Monday 24 February 2014

Ajali mbaya Yatokea eneo la Mikese, Morogoro, leo Asubuhi

 

 

Ankle habari. Leo asubuhi eneo la Mikese, Morogoro, tumekutana na na ajali  mbaya sana ya magari mawili, moja la mafuta, kugongana uso kwa uso na kutumbukia mtaroni na yote kushika moto. Inasadikiwa mtu mmoja ambaye ni dereva wa magari hayo kateketea kabisa kwa moto. 


 

Hakuna cha kufanyika kutokana na moto mkubwa na moshi mwingi wakati magari hayo yakiteketea

 

 

Mlipuko mkubwa wakati matenki ya mafuta yakilipuka

Askari wa kikosi cha zimamoto wakijaribu kuuzima moto huo.Picha na Mdau Sixmund

TANZANIA KUPELEKA MAJESHI SUDAN KUSINI 

 Mzinga 3c649

Serikali inatarajia kupeleka kikosi kimoja cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huko Sudan Kusini kwa ajili ya kulinda amani kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe anasema Dar es Salaam jana kwamba Serikali imekubali kupeleka batalioni moja baada ya kuombwa na Umoja wa Mataifa (UN).
Sudan ya Kusini imekuwa katika machafuko ambayo yamesababisha vifo vya mamia ya raia na wengine kujeruhiwa.
"Tumefanya uamuzi wa kupeleka majeshi yetu Sudan Kusini, tumefanya hivyo baada ya kuombwa na Umoja wa Mataifa kwa sababu ya ubora wa jeshi letu," Membe aliwaambia waandishi wa habari.
Anasema jukumu la kulinda amani katika Bara la Afrika ni la Waafrika wenyewe na kwamba Tanzania inajiona kwamba ina jukumu la kusaidia kupatikana kwa amani.
Anasema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon alimwomba Rais Jakaya Kikwete kusaidia kupeleka majeshi yake Sudan Kusini kusaidia kulinda amani. "Rais alikubali, sasa tuko kwenye maandalizi, nadhani Aprili jeshi letu litaondoka kuelekea Sudan Kusini," alisema Membe.

Kwa sasa Tanzania ina vikosi vya wanajeshi wa kulinda amani katika nchi za DRC, Darfur (Sudan) na Lebanon. Chanzo: mwananchi


MKUU WA MKOA WA NJOMBE ACHEFULIWA NA VYOO VYA MAKETE 

 

Tabia ya wakazi wengi wa wilaya ya Makete mkoani Njombe kujenga vyoo vidogo kiasi cha watumiaji kupata shida kuingia kujisaidia, imemchefua mkuu wa mkoa huo wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo hivi karibuni

Akizungumza wilayani hapa mkuu wa mkoa wa Njombe Kapt. Aseri Msangi amesema anakerwa na tabia ya wananchi wa makete wanaojenga vyoo vidogo hali inayosababisha kero kwa watumiaji kutokana na kupata shida tangu anapoingia hadi kutoka

 Mimi nashangaa kabisa badala ya mtu kujenga choo kikubwa kitakachopelekea mtu kujisikia nafuu anapoingia kujisaidia nyie mnajenga choo ambacho mtu akiingia kwanza anainama, na pili hawezi kugeuka akiingia, yaani akiingia kwa mbele anarudi kinyume nyume" alisema Msangi


Ametoa wito kwa wananchi hao kujenga vyoo vikubwa na vyenye ubora kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza magonjwa ya matumbo ambayo yanawakumba wananchi wengi na uchunguzi kubaini kuwa ni kutokana na kukosekana kwa vyoo bora vinavyotunzwa vizuri

Taswira,Bomoabomoa Inayoendelea Jiji la Arusha

 

 

 

 

Halmashauri aya Jiji la Arusha imevunja nyumba zake338 baada ya kushinda kesi iliyofunguliwa na wapangaji Sangito Sumari na wenzake 216 katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Arusha.

Operesheni hiyo inayojulikana kama “Operesheni Mongela”ilianza saa 12 asubuhi jana kwa kuvunja nyumba 56 eneo la Kilombero, nyumba 198 eneo la Kaloleni na nyumba 84 katika eneo la Themi.

Wengi walitegemea kuibuka vurugu wakati wa uvunjaji nyumba lakini hadi mchana hapakuwa na pingamizi kwa wapangaji badala yake wenyewe walihamisha vitu vyao mapema jana asubuhi kabla ya zoezi la kuvunja kuanza.

Hata hivyo kuvunjwa kwa nyumba hizo kumeleta neema kwa baadhi ya watu wakiwamo vijana wanaokusanya vyuma chakavu kuvamia maeneo hayo na kuokota kila aina ya chuma au kitu ambacho waliamini kinaweza kuuzwa na kuwapatia fedha.

Akiwa eneo la Kaloleni baada ya kukamiliza kuvunjwa nyumba za Kilombero, Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mongela alisema, ‘Operesheni Mongela’ ilipata baraka zote za viongozi wa Serikali wanasiasa wakiwamo madiwani wote Mbunge na Meya wa Jiji.