutoroka.

Msaada wa Marekani kwa Uganda

   

John Kerry asema Uganda inakiuka haki za binaadamu

Marekani haikufurahishwa na hatua ya Uganda kuidhinisha sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.
Waziri wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema tangu Uganda iidhinishe mswada huo miaka minne iliyopita, Marekani ilieleza wazi kwamba sheria hiyo inakiuka jukumu la kuhakikisha kuwepo haki za binaadamu ambalo tume ya haki za binaadamu Uganda inatambua linaambatana na sheria ya Uganda.
Kerry amesema,' Baada ya kuidhinishwa sheria hii, tunaanza ukaguzi wa ndani wa uhusiano wetu na serikali ya Uganda, kuhakikisha kwamba pande zote za uhusiano wetu, ukiwemo miradi ya msaada, zinapinga sera na sheria zinazowaonea watu na tuwe na uhusiano unaodhihirisha maadili yetu'.

Tamko hilo limetolewa siku moja baada ya rais Yoweri Museveni kukaidi shinikizo la kimataifa na kutia saini sheria hiyo iliyo zusha mzozo, inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja Uganda, hatua iliyozusha hisia kali.
Baadhi ya mataifa ya magharibi tayari yanatishia kukatiza msaada wa moja kwa moja kwa serikali ya Uganda.

Marekani inasema kuidhinishwa kwa sheria hiyo kunatishia hatari ya kurudi nyuma katika uwajibikaji wa Uganda kulinda haki za raia wake na kutishia jamii ya wapenzi wa jinsia moja Uganda.


WHY TANZANIA WILL SOON OVERTAKE KENYA IN CREATING MILLIONAIRES 

  

Tanzania is creating dollar millionaires faster than any other East African country, a new report says.
This means that East Africa’s newest millionaires are likely to come from Tanzania, as opposed to Kenya, Uganda, Rwanda or Burundi.

According to the African 2013 Wealth Book, the country is ranked third in Africa, after Ethiopia and Angola, with its millionaires’ club growing at a rate of 51 per cent between 2007 and 2013.

While it had 3,700 millionaires in 2007, this number had risen to 5,600 by 2013. Tanzania is followed in the region by Kenya, the only other regional country that features among the top 10 in Africa. Kenya is reported to have had 8,300 millionaires in 2013 against 6,700 in 2007, a growth rate of 24 per cent.

The report, put together by New World Wealth, defines millionaires or high net worth individuals (HNWIs) as those with net assets worth $1 million or more, excluding the value of their primary residences. The survey includes only those countries that had over 800 millionaires in 2013.

On the scale of absolute numbers, Kenya is up there, mixing it up with Africa’s big boys, coming fourth after South Africa (48,700), Egypt (22,800) and Nigeria (15,700).

Tanzania’s faster acceleration must be understood in the context of a country that is coming from a low base.

After decades of a command economy in which the government controlled most of the wealth, the liberalised economy is just warming up and the risk-takers among the population are clearly cashing in. Tanzania is also more resource-rich than its EAC partners.

It is endowed with vast natural gas and oil deposits, besides substantial quantities of gold, diamond and tanzanite. It also has the region’s biggest water and forest resources and is often referred to as the “lungs of the region.”

Thus the newly created millionaires probably individuals who have bet their money on its rapidly developing oil, gas and minerals sector, where massive deposits of offshore gas have made Tanzania a leading investment destination for prospectors and developers. As of June 2013, 42.7 trillion cubic feet of natural gas (about 7.5 billion barrels of oil equivalent) has been discovered in Tanzania.

Tanzania’s gold sector has also witnessed a boom in the past few years, and it is now the country’s leading export, worth $2.2 billion in 2012, followed by tobacco exports at $223 million and coffee at $187 million.

It recorded a growth of 45 per cent between 2007 and 2012 against Kenya’s 20 per cent. Even then, Kenyans were generally richer than their Tanzanian counterparts at a per capita income of $862 against the latter’s $609 in 2012.

In average terms, the richest Africans are to be found in South Africa ($7,508 per capita income), Angola ($5,485), Algeria ($5,404), Tunisia ($4,237) and Egypt ($3,187). While South Africa is known to have a resource-rich and fairly sophisticated economy, Angola is the beneficiary of its oil. The Maghreb countries’ good fortune is a result of a mix of oil and “welfarist” public policies.

Uganda leads the pack in expanding individual wealth in the region. Closer home, Kenya is expected to have 21,200 dollar millionaires, compared with Tanzania’s 15,200.

Mugabe Aikosoa Afrika kwa Kukosa Shukrani kwa Nyerere...SOMA ZAIDI!

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amesema kushindwa kwa viongozi wa Afrika kumuenzi Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere kwa mchango wake katika ukombozi wa Afrika ni jambo la kufedhehesha.

 Mugabe 

Rais Robert Mugabe
Kiongozi huyo mwenye miaka 90, alikuwa akiongea kwenye sherehe yake ya kuzaliwa iliyofanyika Jumapilii hii nchini Zimbabwe muda mfupi baada ya kuwasili kutoka Singapore alikoenda kufanyiwa upasuaji wa macho. Alisema viongozi wa Afrika wanapaswa kufanya zaidi kumuenzi Hayati Mwalimu Nyerere aliyeifanya Tanzania kimbilio la vuguvugu la ukombozi barani. Nyerere alikuwa na mchango mkubwa kwa kukamata madaraka kwa Mugabe.
Mwalimu Nyerere enzi za Uhai wake 
Mwalimu Nyerere enzi za Uhai wake
Maelfu wa wananchi wa Zimbabwe walijitokeza kwenye uwanja wa Marondera kwenye sherehe hiyo inayodaiwa kugharimu dola milioni 1 za Kimarekani

Mugabe Aelezea Heshima anayonyimwa Nyerere.

“Nataka kusema, wakati ambapo heshima zimekuwa zikimwagwa kwa mashujaa wa Afrika, mtu anayeonewa ni Mwalimu Julius Nyerere,” alisema Mugabe. “Hapa tulipo, vuguvugu za ukombozi, kule tulikokuwepo – tulitegemea msaada wa Tanzania. Lakini hakuna kinachosemwa kuhusu mtu huyu na nchi yake kwenye Jumuiya ya Afrika.”
Mugabe ambaye ni makamu mwenyekiti wa AU, alisema bara la Afrika linapaswa kukumbushwa fadhila inazotakiwa kumlipa Mwalimu Nyerere.
“Nataka sisi Wazimbabwe, kusimama kwaajili ya Nyerere. Afrika inatakiwa kukumbushwa wajibu iliomtupia mtu huyu, mzigo wa kuendesha vuguvugu zote za ukombozi,” alisema. “Mwisho wa siku, hakuna hata mmoja anayesema Tanzania ilistahili japo kutajwa tu kwa kufanikisha mission hii, mission ya kuwa nasi kama marafiki, mission ya kutufanya tuendeshe vuguvugu za ukombozi wa Afrika. Wote tulienda kwa njia tofauti, kwa sura tofauti hadi Tanzania kukomboa nchi zetu na hatujaenda tena Tanzania. Well, naenda kuwa mwenyekiti wa AU, ntashughulikia suala hili,” alisema.
“Hakuna aliyetambua kile Nyerere alichokifanya. Sisi wa Wazimbabwe sio wachoyo wa shukrani, ni taifa lenye shukrani na tutamuenzi mtu huyu.”

 

Watoto milioni moja wauawa katika Vita

 
Watoto wateseka kutoka na vita  
Watoto Milioni moja hufa siku yao ya Kuzaliwa
Shirika la Misaada kwa watoto, Save the Children, linasema kuwa watoto milioni moja hufariki dunia kila mwaka katika siku yao ya kwanza ya maisha.
Katika ripoti mpya ya shirika hilo la misaada kwa watoto linasema vifo vya watoto wachanga vimesalia kuwa moja ya aibu za dunia ya sasa.
Hali ya watoto ni mbaya zaidi hasa katika mataifa yanayokabiliwa na mizozo.
Mwandishi wa BBC aliye Sudan Kusini, Anne Soy, amesema kuwa katika mazingira ya sasa ya Sudan Kusini, watoto na wanawake, hasa wale waja
wazito wanaokabiliwa na athari nyingi za vita vinavyoendelea nchini humo.
Amesema kuwa kutokana na vita watoto, walioandamana na wazazi wengine wakiwa pekee, wanaungana na akina mama kutembelea mwendo
mrefu ili kujiepusha na vita vya kikabila vinavyoendelea nchini.
Miundo msingi katika Sudan Kusini, kama vile hospitali ni chache sana jambo ambalo linatatiza maisha ya wanawake na watoto.
Katika hospitali ya mji wa Nimule kwenye mpaka wa Sudan Kusini na Uganda Kuna vitanda 174 pekee hospitalini idadi ambayo haiafikiana kamwe
na maelfu ya wagonjwa na wahasiriwa wa vita .
Save the children inasema kuwa vita vinawaathiri zaidi watoto huko Syria, Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la Save the Children linasema kuwa vifo hivi vingi vinaweza kuzuiliwa.


WAZIRI MKUU AKIWA NA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOMA LEO


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. Kulia ni mbunge wa Sumve Richard Ndassa.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014.

  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Singida Magharibi Mohamed Bissanga na Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa ,wote wakiwa ni wabunge wa Bunge Maalum la Katiba, nje ya ukumbi wa Bunge Mjiji Dodoama Februari 24, 2014.

 

 Waziri Mkuu, Mizengo, Pinda akizungumza na Katibu wa Bunge, Thomas Kashilillah, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. (Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)

SIKU TATU ZA CHADEMA WALIZOMPA RAIS KIKWETE ZIMEISHIA WAPI ?

 

Chadema kupitia kigaila walitoa siku tatu kwa rais afute kauli yake kuwa uvumilivu kwa wanaccm sasa basi. Leo ni zaidi ya wiki moja, aona kimya. Vipi, wamesahau? Hawana la kumfanya? Wamesalimu amri? Wamemuogopa? Tunaomba mrejesho wa kinachoendelea.