Tuesday 11 March 2014

GARI LA KUBEBEA TAKA LILILOACHWA KITUO CHA GEREJI BARABARA YA MANDELA LAWA KERO KWA ABIRIA WANAOTUMIA KITUO HICHO 

 

 

Lori la kubeba taka likiwa eneo kituo cha gereji barabara ya mandela road,huku likiwa limebeba uchafu baada ya kuharibika na limekaa hapo siku mbili.

 

Huo unaonekana kwa juu ni uchafu uliooza na unatoa harufu kali kituoni hapo. eneo la kituo cha gereji mandela road 

 

Abiria wanaotumia kituo cha gereji barabara ya mandela kwa siku mbili mfululizo wamekuwa wakipata kero ya harufu kali inayosababishwa na gari ya kubebea taka iliyopaki kwenye kituo hiko.Wakiongea na mtandao wa wetu huu wa Dj sek abiria hao wamesema kwamba gari hiyo iliharibika ikiwa inaelekea kumwaga uchafu huo na wakaisogeza kituoni hapo ili waweze kuitengeneza, lakini badala yake dereva na wasaidizi wake wakaitelekeza gari iyo toka juzi.Wakiendeleaa kuongea na mtandao wetu wamesema eneo lote la kituoni hapo linatoa harufu kali ambayo ni kero kwa wao wanaosubilia usafiri eneo hilo.

Mwandishi wa blog hii nilishuhudia mwenyewe na kupiga picha pia kuonja adha ya harufu kali inayotoka kwenye gari hiyo.Manispaa ya kinondoni na wasimamizi wa usafi mnaombwa kufuatilia hili na kuweza kulitatua kwani ni kero kwa watumiaji wa kituo hiki. 

KAMPUNI YA GOOGLE YAKANUSHA PICHA YA GOOGLE MAP INAYOONESHA NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA 

KAMPUNI YA GOOGLE YAKANUSHA PICHA YA GOOGLE MAP INAYOONESHA NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA

Kampuni ya google imekanusha habari zilizotapakaa kwenye mitandao mbalimbali duniani kwa kuweka picha ya Google Map ambayo inaonesha ndege ya Malaysia Airline ikiwa imedondondoka ndani ya maji. Msemaji wa google nchini Malaysia amesema
"Yes, the images may be there, but it is not real time satellite images as the images may have provided to us several weeks or months ago," he said when contacted.
Hii imetokana na kutapakaa kwa picha inayoonesha ndege ya Malaysia Airline imedondoka kwenye maji.
Mpaka sasa meli zipatazo 40 na ndege 34 zinazunguka bahari inayizunguka maeneo ya Vietnam na Malysia wakitafuta ndege ya Malaysia Airline iliyopotea toka jumamosi.
Nchi zinazoshiriki kuitafuta ndege hiyo ni Australia, China, Thailand, Indonesia, Singapore, Vietnam, Philippines, New Zealand na Marekani.

 

Askofu Mtetemela awatuliza wananchi

Dodoma. Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Donald Mtetemela amewahakikishia Watanzania kuwa Katiba itapatikana kwa wakati.
Hata hivyo, amesema kuna haja kwa Watanzania wa dini zote kuliombea Bunge Maalumu la Katiba lifanye mambo kwa kumshirikisha Mwenyezi Mungu ili mchakato wa Katiba uende vizuri.
Askofu Mtetemela, ambaye ni mmoja wa mjumbe wa Bunge hilo, alitoa ushauri huo jana kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Alisema kuyumba kwa Bunge la Katiba kwa sasa kunatokana na misimamo ya vyama vya siasa na kwamba kitendo hicho kimesababisha kuchelewa kwa kazi ya msingi.
“Mambo ya misimamo hayawezi kuzuilika na wala si kosa kila kikundi kuwa na msimamo wake, lakini kinachotakiwa ni wajumbe kufuta mambo ya vyama vichwani mwao na hasa pale panapokuwa na hoja ya msingi,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.
“Watanzania waendelee kutuombea kwa nguvu zote. Sina shaka tutatoka hapa tukiwa wamoja kwa sababu tunaimba wimbo mmoja wa kutaka kitu kizuri mbele yetu,” alisisitiza Askofu Mtetemela.
Askofu Mtetemela alisema kuwa katika hatua za awali kulikuwa na misukosuko mikubwa ndani ya Bunge, lakini sasa kuna mwelekeo wa kuridhisha kutokana na wajumbe kuelewa wajibu wao katika mchakato huu.

