TOTAL YAZINDUA AWANGO KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME
Mgeni
rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo
akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla
ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt
Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo
aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania
kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na
kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua.
Waziri
wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika
hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme
zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa
nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL
nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia tukio mojawapo katika
hafla hiyo.
Kikundi
cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa
(hawapo pichani) kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa
zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni
ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa
nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini
na pembezoni mwa miji.
No comments:
Post a Comment