Monday 24 February 2014

MKUU WA MKOA WA NJOMBE ACHEFULIWA NA VYOO VYA MAKETE 

 

Tabia ya wakazi wengi wa wilaya ya Makete mkoani Njombe kujenga vyoo vidogo kiasi cha watumiaji kupata shida kuingia kujisaidia, imemchefua mkuu wa mkoa huo wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo hivi karibuni

Akizungumza wilayani hapa mkuu wa mkoa wa Njombe Kapt. Aseri Msangi amesema anakerwa na tabia ya wananchi wa makete wanaojenga vyoo vidogo hali inayosababisha kero kwa watumiaji kutokana na kupata shida tangu anapoingia hadi kutoka

 Mimi nashangaa kabisa badala ya mtu kujenga choo kikubwa kitakachopelekea mtu kujisikia nafuu anapoingia kujisaidia nyie mnajenga choo ambacho mtu akiingia kwanza anainama, na pili hawezi kugeuka akiingia, yaani akiingia kwa mbele anarudi kinyume nyume" alisema Msangi


Ametoa wito kwa wananchi hao kujenga vyoo vikubwa na vyenye ubora kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza magonjwa ya matumbo ambayo yanawakumba wananchi wengi na uchunguzi kubaini kuwa ni kutokana na kukosekana kwa vyoo bora vinavyotunzwa vizuri

No comments:

Post a Comment