Friday 28 February 2014

Viwanja vya ndege vyadhibitiwa Crimea

Waziri wa mambo ya ndani wa Ukraine amesema majeshi ya Urusi yamekuwa yakiweka vizuizi katika uwanja wa ndege wa Sevastopol uliopo katika jimbo la Crimea.

 

Watu wenye silaha wakilinda doria uwanja wa ndege Simferopol, Crimea, Ukraine

Waziri huyo wa Ukraine, Arsen Avakov ameita uwepo wa majeshi ya Urusi katika jimbo hilo kuwa "uvamizi wa kijeshi".
Watu hao wenye silaha pia wameutwaa uwanja mwingine mkubwa wa ndege wa Simferopol, uliopo pia Crimea Ijumaa asubuhi.
Uhusiano kati ya Urusi na Ukraine umeyumba tangu kuondolewa madarakani kwa Rais wa Ukraine, Viktor Yanokovych, ambaye kwa sasa yuko nchini Urusi.
Uhasama huu umedhihirika zaidi katika jimbo la Crimea, nchini Ukraine, ambalo wakaazi wake wengi ni Warusi.
Siku ya Alhamisi, watu wenye silaha wenye mwelekeo wa Urusi, walivamia ofisi za bunge la Simferopol, na kuliondoa baraza la sasa la mawaziri na kumchagua waziri mkuu mpya.
Bado haijafahamika watu hawa wenye silaha katika mji wa Simferopol waliowasili katika uwanja wa ndege mapema ni kina nani.
Licha ya kuwepo kwao, inasemekana shughuli zinaendelea kama kawaida katika uwanja wa ndege wa Simferopol.
Watu walioshuhudia tukio hilo wameliambia shirika la habari la Ukraine, Interfax, kuwa watu wapatao 50 waliwasili katika uwanja wa ndege wa Simferopol wakiwa wamebeba bendera za jeshi la wanawamaji la Urusi.

 

Kenya: Wajumbe wa ODM wazua vurugu

Vurugu zimezuka katika uchaguzi wa kuwachagua maafisa wapya wa chama kikuu cha upinzani cha ODM nchini Kenya, chake aliyekuwa waziri mkuu wa taifa hilo Raila Odinga.

 

Bwana Odinga anatarajiwa na wengi kuwa atagombea kiti cha urais 2017

 Polisi waliwasili katika ukumbi wa uwanja wa michezo wa kimataifa wa Kasarani viungani mwa jiji la Nairobi kurejesha utulivu baada ya baadhi ya wafuasi wa chama hicho waliodaiwa kuwa walinda usalama kurusha vita pamoja na masanduku ya kupigia kura wakijaribu kuvuruga uchaguzi huo.

Ugomvi ulizuka baada ya kuzuka madai kuwa kulikuwa na orodha ya wajumbe bandia iliyokuwa ikisambazwa pamoja na makaratasi bandia ya kupigia kura. Mbunge maalum Isaac Mwaura ambaye anaishi na ulemavu wa ngozi-Albino-alionekana akisukwasukwa na wajumbe baada ya kuzua zahama kuhusu madai hayo ya udanganyifu katika zoezi hilo la upigaji kura.
Chama cha ODM ndicho chama kikubwa zaidi cha kisiasa nchini Kenya kikiwa na idadi kubwa ya wabunge katika bunge la kitaifa pamoja na Senate. Chama hicho kimemudu mgao mkubwa zaidi wa pesa za kufadhili shughuli za vyama vya kisiasa kutoka kwa serikali ya Kenya.
Kutokana na raslimali za chama hicho uchaguzi wa leo umeonekana kuzua msisimko mkali pamoja na patashika baina ya wanasiasa mashuhuru ambao wanagombania vyeo mbali mbali.
Bwana Odinga ambaye alishindwa na rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliokumbwa na madai ya udanganyifu mwezi Machi mwaka uliopita anatetea kiti chake kama kiongozi wa chama, dalili kwamba huenda akagombea tena kiti cha urais mwaka 2017.
Akizungumza kabla ya kuanza kwa zoezi la upigaji kura Bwana Odinga alizungumzia maswala mbali mbali yanayohusiana na usalama nchini Kenya pamoja na kuiponda serikali ya mpinzani wake Rais Uhuru Kenyatta kwa kushindwa kuleta suluhu ya matatizo ya kiuchumi yanayowakabili wakenya.

 

Shambulizi lawaua 12 Mogadishu

Mshambuliaji wa kujitoa muhanga amejilipua ndani ya gari na kuwauwa watu 12 na kujeruhi wengine wanane mjini Mogadishu Somalia.

