Monday 17 March 2014


RIDHIWANI AANZA MBIO ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE‏


Meneja wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo, wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.Baada ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.

No comments:

Post a Comment