Watu 28 wauawa nchini China
Nchini Uchina, kundi moja la watu waliojihami kwa visu limewauawa takriban watu 28 katika kituo kimoja cha treni kusini magharibi mwa mji wa Kunming.
Kulikuwa na takriban washambuliaji 10.
Polisi waliwapiga risasi na kuwaua washambuliaji 5 huku wakiwasaka waliosalia.
Shirika la habari la Xhinua limewalaumu watu wanaopigania kujitenga katika mkoa wa Shinjiang kwa tukio hilo.
No comments:
Post a Comment