 

Mogadishu imeshuhudia mashambulizi ya mara kwa mara hivi karibuni

Mlipuko huo umetokea nje ya makao makuu ya maafisa wa usalama .
Mwandishi wa BBC anasema kuwa waliofariki ni maafisa usalama na wengine raia wa kawaida waliokuwa katika mkahawa karibu na hapo.
Kumekuwa na ongezeko la mashambulizi huku vikosi vya nchi hiyo vikipambana na wanamgambo wa al shaabab.
Kundi la wanamgambo la Al Shabaab limekiri kufanya shambulizi hilo ambalo limetokea chini ya wiki mbili baada ya kundi hilo kushambulia ikulu ya Rais mjini Mogadishu
Msemaji wa kijeshi wa kundi hilo amenukuliwa na shirika la habari la Reuters akisema kuwa huu ndio mwanzo tu wa kundi hilo kushambulia Mogadishu na kwamba operesheni yao itaendelea.
Alisema kuwa shambulio hilo lililenga maafisa wa usalama waliokuwa wameketi katika mkahawa mmoja na kuwaua watu 11 huku 15 wakijeruhiwa.

 

Marekani kuleta umeme Afrika

Wabunge nchini marekani wameidhinisha mpango wa kuleta umeme kwa zaidi ya watu millioni hamsini katika jangwa la Sahara barani Afrika na hivyo basi kutoa fursa kwa mradi huo wa serikali ya Obama kuanza kutekelezwa.

      

Mswada huo uliopitishwa na kamati ya maswala ya kigeni nchini humo unalenga kujenga megawati elfu ishirini barani Afrika ifikiapo mwaka 2020 na kuwafikia watu elfu hamsini ambao wanaishi bila umeme.

Mpango huo ulitangazwa na rais Obama wakati wa ziara yake barani afrika mnamo mwezi juni mwaka jana.
Mswada huo utahitajika kupitishwa na bunge la wawakilishi pamoja na lile la sineti lakini hatua hiyo ya kamati ya maswala ya kigeni ni dhihirisho tosha kwamba unuangwa mkono na pande zote za kisiasa.

 

Wanafunzi wa Tanzania Thailand Waizungumzia sekta ya Madini.

                    

1 
Kamishna Msaidizi wa Madini  Mhandisi Hamis Komba katikati akiwa pamoja na Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand. Wa kwanza kulia ni Agatha Mwinuka, anayefuata ni Emmanuel Minja na wa kwanza 

kushoto ni Doricas Moshi. Wanafunzi wa Kitanzania nchini Thailand, wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenzao kutoka mataifa mbalimbali , ambao wamelitembelea  banda la Tanzania.
   
Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini katika picha ya pamoja na wanafunzi hao katika banda la Tanzania.
2
3 (2)
……………………………………………………………………………………
Na Asteria Muhozya, Bangkok
Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand, wamewataka wadau wa tasnia ya madini ya vito na usonara nchini Tanzania kuichukua sekta hiyo kwa umakini mkubwa kutokana na  mchango wake kiuchumi.
Aidha, wameeleza kuwa, nchi ya Thailand imepiga hatua kubwa katika sekta ya madini ukilinganisha na Tanzania lakini bado Tanzania inaweza kufaidika zaidi katika sekta hiyo ikiwa kila mdau atatimiza wajibu wake kikamilifu ili madini ya vito yaongeze mchango katika pato la taifa.
Wameongeza kuwa, Tanzania bado ina nafasi ya kujipanga upya kuhusu kuboresha zaidi sekta hiyo kama ilivyo kwa nchi nyingine  endapo mipango mikakati ya maboresho itatekelezwa  na kusimamiwa kikamilifu.
Wanafunzi hao wameyasema hayo, wakati walipolitembelea banda la Tanzania katika maonesho ya 53 ya Vito vya Usonara na Madini yanayoendelea katika jiji la Bangkok ambapo nchi zaidi ya 150 zinashiriki maonesho hayo.
“Thailand wamejipanga vizuri katika sekta ya madini. Wafanyabiashara wa madini wana umoja. Wadau wa madini wanatakiwa kuelewa  kuwa madini yanawakilisha utajiri wetu tulionao”. Amesema Agatha Mwinuka.
Aidha, wameitaka serikali na  wadau wa Tanzania  wanaoshiriki maonesho hayo kujifunza kutokana na changamoto wanazozipata kutoka kwa nchi nyingine, jambo ambalo litasaidia kuboresha sekta ya madini na vito, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kuhakikisha  kuwa wanafuata sheria na taratibu zilizopo.
“Tunaiomba serikali iendelee kuendeleza viwanda vya kukata madini. Ni jambo zuri kama shughuli hizi za kukata madini zitafanyika ndani ya nchi badala ya nje. Jambo hili linasaidia sana kuongeza thamani ya madini.  Ameongeza, Emmanuel Minja.
Akiongelea kuhusu umuhimu wa kuendeleza na kuboresha kituo cha Tanzania Geomological Center,  Doricas Moshi, ameeleza kuwa,  kituo hicho kinaweza kutoa mchango mkubwa katika tasnia hii hasa katika nyanja ya ukataji madini  na uthamini wa madini hivyo, ameitaka Serikali kukiongezea nguvu kituo hicho kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya  Tanzania.
“Chuotunachosoma hapa kinatumia sana mifano ya madini ya Tanzania katika kufundisha.  Mengi yametoka nyumbani, hii ni ishara nzuri. Serikali iliangalie hili. Ameongeza Doricas.
Aidha, wameeleza kuwa, soko la kimataifa kwa madini ya Tanzania lipo, hivyo, wamewataka wadau wote kuhakikisha wanashirikiana vizuri na serikali kuendeleza sekta hiyo kutokana na umuhimu na mchango wake kwa taifa. 
Akizungumzia  mipango iliyopo ya kuboresha sekta hiyo, Kamishna Msaidizi wa Madini, Mhandisi Hamis Komba, amesema kuwa, Serikali kupitia Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), inatekeleza mikakati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo na wa kati  ili waweze kuendana na   mahitaji ya soko la kimataifa kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali yakiwemo ya kukata madini, kuyaongezea thamani na  kuwapatia mikopo kupitia Benki ya TIB.
“STAMICO imepewa jukumu la kuwaendeleza wachimbaji wadogo katika sekta ya madini hususani katika masuala ya uchimbaji, uongezaji thamani madini na biashara ya madini. Serikali imejipanga vizuri katika hilo”. Ameongeza Kamishana. 
Ameongeza kuwa, Serikali inatambua kwamba wachimbaji wengi wapo katika sekta ya madini ya vito na usonara hivyo, jitihada za kuwaendeleza  zitasaidia kufikia kiwango bora cha utendaji wao wa kazi.
Vilevile, ameongeza kuwa, kutokana na kuboreshwa kwa Sheria ya madini ya mwaka 2010 ambayo inaiwezesha STAMICO kumiliki asilimia 50 ya hisa katika mgodi wa Tanzanite One, jambo ambalo linaifanya Serikali kuwa mmiliki katika mgodi huo

Mtikila akwaa Kashfa ya Kuwatunza Viongozi wa FDLR Jijini Dsm




Nilikuwa nasoma ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliyowakilishwa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa January 2014. Ripoti inaongelea masuala mengi, lakini nimeona siyo vibaya ku-share nanyi sehemu inayohusiana na Mchungaji Mtikila kukubali kuwa-host rebels wa FDLR nyumbani kwake Dar Es Salaam na masuala mengine kuhusiana na Tanzania.
Pia ripoti inadai kuwa vyombo vya usalama vya Tanzania vilimweka under house arrest Dar Es salaam mmoja ya viongozi wakuu wa FDLR anayejulikama kama Stanislas Nzeyimana (Bigaruka). Kwa wale wafuatiliaji wa mambo kwenye eneo la maziwa makuu watakumbuka kuwa kiongozi huyo alikuwa amepigwa ban ya kusafiri.

Serikali ya Tanzania ilipoulizwa na kundi hilo la wataalam wa Umoja wa Mataifa kuhusiana Bigaruka kusafiri na kukaa Tanzania, ilidai haikuwa na taarifa za kiongozi huyo kusafiri na kuishi Tanzania na hatimaye kupotea kwake ghafla. Inasemekana mpaka sasa hajulikani alipo kiongozi huyo huku taarifa nyingine zikidai kuwa wamekamatwa na serikali ya Rwanda. Wataalam hao wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuchunguza kuhusiana na kutoonekana kwa Bigaruka. Kwa wale ambao siyo wavivu wa kusoma, link ya ripoti nzima ya UN ipo hapo chini.

============================== ==============



A UN photo of Reverend Christopher Mtikila’s residence in
Dar Es Salaam, Tanzania, where FDLR second in command, Gen. Deogratias Nzeyimana, alias Bigaruka, stayed.
Reverend Christopher Mtikila has on several occasions hosted senior commanders of Rwandan FDLR rebels transiting through Dar es Salaam Tanzania in efforts to link them up with the outside work, the UN and the politician himself have confirmed. While in Dar es Salaam, they stayed at the personal residence of Rev. Mtikila which is identified in the photo above. According to UN Group of Experts report on DRC released on 24 January 2014, Reverend Mtikila confirmed to them that he had indeed hosted the FDLR political and military officials.

