Monday 3 March 2014

Urusi yatetea hatua ya kijeshi Ukraine 

   

Hali ya taharuki bado imelikumba jimbo la Crimea.

Urusi imetetea uamuzi wake kutuma wanajeshi nchini Ukraine, katika kikao cha dharura cha baraza la usalama la Umoja wa mataifa.

Balozi wa Urusi katika umoja wa mataifa, Vitaliy Churkin, amesema kuwa rais wa Ukraine aliyeng'olewa madarakani Viktor Yanukovych alikuwa ameiomba Moscow kutuma wanajeshi ili kuwalinda raia na kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Akizungumza baada ya mkutano huo wa Baraza la Usalama, Balozi Vitaly Churkin amesema kuwa malalamishi ya bwana Yanukovich yanafanana na yale ya Urusi.
"Nadhani ni muhimu kuzingatia kwamba mtu tunayeamini kuwa ndiye rais halaIi wa Ukraine pia ana wasiwasi tulio nao kuhusu idadi kubwa ya raia wa Ukraine, kuhusu kinachoendelea. Na ametoa wito kwa Urusi kutumia majeshi yetu kuzuia mambo kuwa mabaya zaidi.''
 
Marekani imesitisha ushirikiano na Urusi

Lakini balozi wa Ukraine, Yuriy Sergeyev, amesema kuwa madai ya Urusi hayahusiani na kile kinachojadiliwa kwani bwana Yanukovich hakuwa tena rais wa Ukraine.
"Hana lolote kwa sasa. Tukizungumzia hali ilivyo kwa sasa nchini Ukraine na madaraka ya kisheria ya mbunge ambalo lilimng'oa madarakani-hata balozi Churkin hivi leo kama ulisikia alichosema, ametaja kwamba tunaamini hatawahi kuwa rais wa Ukraine. Hii ina kwamba yeye siye mtu wa kuzungumza naye na hana lolote la kuzingatiwa."
Marekani imejibu kwa kusitisha mazungumzo ya kibiashara pamoja na uekezeji kati yake na Urusi, na idara ya Ulinzi ya Pentagon imetangaza kuwa ushirikiano wote wa kijeshi kati ya Marekani na Urusi ikiwemo mazoezi ya kijeshi, ziara za bandarini na mikutano ya mipango yote imesitishwa.

 

Watu 28 wauawa nchini China

Nchini Uchina, kundi moja la watu waliojihami kwa visu limewauawa takriban watu 28 katika kituo kimoja cha treni kusini magharibi mwa mji wa Kunming.  


 

Kituo cha habari cha Xhinua kimesema kuwa zaidi ya watu mia moja walijeruhiwa.
Mashahidi wamesema kuwa washambuliaji hao waliovalia nguo nyeusi,waliwavamia abiria waliokuwa wakingojea kuabiri treni na kuwakatakata huku wengine wakiwadunga visu wale walioshindwa kukimbia kwa kasi.
Kulikuwa na takriban washambuliaji 10.
Polisi waliwapiga risasi na kuwaua washambuliaji 5 huku wakiwasaka waliosalia.
Shirika la habari la Xhinua limewalaumu watu wanaopigania kujitenga katika mkoa wa Shinjiang kwa tukio hilo.

Obama aionya Urusi kuhusu Ukrain


Rais Obama aongea na rais wa Urusi Vladmir Putni katika simu


Rais Obama amesema kuwa Urusi inakiuka sheria ya kimataifa kufuatia hatua yake ya kuingiza vikosi vyake nchini Ukrain na sasa ametoa wito kwa rais Vladmir Putin kuvirudisha vikosi hivyo katika kambi zake za jimbo la Crimea.
katika mazungumzo ya simu yaliochukua takriban dakika 90,rais Putni amemwambia Obama kwamba Urusi ina haki ya kutetea maslahi yake iwapo ghasia zaidi zitaelekea mashariki kwa Ukrain pamoja na jimbo la Crimea.

