Monday 3 March 2014

YALIYOJIRI KATIKA PICHA KWENYE BUNGE MAALUMU LA KATIBA


 Mbunge wa Mtera, Livingstone  Lusinde na mbunge wa Moshi mjini Mhe. Philemon Ndesamburo ambao pia ni wabunge wa bunge maalumu la katiba wakiagana mara baada ya kuahirishwa kwa semina ya kuandaa kanuni zitakazo tumiwa wakati wa kikao cha bunge maalumu la katiba mjini Dodoma.


Mwenyekiti wa chama cha UDP Mhe. John Momose Cheyo wakizungumza jambo na mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi Mhe. James Mbatia ambao pia ni wajumbe wa bunge maalumu la katiba wakijadiliana wakati wakitoka katika semina ya kujadili rasimu ya kanuni za kuongoza bunge hilo.

Mhe. Ole Sendeka akichangia mswada wa kanuni zitakazo tumika wakati wa kikao cha bunge maalumu la katiba jana jioni.


Mhe. James Mapalala akiwelekeza jambo mjumbe mwenzake kwa kidole wakati wa semina ya  kujadili rasimu ya kanuni zitakazo tumika wakati wa kikao cha bunge maalumu la katiba. Picha na Deusdedit Moshi

No comments:

Post a Comment