Disappearance of sanctioned FDLR leader Stanislas Nzeyimana (Bigaruka)
Early in February of 2013, one of the FDLR commanders from DRC disappeared. The UN experts say that while FDLR officers and intelligence sources from the region had told the Group that Rwandan officials were detaining Bigaruka, other FDLR sources alleged that Tanzanian security services placed Bigaruka under house arrest in Dar Es Salaam. The UN Group attempted to confirm this allegation with the Tanzanian authorities, which told the Group they were not aware of Bigaruka’s travel and stay in Dar Es Salaam, and had no information about his disappearance or whereabouts.

The UN Group however documented Bigaruka’s travel to Tanzania in violation of the travel ban imposed upon him. Three individuals, including Joseph Nzabonimpa (see S/2012/843, para. 101; Annex 40), told the Group that they – along with Faustin Murego – travelled to Dar es Salaam in January 2013 and met Bigaruka to discuss demobilization and disarmament as well as the issue of child soldiers (see annex 41).

At the beginning of his stay in Dar es Salaam, Bigaruka stayed in the house of Tanzanian reverend Christopher Mtikila, which the reverend acknowledged to the UN Group (see annex 42). In early February, after these meetings, Bigaruka disappeared. The Group continues to investigate the matter.

TOTAL YAZINDUA AWANGO KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME


Mgeni rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua.
Waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia tukio mojawapo katika hafla hiyo.
Kikundi cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini na pembezoni mwa miji.
Meneja wa Maswala ya Kisheria na Ushirika wa kampuni ya TOTAL Tanzania Bi. Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.

DTBi - COSTECH WATILIANA SAINI YA USHIRIKIANO NA SILION VALLEY YA MAREKANI

Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi sign MOU copy  Bw.Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi (kulia) wakisaini MOU.

 

Na Mwandishi Wetu, MOblog Tanzania
KAMPUNI tanzu ya Tume ya sayansi na teknolojia ya DTBi-COSTECH na Silicon Valley Black Chamber of Commerce’s Center for Entrepreneurial Development (SVCED) wametiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano (MoU) ambapo pande zote mbili zitashirikiana kwa njia mbalimbali kwa ajili ya ukuaji wa wajasiriamali.

Mkataba huo, kati ya DTBi na SVCED utawezesha pande hizo mbili kukuza ujasiriamali na kujenga uwezo katika Habari, Teknolojia na Mawasiliano kwenye sekta zote za kiuchumi.

Mkataba huo wa MoU utawafanya wadau kufanya shughuli za biashara kwa kuanza na mfumo wa teknolojia ya habari na mawasiliano kwa kupitia njia ya mtandao na kusaidia wale walio na ubunifu katika nyanja mbalimbali za biashara.

 

 Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi shake hands after signing MOU copy

Bw. Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi kupeana mikono baada ya kusaini MOU.

Mkataba huo pia utasaidia wajasiriamali kuweza kukua na kufanya biashara kwa kutumia mifumo habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ujasiriamali na kuanzisha mfumo wa kubadilishana uzoefu katika kuendeleza biashara na ukuaji wa ujasiriamali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi, Injinia. George Mulamula amesema mkataba MOU utatoa ushirikishiano ambao utaruhusu wajasiriamali wa Tanzania kufaidika na ujuzi, maarifa ya Silicon Valley ya ujasiriamali.

Amesema hii itasaidia nchi ya Tanzania kuruhusu uanzishwaji wa biashara kupitia njia ya mtandao na mifumo ya Habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ajira na kuchangia pato la taifa.
Mr Mulamula explains the partnership to the press copy 
Eng.George Mulamula akielezea ushirikiano kwa vyombo vya habari.
Baada ya kutiliana saini ya MOU, Bw Carl Davis Jr, alikuwa na semina kwa wajasiriamali yenye jina la “The Mindset of the Silicon Valley Entrepreneur: Lessons for the Tanzania Entrepreneur/Innovator”.

Mr Davis Jr amesema anaweza kuwasaidia “wajasiriamali kuelewa jukumu la uzinduzi na ujasiriamali na jinsi Wajasiriamali hapa nchini jinsi wanavyoweza kujiinua katika kufikiri chanya kwenye maeneo ya biashara.

