Thursday 27 March 2014

ANGALIA PICHA ZA KUTISHA WATU WANAVYOJICHUKULIA SHERIA MKONONI


 KUMRADH kwa picha mbaya na za kutisha.Tunaungana na Jeshi la Polisi nchini kupinga unyama huu wanaofanyiwa binadamu wenzetu licha ya kwamba wanakuwa waharifu hii ni kosa kisheria.


I

Bei ya gesi kupanda maradufu Ukraine

Serikali ya mpito ya Ukraine imesema itaongeza bei ya gesi kwa watumiaji wa ndani kwa asilimia 50 zikiwa jitihada za kuhakikisha kuwa wanafanikiwa kupata mkopo kutoka Shirika la fedha duniani, IMF

 

Shirika la taifa la nishati ya gesi, Naftogas limetangaza nyongeza ya gharama hizo kuanza kutekelezwa tarehe mosi mwezi Mei.
Ukraine hununua gesi nusu ya gesi yake ya asili kutoka kampuni ya Gazprom ya Urusi, kisha huiuza kwa watumiaji wake kwa gharama nafuu.
IMF halikadhalika inaitaka Ukraine kupambana na vitendo vya rushwa na kusitisha mchakato wa Benki kuu ya Ukraine kusaidia fedha ya nchi hiyo.
Siku ya jumanne, waziri wa fedha wa nchi hiyo Olexander Shlapak alisema Ukraine inahitaji kiasi cha Pauni bilioni 9-12 kutoka kwa IMF.
Jarida la Financial Times limeripoti kuwa uamuzi uko mbioni kufikiwa kuhusu kiasi cha fedha cha takriban dola za kimarekani bilioni 15
ambacho Ukraine inatakiwa kujiokoa na kwamba maamuzi hayo yatatangazwa rasmi Alhamisi.
Makubaliano kati ya Ukraine na IMF ni muhimu wakati huu ili kuweza kupata misaada zaidi kutoka kwa Jumuia ya Ulaya na Marekani.
Msaada wa kifedha unahitajika haraka wakati nchi hiyo ikiwa imelazimika kutumia hifadhi ya fedha za kigeni,huku uchumi nao ukitarajiwa kuanguka kwa 3% mwaka huu.
Wizara ya fedha nchini humo pia inatarajia msaada kutoka kwa Marekani japo kiasi kamili kinasubiri mjadala na bunge la Congress.

 

Rais Uhuru na naibu wake walipoamua kusimamisha msafara ili kula.

 Screen Shot 2014-03-27 at 12.06.56 PM 

Ni picha ambayo nimetumiwa na Mwandishi wa habari wa Kenya ikimuonyesha Uhuru Kenyatta ambae ni Rais wa nchi hiyo akiwa na naibu wake William Ruto baada ya kuamua kusimama njiani wakitokea Arusha kwa gari na kula chakula chini ya mti Kajiado.

Rais Uhuru ameripotiwa kufanya mambo kadhaa ambayo hayajawahi kufanywa na Marais wengine wa nchi hiyo likiwemo la kutembea Nairobi bila msafara ambapo hivi juzi kuna video ilitoka ikidaiwa kumuonyesha Rais huyo akinunua karanga kutoka kwa watoto barabarani Nairobi.
Hii picha ya leo hapo juu inadaiwa ni msafara wake uliosimama na kula chakula wakati akitokea Arusha Tanzania kwenye mkutano ambapo alitumia usafiri wa gharama nafuu (gari) na kuendeshwa kutoka Nairobi, siku kadhaa tu baada ya nchi hiyo kutangaza kuvunja safari za nje ya nchi za viongozi wa serikali zisizo za lazima ili kuokoa matumizi makubwa ya fedha.
Ni siku kadhaa pia baada ya Rais huyu kutangaza maamuzi ya kupunguza mshahara wake, naibu wake, Mawaziri na hata wakuu wa mashirika ya umma nchini humo.
Screen Shot 2014-03-27 at 12.52.17 PM

 

Tazama jinsi fundi alivyookolewa dakika za mwisho kwenye jengo lililowaka moto

Screen Shot 2014-03-27 at 12.14.25 PM 

Ni moto ambao umetokea kwenye gorofa ya tano ya jengo moja huko Houston Texas Marekani ambapo kikosi cha zimamoto kilifanya pia jitihada za kumuokoa fundi ujenzi mmoja aliekua kwenye gorofa hilo dakika za mwisho wakati moto umeshashika.

Screen Shot 2014-03-27 at 12.14.39 PM

 

Kuna njama kuvuruga Bunge

a Uvumilivu una mwisho wake, ukifika wakati huo tutawaambia Watanzania nini kinachoendelea na sisi tunakusudia kufanya kitu gani.

Dodoma/Dar. Kuna njama. Maneno haya mawili ndiyo yametumiwa na pande mbili zinazopingana ndani ya Bunge Maalumu la Katiba, kuelezea hali iliyojitokeza jana wakati wa kikao cha Bunge hilo kuhusu mvutano wa mabadiliko ya kanuni.
Njama zinazoelezwa na pande hizo ni za kuvuruga mchakato wa Katiba Mpya, zikirejea yaliyotokea jana jioni ikiwamo zomeazomea hali iliyomlazimu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta kuliahirisha Bunge hadi leo jioni.
Baada ya kuahirisha Bunge hilo, Sitta alikutana na waandishi wa habari na kusema kwamba kuna njama za baadhi ya wanasiasa kutumia vurugu kuhujumu mchakato wa upatikanaji wa Katiba, badala ya kujenga hoja.
Bila kuwataja wanasiasa hao, Sitta alisema ikiwa hawataki kuendelea na mchakato huo, basi waondoke na kuwaacha wenye nia njema.
“Wanasiasa hawa wamedhamiria kuvuruga mchakato wa Katiba, tuhuma ambazo tumetuhumiwa leo na Lissu (Tundu) ni uongo na uzushi, mimi sihusiki na kupeleka marekebisho ya kanuni kwenye Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge,” alisema Sitta.
Sitta alikuwa anajibu mchango wa mjumbe wa Bunge, Tundu Lissu alioutoa mapema kwenye kikao cha jioni, akipinga kilichoelezwa ni njama za kutaka kubadili kanuni kinyemela ili kumsaidia mwenyekiti kulidhibiti Bunge.
Sitta alisema kwa kuzingatia kanuni ya 59 (1), Kamati ya Uongozi ina mamlaka ya kupeleka marekebisho ya kanuni ili kuliwezesha Bunge kufanya kazi vizuri.
Alisema hoja kwamba haiwezekani kufanyika mabadiliko hata kabla ya kuanza kutumika kanuni, siyo ya msingi kwani kila kitu kinabadilika kutokana na mazingira yake.
“Kamati ya Uongozi ndiyo ilipeleka waraka wa mabadiliko ya kanuni kwa Kamati ya Kanuni na Haki kwa kuzingatia kanuni, lakini hata kabla ya kujadiliwa na kamati husika inaonekana kuna wajumbe ndiyo wameichukua na kuifikisha bungeni,” alisema Sitta.
Alisema kwa kiasi kikubwa marekebisho ambayo yangesomwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Pandu Ameir Kificho, yalilenga kutoa ufumbuzi wa kanuni ya 37 na 38 juu ya upigaji kura ama uwe wa wazi au siri.
Sitta alisema pamoja na hilo, kulikuwa na marekebisho ya msingi kama kuweka utaratibu mzuri wa majadiliano katika kamati pia kuweka utaratibu wa vikao vya Bunge kuanzia Jumatatu hadi Jumapili.
“Mengi ambayo alikuwa anayasema Lissu kama ni takataka hayakuwapo katika taarifa ya Kificho,” alisema Sitta.

 

 

Rais akistaafu afutiwe kinga’

 

Dar es Salaam. Wakati Bunge la Katiba likiwa bado halijaanza kujadili Rasimu ya Katiba, taasisi moja ya viongozi wa dini imetoa maoni mapya ikitaka Rais wa nchi awe tu na kinga anapokuwa madarakani, akiondoka awajibike kwa matendo yake.
Mapendekezo hayo yalitolewa Dar es Salaam jana na Baraza la Wadhamini la Taasisi ya Viongozi wa Dini Tanzania (IRCPT), lilipokutana kwa ajili ya kutafakari kwa pamoja juu ya mchakato wa Katiba Mpya.
Mkutano wa Baraza hilo linalojumuisha Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Titus Mdoe, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Musa Salum na Padri John Solomon, uliongozwa na kaulimbiu ya ‘Katiba Moja Kwa Watanzania Wote, Pamoja Tutafika’.
Mwenyekiti wa IRCPT, Jaji Mstaafu Raymond Mwaikasu alisema tafakari inahitajika kuhusu kinga ya Rais na kwamba wao wanapendekeza awe nayo anapokuwa madarakani, lakini kinga hiyo iondolewe anapoachia madaraka, ili awajibishwe pale alipokosea.
Jaji Mwaikasu alisema pamoja na kwamba waliwasilisha maoni kwa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, hatua ya sasa inawalenga watu wenye lengo la kuingia Ikulu wakiwa na mawazo ya kujinufaisha wao, ndugu, jamaa na marafiki zao badala ya kuwatumikia wananchi.
“Hili linapaswa kutazamwa kwenye Katiba yetu mpya na sisi hatutakuwa wa kwanza kufanya hivyo, ila itasaidia kuwafanya viongozi kufuata maadili na iwapo itatokea Rais kuvunja Katiba, apelekwe mahakamani na akikutwa na hatia, awajibike hata kwa kujiuzulu,” alisema Jaji Mwaikasu. Naye Sheikh Salum alisema mali zote ni miliki ya Mungu, hivyo zinapaswa kugawanywa kwa usawa na ikitokea mtu akajimilikisha ni jambo lisilokubalika, hivyo ziwepo sheria za kuwabana viongozi wa aina hiyo.
Askofu Mdoe alisema Rasimu ya Katiba ni nzuri ingawa hakuna kitu kinachokamilika kwa asilimia 100, hivyo mazuri yaboreshwe, upungufu usahihishwe na yaliyokosekana yapatiwe fursa.
Alisema malumbano yanayoendelea kwenye Bunge la Katiba hayana tija kwani yana mwelekeo wa masilahi ya kisiasa badala ya masilahi ya umma.
“Wamebadilisha hali waliyotakiwa kuwa nayo, wanarudi katika makundi hasa ya kisiasa na mijadala kuwa ya kichama zaidi, wakifika bungeni wawe wazalendo wajadili na kuacha ushabiki,” alisema Askofu Mdoe.
Muundo wa Muungano
Kuhusu mjadala wa serikali mbili au tatu, Jaji Mwaikasu alisema hauna tija isipokuwa jambo muhimu ni kujenga msingi imara wa kuheshimiwa kwa Katiba itakayopitishwa. “Tunaambiwa Katiba imevunjwa, tunafanya nini? muhimu ni kuangalia viongozi wanaohusika wanadhibitiwa vipi, vinginevyo itakuwa ni bure,” alisema.
Alibainisha kuwa tatizo Bunge la Jamhuri ya Muungano limelala na walioteuliwa kutetea wanatetea mikate yao, hivyo akapendekeza kuwapo haja ya wananchi nao kupewa meno ya kuhakikisha Katiba inalindwa, ili pale itakapothibitika Rais amevunja Katiba wachukue hatua.

 

Seif: Hatuko tayari kujadili serikali mbili

Zanzibar. Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake cha CUF hakiko tayari kujadili mfumo wa Muungano wa serikali mbili kama inavyotetewa na wabunge wa CCM na Rais Jakaya Kikwete.
Amesema tayari amewaandikia barua Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwaeleza juu ya msimamo huo.
Maalim Seif alitoa msimamo huo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.
Isitoshe, alisema CUF imebaini kuwa kuna njama za kufuta kipengele katika Katiba ya Zanzibar kinachosema; “Zanzibar ni nchi” na kwamba hiyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa kuwa Wazanzibari kamwe hawatakubali kufanya hivyo.
Maalim Seif alisema haikuwa mwafaka kwa Rais Kikwete kukosoa mapendekezo ya Rasimu ya Katiba yanayotaka mfumo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.
Alisema Jaji Warioba aliweka kando itikadi yake ya CCM katika utendaji wake kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuja na uamuzi huo kwa vile ndiyo tiba ya kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Mapendekezo yaliyowasilishwa na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya wananchi, Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili kujenga mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali tatu,” alisema Maalim Seif.
Alisema Muungano wa serikali mbili hauvumiliki na kama kuna watu wanaendelea kuutetea mfumo huo, Zanzibar inaweza kutumia sheria yake ya kura ya maoni kuwauliza wananchi wanaotaka na wasiotaka jambo hilo.
“Nimemwandikia barua Rais Kikwete, nakala nimempelekea Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, Tanzania Bara wanataka Zanzibar iondoe kifungu cha Katiba kinachosema Zanzibar ni nchi, jambo hilo halitapita...tutafanya kampeni wananchi walikatae,” alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Alisema ni jambo la kusikitisha katika hotuba yake alijisahau kama ni mkuu wa nchi na analihutubia Bunge Maalumu badala yake akaegemea kuwa mwenyekiti wa CCM.
Alisema haikuwa sahihi kutoa vitisho na kutaja ikiwa Serikali ya Muungano chini ya Serikali tatu italegalega, jeshi litachukua madaraka ya nchi.
“Rafiki na ndugu yangu Kikwete, usifikiri huu ni wakati ule wa Julius Nyerere, akisema yeye hakuna wa kumpinga. Mambo yamebadilika, usijifanye ni Nyerere mpya, hakuna atakayekusikiliza na kubabaika,” alisisitiza Maalim Seif.