 

Bunge Maalumu la Katiba sasa vululu vululu

 

Dodoma. Matarajio ya Bunge Maalumu la Katiba kukamilisha kanuni kwa maridhiano yaliyeyuka tena jana huku mambo ndani ya ukumbi yakionekana kuwa vululuvululu kwa baadhi ya wajumbe kuzungumza nje ya utaratibu na wengine kurushiana vijembe.
Baadhi ya wajumbe waliamua kutoleana lugha chafu na kuweka kando hoja za msingi zinazowafanya watofautiane na kuchelewesha kazi ya kuandika Katiba Mpya.
Hali ilichafuka mchana wakati wajumbe walipokutana kupitisha kanuni baada ya mmoja wao, Felix Mkosamali kuomba mwongozo kwa Mwenyekiti wa muda, Pandu Ameir Kificho. Hata hivyo, Kificho alimtaka kukaa chini kwa muda kwa maelezo kuwa wajumbe waliofika katika kikao hicho walikuwa wachache, hivyo mwongozo wake kama ulikuwa unahitaji majibu ingekuwa vigumu kutolewa.
Baada ya muda alisimama, James Mbatia na kuomba mwongozo, akihoji sababu za kutaka kuanza kikao cha kupitisha kanuni hizo wakati wajumbe hawajapewa vitabu vya rasimu ya kanuni zenyewe.
“Mwenyekiti ulitangaza asubuhi kuwa tutagawiwa kanuni kabla ya saa tisa lakini hadi sasa tunataka kusomewa kanuni wakati hatujagawiwa kanuni hizo,” alihoji Mbatia.
Kificho alitoa ufafanuzi kuwa kanuni hizo zilikuwa bado zinadurufiwa na kuwataka wajumbe wawe na nidhamu kwani anapotangaza wanapiga kelele.
Ghafla alisimama Mkosamali tena na kuwasha kipaza sauti na kuhoji kitendo cha mwenyekiti huyo kumpa Mbatia nafasi ya kutoa mwongozo wakati yeye amenyimwa... “Mwenyekiti hivi unaongozaje kikao, inakuwaje mimi nikuombe mwongozo uninyime na mwenzangu umpe? Mwenyekiti nakuheshimu sana, lakini sijui unatumia kanuni ipi kutoa nafasi kwa mjumbe wakati mimi ulinizuia nisiseme,” alihoji Mkosamali.
Baada ya kauli hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Hawa Ghasia aliwasha kipaza sauti na kwa sauti ya juu alisema “Mtoto mdogo hana adabu.” Kauli hiyo iliibua hasira za Mjumbe mwingine, Moses Machali ambaye naye aliwasha kipaza sauti na kumjibu: “Kubwa jinga halina adabu,” kauli iliyoibua miguno ndani ya Bunge.
Hata hivyo, licha ya Mwenyekiti kutoa onyo kwa kauli hizo kwamba hazifai, Mkosamali alisimama katika sehemu yake na kusema kuwa hakuna mtoto mdogo na kwamba tangu lini mtoto aliishinda CCM.
Chanzo cha tatizo
Chanzo cha mvurugano huo ambao wiki iliyopita kidogo usababishe ngumi kurushwa bungeni, ni mfumo wa upigaji kura katika kupitisha ibara za rasimu, ambao jana uliendelea kuwagawa wajumbe na kufanya ukumbi huo kuonekana kama eneo la mzaha.
Kauli za ‘ndiyoooo’, ‘hapanaaaa’ na vitendo vya kugonga meza viliongezeka katika kipindi cha asubuhi baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Kanuni, Profesa Costa Mahalu kuwaleza wajumbe kuwa kamati yake haijafikia mwafaka wa ama iwe kura za siri au wazi na kwamba suala hilo limerejeshwa kwa wajumbe wenyewe.

 

Meli ya Korea Kaskazini yanaswa Libya

Wakuu nchini Libya, wamesema kuwa wameikamata meli moja iliyokuwa na bendera ya Korea Kaskazini, ikiwa na shehena haramu ya mafuta katika bandari inayodhibitiwa na waasi.

 

Msemaji wa shirika la kitaifa la mafuta, amesema kuwa meli hiyo ilisimamishwa ilipokuwa ikijaribu kungoa nanga na kwa sasa inasindikizwa katika bandari inayodhibitiwa na serikali ya Libya.
Maafisa wa serikali ya Libya waliisimamisha Meli hiyo ya Korea Kaskazini ilipokuwa ikiondoka kutoka bandari inayodhibitiwa na waasi siku ya Jumatatu ikiwa imesheheni mzigo usio rasmi wa mafuta ghafi.
Jeshi la nchi hiyo limethibitisha tukio hilo.
Waasi wa zamani wanaotaka kuitenga eneo la Libya Mashariki, wamekuwa wakimiliki bandari ya Al-Sidra na vituo vingine muhimu vya kuuzia bidhaa nje katika eneo hilo tangu Julai mwaka uliopita.
Mnamo siku ya Jumamosi, walianza kupakia shehena ya mafuta yasiyosafishwa ndani ya meli hiyo ya Korea Kaskazini iitwayo Morning Glory, iliyokuwa imetia nanga katika bandari ya Al-Sidra.

Viongozi walaani wizi wa mafuta

Kiwanda cha mafuta nchini Libya
Siku ya Jumatatu jeshi la wanamaji lilizuilia meli hiyo ilipokuwa ikiondoka bandarini, huku amri ikitolewa ielekezwe hadi katika bandari inayodhibitiwa na serikali.
Chama kikuu cha kisiasa nchini humo cha General National Congress, GNC, kimethibitisha kuzuiliwa kwa meli hiyo.
Runinga ya taifa Nchini Libya Al-Nabaa pia imeripoti tukio hilo kwa undani.
Walid al-Tarhuni, ambaye ni msemaji wa zamani wa kundi la waasi ambalo limekuwa likidhibiti bandari hiyo, ameiambia runinga ya Al-Nabaa kuwa meli hiyo ya mizigo ilikuwa ikielekea katika bandari ya Zawiyah, kilomita 50, Magharibi mwa mji mkuu Tripoli, kupakua mafuta hayo.
Utawala wa Washington umesema kuwa umeshangazwa na tukio hilo na kukariri kuwa mafuta inayotoka Libya ni mali ya raia wa nchi hiyo na wala sio ya makundi fulani.

 

Malaysia yazidisha kasi kutafuta Ndege 

Zoezi la kutafuta ndege ya abiria ya Malaysia limeendelea kushika kasi baada ya kuwepo kwa hali ya sintofahamu na wasiwasi mwingi kutoka kwa ndugu za watu waliopotea wakiwa katika ndege hiyo.

 

Ndugu wa waliopotea wameelezwa kuwa wakae tayari kupata habari mbaya

 Mamlaka nchini Malaysia zinasema wameongeza mipaka ya eneo la utafutaji, mara mbili Zaidi, huku China ikiwa imepeleka mitambo 10 ya satelaiti kwa ajili ya kusaidia kutafuta ndege hiyo.

Mkuu wa Idara ya anga Azharuddin AbdulRahman amewaambia waandishi wa habari kuwa eneo la kusaka ndege hiyo limeongezeka mara mbili kutoka maili 50 za baharini kunakosemekana ndege ilipotelea mpaka maili 100.
Ndege iliyokua imebeba watu 239 ilipotea bila kutoa taarifa yeyote na hakuna dalili yeyote mpaka sasa ya kupatikana kwa mabaki ya ndege hiyo.