Bw. Carl Davis Jr, akitoa majadiliano DTBi kwa wajasiriamali wa Tanzania juu ya jinsi ya kuwa mwekezaji mwenye mafanikio.
Attendee contributing to the discussion copy
Mshiriki akichangia mjadala.

Tanzania tunapaswa kuiga hili: Roboti zatumika Kuongoza magari DRC

 

Roboti barabarani DRC

Je Roboti kubwa zenye sauti nzito na mikono mikubwa zinaweza kuwa jibu kwa kupunguza msongamano wa magari barabarani?
Hili ndilo suluhu abalo serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imebuni ili kupunguza foleni ya magari mjini Kinshasa.
Mbinu hii ya kupunguza foleni ya magari inafanyiwa majiribio mjini Kinshasa.
Roboti mbili zilizotengezwa na kikundi cha watu zimepata kuungwa mkono na wananchi na maafisa wakuu, wanasema kuwa zinasaidia kupunguza msongamano wa magari barabarani.
Mji wa Kinshasa una wakazi milioni 10 na sifa yake kuu ni uendeshaji ovyo wa magari pamoja na msongamano mkubwa wa magari.
Licha ya kuwepo roboti, kuna pia taa za kawaida ambazo hutumiwa kurahisisha kuelekeza magari barabarani. Magari makuu kuu na madereva wasiojali sana sheria za barabarani.
Polisi wa trafiki pia wamekuwa wakituhumiwa kwa kuchukua hongo kutoka kwa wakiukaji wa sheria za barabarani hasa kutokana na kupokea mishahara midogo.
Mmoja wa wakazi wa Kinshasa anasema kuwa wakati Roboti hizo zinaposimamisha magari, unaona madereva wanatii huku watu wakivuka barabara bila matatizo yoyote.
Wengi wanalaumu polisi wa trafiki kwa kuwahangaisha . Wanataka Roboti waachwe zifanye kazi hiyo ya polisi.
Roboti hizo zina urefu wa mita 2.5 na zilianza kutumika mwezi Juni mwaka jana katika barabara yenye shughuli nyingi sana mtaa wa Lumumba Boulevard.
Roboti hiyo husema kwa sauti kubwa: ''Madereva mnahitaji kutoa nafasi kwa watu kuvuka barabara,'' huku ikiinua mkono mmoja ukionyesha taa nyekundu na kijani kama ishara ya kuenda au kusimama.CHANZO BBC SWAHILI

 

World Bank defers $90m loan to Uganda due new anti gay law.

 

President Museveni signed the controversial bill on Monday 

The World Bank has postponed a $90 million loan to Uganda after the country new anti gay law has drawn harsh criticism from across the globe. The loan was due to support and boost Uganda’s health services.
World Bank officials stated that they would not be willing to donate the money unless they could guarantee that projects that the money was destined to support would not be adversely affected by the new law.         
The new law was passed on Monday and is set to strengthen already strict legislation concerning homosexuals in Uganda. The law states that any person ‘promoting’ homosexuality is deemed a criminal and acts of ‘aggravated homosexuality’ are punishable by life imprisonment. The bill originally proposed the death penalty for some homosexual acts, but that was later removed amid international criticism.
The Ugandan government’s move has drawn harsh criticism from the EU with countries such as Denmark and Norway redirecting aid away from the government.
The US has also condemned the move with US Secretary of State John Kerry calling the law “atrocious”. South African Nobel peace laureate Desmond Tutu has compared the law to the anti-Semitic laws in Nazi Germany or the racial abuse seen in apartheid South Africa.
 World Bank President, Jim Yong Kim warned that the restriction of sexual rights through legislation ‘can hurt a country’s competitiveness by discouraging multinational companies from investing or locating their activities in those nations’.
The loan was due to be accepted on Thursday to support a loan given in 2010 focusing on family planning, maternal health and newborn care.
A spokesman for the World Bank said: ‘We have postponed the project for further review to ensure that the development objectives would not be adversely affected by the enactment of this new law.’
Uganda has already incurred huge financial loss due to the law but the World Bank’s withdrawal is by far the largest financial penalty the country has had to sustain. US President Obama has warned the law could ‘complicate’ Washington’s relations with Uganda, which receives a reported $400m (£240m) in annual aid from the US.
Despite vocal international criticism, Ugandan President Yoweri Museveni pushed forward and signed the anti-gay bill earlier this week.
Government spokesman Ofwono Opondo defended Museveni, stating he wanted ‘to demonstrate Uganda’s independence in the face of Western pressure and provocation’.
Homosexuality is illegal in 38 African countries, where most sodomy laws were introduced during colonialism. In Uganda, homosexual acts were punishable by 14 years to life in prison even before the controversial bill was signed into law.