Rwanda na A.Kusini kusuluhisha mgogoro

Rais Jacob Zuma wa Afrika-Kusini na Paul Kagame wa Rwanda wamekubaliana mjini Luanda Angola, kuanzisha mazungumzo ya pamoja ya kumaliza mzozo wao wa kidiplomasia

Jaribio la kumuua Kayumba Nyamwasa lilitibuka Afrika Kusini
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulianza kuzorota pale Rwanda ilipowafukuza maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini, saa chache baada ya Afrika Kusini kuwatimua wanadiplomasia watatu wa Rwanda kuondoka nchini humo karibu wiki tatu zilizopita.
Afrika Kusini ilichukua hatua hiyo baada ya nyumba ya mpinzani mmoja wa Rwanda anayeishi Afrika Kusini Kayumba Nyamwasa kushambiliwa.
Lakini Serikali ya Rwanda ilisema hatua ya kuwatimua maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini mjini Kigali ni ya haki na ilizingatia uchokozi ambao ulianzishwa na serikali ya Afrika Kusini yenyewe kwa kufukuza maafisa watatu wa ubalozi wa Rwanda.
Rwanda ilisema kuwa Afrika Kusini ndio ilianza uchokozi kwa kuwatimua mabalozi wake watatu 

Jenerali Kayumba Nyamwasa, ambaye aliwahi kuwa mkuu wa majeshi nchini Rwanda, hakuwa nyumbani wakati wa shambulio hilo.
Nyumba yake iliharibiwa huku komputa na baadhi ya nyaraka zilichukuliwa.
Mkutano wa usalama uliofanyika mjini Luanda ulijadili hali kati ya nchi hizo mbili huku viongozi hao wawili wakikikutana ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mzozo huo kutokea.
Rais Zuma alisema kuwa wamekubaliana kusuluhisha mgogoro huo na pia kupata taarifa ya pamoja ili kuweza kusuluhisha tofauti kati yao.
Kadhalika Rais Zuma aliongeza kwamba serikali yake inatekeleza wajibu wake wa kimataifa kwa kuwapa hifadhi watu wanaoomba. Viongozi hao wawili wamekubaliana kukutana kwa ajili ya kuzungumzia swala hilo baadaye.

Obama kukutana na Papa Francis


Obama Kukutana na Papa Francis

Rais Barrack Obama wa Marekani anatarajiwa kukutana na kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, katika makao yake makuu huko Vatican.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Obama kukutana na papa Francis.
Wawili hao wanatarajiwa kujadili namna ya kupunguza tofauti iliyopo kati yao katika maswala mengi mbali na kujaribu kuinua maisha ya watu maskini duniani baada ya takwimu kuonyesha kuwa tofauti ya mapato kati ya matajiri na Masiki inaendelea kupanuka .
Aidha viongozi hao wawili wanatazamiwa kujadili hali ilivyo Nchini Ukraine, na swala la upatikanaji wa amani mashariki ya kati.
Mwafaka baina ya mitazamo tata kuhusiana na maswala ya uavyaji mimba, matumizi ya dawa za kupanga uzazi na ndoa ya jinsia moja pia inatarajiwa kuwa kati ya mada itakayojadiliwa .

 

Mkuu wa Jeshi kugombea Urais Misri

 Mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi Misri, Abdul Fattah al-Sisi, ametangaza kujiuzulu jeshini ili kugombea katika uchaguzi wa urais mwezi ujao.Wagombea wote wanapaswa kuwa raia.

Akizungumza Kwenye hotuba ya Televisheni huku akiwa amevalia sare ya kijeshi Abdel Fattah El Sissi amesema yeye sio mwanajeshi tena baada ya miaka 44 na kwamba amechukua hatua hiyo ili aweze kutimiza jukumu lingine muhimu.
Ni Bayana kwana Sisi hatakua na kibarua kigumu kujipatia ushindi katika uchaguzi wa Urais. Anaungwa mkono na idadi kubwa ya raia wa Misri na hadi sasa hana wapinzani wowote.
Baadhi ya waliotaka kugombea urais wamejiondoa wakidai kwamba hawataweza kuendesha kampeni zao kwa njia huru.
Wafuasi wake Sisi wanamuona kama kiongozi imara ambaye anaweza kurejesha amani na udhabiti nchini Misri baada ya miaka mingi ya machafuko.
Wakosoaji wake wanasema ana msimamo mkali na amechangia pakubwa katika kusambaratisha na kuhujumu upinzani nchini Misri.
Mkuu huyo wa jeshi atakabiliwa na majukumu mazito ya kufufua uchumi uliofifia , kupambana na uasi na kuileta pamoja nchi iliyogawanyika. Ameahidi kutekeleza mabadiliko makubwa lakini akaonya kuwa hawezi kufanya miujiza.