Monday 17 March 2014


RIDHIWANI AANZA MBIO ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE‏


Meneja wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo, wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.Baada ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.

Mbunge wa Arumeru Mshariki , Joshua Nassari aumbuka bungeni




Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Joshua Nassari, juzi alijikuta akiumbuka bungeni baada ya kushindwa kutaja kanuni aliyoitumia, kuomba mwongozo. 
 
Hali hiyo ilitokea muda mfupi kabla ya wajumbe kupiga kura za kumchagua Mwenyekiti wa Bunge hilo.
 
Kuumbuka kwa mjumbe huyo ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Mshariki, kulitokana na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho, kumtaka kutaja kanuni aliyoitumia.
 
Hata hivyo, baada ya kusita kwa muda Nassari bila kutaja kanuni aliyoitumia, alisema wajumbe wengi hawajasikia utaratibu unaotumika katika upigaji kura kwa sababu walichelewa kwenye msongamano wa watu getini.
 
“Wengi wetu tumeingia tukiwa tumechelewa kwa sababu wengi tunapita katika geti moja. Ningependa ufafanuzi wako kuhusu aina ya kura tunayokwenda kupiga ni ya wazi au ya siri,”alisema.
 
Hata hivyo, kificho alimjibu kuwa kura zitakazopigwa kumchagua mwenyekiti zitakuwa ni za siri.
 
Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya Bunge hilo kupitisha kanuni za uendeshaji wake ambapo hata hivyo nyingine bado zimekuwa na mgongano wa maridhiano kwa baadhi ya wajumbe kutaka ufafanuzi zaidi.