Lakini rais Obama ameonya kwamba Urusi huenda ikatengwa kisiasa na kiuchumi iwapo uvamizi huo utaendelea.
Amemwambia rais Putni kwamba wasiwasi wowote wa Urusi kuhusu hali ya raia wa Urusi wanaoishi nchini Ukrain unafaa kujadiliwa ana kwa ana na serikali ya Ukrain.
Kaimu rais wa Ukrain, Oleksandr Turchynov,ameviweka vikosi vyake vya kijeshi nchini humo katika hali ya tahadhari.
Hatua hiyo inajiri baada ya bunge la Urusi kumruhusu Rais Vladimir Putni kutuma wanejeshi nchini Ukrain.
Wakati huohuo kaimu waziri mkuu Arseniy Yatsunuk amevitaka vikosi vya kijeshi vya urusi vinavyopiga doria katika eneo la Cremia kurudi kambini.
Ameonya kuwa iwapo mzozo huo utaendelea,Urusi ipo hatarini ya kukabiliwa kijeshi mbali na kumaliza uhusiano wake na Ukrain.

 

Ukraine yajizatiti kijeshi

Ukraine imeagiza kuimarisha vikosi vyake katika kukabiliana na Urusi ambayo inaimarisha jeshi lake katika jimbo la Ukraine la Crimea.

 

Kaimu Rais wa Ukraine Olexander Turchynov ameagiza kufungwa kwa safari za anga la nchi hiyo kwa ndege zote zisizo za kiraia.
Rais wa Marekani Barack Obama ameeleza usambazaji wa majeshi ya Urusi katika jimbo hilo ni "kuingilia uhuru wa Ukraine".
Waziri mkuu mpya wa jimbo la Crimea lenye mamlaka ya kujiamulia mambo yake lenyewe, Sergiy Aksyonov, mwenye mwelekeo wa kuipendelea Urusi, amesema amemwomba Bwana Putin ili kuhakikisha usalama wa eneo hilo.
Hata hivyo serikali ya mpito ya Ukraine haimtambui Bwana Aksyonov na serikali yake ya Crimea.

 

 

G7 yailaani Urusi kuihusu Ukraine

  

Maandamano ya kuipinga Urusi, Ukraine.
Kundi la mataifa saba yaliyostawi zaidi kiviwanda almaarufu kama G7 limelaani vikali hatua za kijeshi zilizochukuliwa na Urusi nchini Ukraine-viongozi kundi hilo wakitaja hatua ya Urusi kama ukiukaji wa uhuru wa Ukraine.
Katika taarifa ya pamoja iliyotiwa pia saini na Umoja wa Ulaya EU-Urusi imetakiwa kushughulia wasiwasi wake kuihusu Ukraini kupitia mashauri au upatanishi.
Kundi hilo la mataifa saba tajiri zaidi duniani maarufu kama G-Seven limesema kuwa linachukuwa uamuzi wa kuahirisha matayarisho ya kongamano ambalo lingefanyika nchini Urusi mwezi juni mwaka huu kutokana na vitendo vya Moscow. Taarifa hiyo inakuja wakati vikosi vya Urusi vikiimarisha uthibiti katika rasi ya crimea ambapo Urusi inasema kuwa inalinda raia wake baada ya serikali kupinduliwa mjini Kiev.
Mbunge mashuhuri wa Urusi - Vyacheslav Nikonov, ameimabia BBC kwamba Urusi imejiandaa kwenda vitani kulinda maslahi yake nchini Ukraine na hususan katika mji wa Sevastopol.
"Ukraine ilialikwa kujiunga na Nato na hii ina maana kuwa marekani, au vituo vyake vya kijeshi vitawekwa nchini Ukraine. Urusi itafanya lolote, itahatarisha kuingia vita kuzuia hilo kutokea. Ni kuhusu kituo cha kijeshi, ni kuhusu mustakabal wa Urusi, mustakabal wa Ukraine. Sidhani kama mataifa ya magharibi yanaelewa kwamba Ukraine ni mahali ambapo Urusi ilizaliwa," amesema Nikonov.
Wanajeshi wasiotambuliwa washika doria katika kambi moja ya kijeshi nchini Ukraine.
Awali serikali ya mpito ya Ukraine iliishutumu Urusi kwa kutangaza vita na kuwaamuru wanajeshi wake kuwa tayari kwa makabiliano.Shirika la kujihami kwa mataifa ya Magharibi NATO limetowa wito kwa Urusi kuwaondoa wanajeshi wake nchini Ukrainena kuzitaka pande zote kusuluhisha mgogoro huo kwa njia ya amani. Taarifa hiyo imetolewa baada ya mkutano wa dharura wa mabalozi wa NATO mjini Brussels kujadili mgogoro huo. Katibu mkuu wa NATO, Anders Fogh Rasmussen, amesema kuwa huenda wachunguzi wa umoja wa mataifa wakatumwa kusaidia kusuluhisha hali ya mambo.
"Tunatoa wito kwa urusi kuheshimu ahadi zake za kimataifa, kuondoa vikosi vyake na kujiepusha na uvamizi katika maeneo mengine nchini Ukraine. Tunatowa wito kwa pande zote kufuata njia ya amani katika kusuluhisha mgogoro huo kupitia mazungumzo, kupitia wachunguzi wa kimataifa chini ya mwavuli wa umoja wa baraza la usalama la umoja wa mataifa au shirika la ushirikiano wa kiusalama ulaya OSCE,'' amesema bwana Rasmussen.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa marekani , John Kerry, anatarajiwa kuzuru Kiev hapo kesho jumanne kuiunga mkono serikali mpya ya Ukraine.
Haya yanajiri wakati mkuu wa jeshi la wanamaji wa Ukraine, Denis Berezovsky, akipokonywa madaraka yake baada ya kusema hadharani kwamba anaunga mkono serikali mpya ya Jimbo la Crimea ambayo inaunga mkono Urusi. Serikali ya Kiev imesema kuwa inamfanyia uchunguzi kwa nia ya kumfungulia mashtaka ya uhaini.

Milipuko miwili yatikisa Maiduguri

Mji wa Maiduguri uliopo kazkazini mwa Nigeria umekumbwa na milipuko miwili, huku ripoti zikiarifu kwamba takriban watu 10 huenda wamepoteza maisha yao. 

 

Mkaazi mmoja ameliambia shirika la habari la Ufaransa kwamba mlipuko wa kwanza ulitokea katika eneo lililojaa watu huku wa pili ukilipuka wakati majirani walipokuwa wakiwasaidia waathiriwa.
Maafisa wa polisi wamesema kuwa watu wengi wamekwama chini ya vifusi.
Mji wa Maiduguri hutumiwa kama kambi ya wanajeshi wanaopigana na wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
Awali ripoti zimearifu kuwa kulikuwa na shambulizi la angani katika kijiji kimoja cha jimbo la Borno siku ya ijumaa.
Shahidi mmoja ameiambia BBC kwamba takriban raia 20 wamefariki.
Jeshi la Nigeria linadaiwa kuvilipua vijiji inavyoamini ni makao ya wanachama wa Boko Haram.

 

 

Na hivi ndiyo red carpet ya Oscar awards 2014 ilivyokuwa.

1
Tukio la utoaji wa tuzo zenye heshima kwenye movie industry limefanyika weekend iliyopita huko Marekani.
Zaidi ya nani kashinda tuzo gani kitu kingine kinachofatiliwa ni fulani alivaaje.
Hivi ndivyo jinsi mastaa wa movie walivyopendeza kwenye red carpet ya tukio hilo
amy-adams
anna-kendrick
anne-hathaway
brad-pitt-angelina-jolie
bradley-cooper
bette-midler
barkhad-abdi
elsa-pataky-chris-hemsworth
charlize-theron
chiwetel-ejiofor-sari-mercer
emma-watson
gabourey-sidibe
chrissy-teigen
christian-bale-sibi-blazic
giuliana-rancic
glenn-close
jared-leto
jenna-dewan-tatum
goldie-hawn
idina-menzel-kristen-bell
jennifer-garner
jennifer-lawrence
ireland-baldwin
kelly-ripa
lady-gaga
jessica-biel
jonah-hill
kerry-washington
lara-spencer
leonardo-dicaprio
kevin-spacey
julie-delpy
kelly-osbourne
kristin-chenoweth
liza-minnelli
lupita-nyong
penelope-cruz
ryan-seacrest
sandra-bullock
pharrell-williams-helen-lasichanh
matthew-mcconaughey-camila-alves
portia-de-rossi
michael-strahan
smith-jada-pinkett-smith
viola-davis
robin-roberts
olivia-wilde-jason-sudeikis