Monday 3 March 2014

Watu 28 wauawa nchini China

Nchini Uchina, kundi moja la watu waliojihami kwa visu limewauawa takriban watu 28 katika kituo kimoja cha treni kusini magharibi mwa mji wa Kunming.  


 

Kituo cha habari cha Xhinua kimesema kuwa zaidi ya watu mia moja walijeruhiwa.
Mashahidi wamesema kuwa washambuliaji hao waliovalia nguo nyeusi,waliwavamia abiria waliokuwa wakingojea kuabiri treni na kuwakatakata huku wengine wakiwadunga visu wale walioshindwa kukimbia kwa kasi.
Kulikuwa na takriban washambuliaji 10.
Polisi waliwapiga risasi na kuwaua washambuliaji 5 huku wakiwasaka waliosalia.
Shirika la habari la Xhinua limewalaumu watu wanaopigania kujitenga katika mkoa wa Shinjiang kwa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment