RIDHIWANI AANZA MBIO ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE
Meneja
wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa
ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM), Ndg. Ridhiwani
Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika
kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.

Mgombea
Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ndg. Ridhiwani
Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Saadani
Wilayani Bagamoyo, wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza
rasmi jana Machi 14,2014.
Baada
ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Mgombea Ubunge
katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete
alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana
na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.