Thursday 6 March 2014

KAULI KUMI(10) NA ZA KUSISIMUA ZILIZOVUTA HISIA ZA WENGI KWENYE BUNGE LA KATIBA MJINI DODOMA,ZISOME HAPA

Ni vigumu kueleza matukio yote yaliyotawala kauli na hisia za wengi kwa wiki nzima mjini Dodoma bila kuangalia  michango ya baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba.

Michango hiyo ya mawazo katika mjadala kuhusu rasimu ya kanuni zinazopaswa kuongoza kikao kwa siku 70 za kikao hicho, baadhi yake zilikuwa kali. 
Zifuatazo ni baadhi ya kauli hizo:
 1. Mchungaji Christopher Mtikila

Mtikila, ambaye ni mwenyekiti wa Democratic Party (DP), alitumia dakika tano kutoa somo kwa wajumbe wa Bunge hilo kuhusu umuhimu wa kupiga kura ya siri badala ya ile ya wazi.
Anasema haki ya kupiga kura kwa siri haitofautiani na haki ya mtu kuwa na miguu miwili na kwamba itashangaza akitokea mtawala akaamuru kila mtu awe na mguu mmoja, halafu watu wakakaa kujadili.
“Wote tutaonekana tuna matatizo ya akili,” alisema Mch. Mtikila.
Alisema Bunge Maalumu la Katiba litaingia katika hatia na aibu kwa kujadili mambo ya msingi ya kidemokrasia ambayo pia yameainishwa katika katiba ya sasa, likiwamo suala hilo la kura ya siri.
“Mwenyekiti (akimlenga Pandu Ameir Kificho) tumekuchagua kwa kura ya siri siyo kwamba tulikuwa wajinga kuliko wenzetu, hapana! Ni ‘democratic civility’ (ustaarabu wa kidemokrasia),” alisema.
 “Ni aibu waheshimiwa na hii nasema si jambo la mjadala kuna vitu vya kujadili, lakini si haki ya kupiga kura kwa siri. Hii ni haki ya msingi ya kidemokrasia,” alisema.

 2. Profesa Ibrahim Lipumba (Mwenyekiti –CUF Taifa)
Mwenyekiti huyo wa CUF alisema msingi wa kupiga kura ya siri ni kujaribu kuwalinda wajumbe ambao wanaweza kupiga kura kinyume na misimamo ya vyama vyao au makundi yao.
 Akijenga msingi wa hoja yake, Profesa Lipumba alisema hata Jaji Joseph Warioba katika taarifa yake alisema moja ya taasisi zilizotoa maoni ni Baraza la Wawakilishi lililopendekeza Serikali tatu.
“Tunadai kura za siri kusudi kuwalinda hawa wenzetu ambao wametoa misimamo, wakija kupiga kura hapa  inaweza kuwapa matatizo huko walikotoka,” alisema.
 Aliongeza : “Tunapolishabikia hili kuwa pasiwe na kura ya siri inaonekana wazi pana ajenda ya kuwashughulikia watakaokwenda kinyume cha msimamo.”
 3. Esther Bulaya (Viti Maalumu-CCM)
Bulaya, tofuti na wajumbe wenzake wengi kutoka chama tawala (CCM), alionekana kutoa mchango uliogusa hisia za wengi hasa pale alipoeleza bayana kuwa hayuko tayari kuona ukandamizaji unafanyika kumlazimisha apige kura ya wazi.
Akirejea msimamo wa kura ya wazi unaoshabikiwa na wajumbe wengi wanaotokana na chama chake, alisema hawezi kupiga kura ya aina hiyo wakati anajua inamnyima uhuru wake.
“Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko. Ni lini na wapi katika uamuzi mgumu kama huu kulifanyika kura za wazi kama wengi wanavyotaka,” alisema.

  4. Pandu Ameir Kificho (Mwenyekiti wa Muda)

Naye Kificho, ambaye pia ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, alionyesha kukerwa na baadhi ya vyombo vya habari hasa vilipolishikia bango suala la posho.
 “Kusema kweli, jamii tunaichanganya mpaka  jambo hili la kutupatia Katiba Mpya lionekane ni la mchezo au tumekuja kudai posho. Nawataka wenzetu (wanahabari) wawe makini sana juu ya jambo hili wasiupotoshe umma ili kazi hii isiingie dosari,” alisema.
“Vyombo vyote vya habari vizingatie kupata habari kwa uwazi na ukweli kutoka kwa wanaohusika ili jamii yetu ya Watanzania ipate habari za kweli na hilo la kupokea tu posho kwa kusoma magazeti tunalikanusha kwa nguvu zote”.

 5. Philemon Ndesamburo (Moshi Mjini-Chadema)
Ndesamburo aliwataka wajumbe wenzake kuacha ushabiki wa kisiasa na kutambua wanatengeneza katiba itakayodumu miaka 50 ama miaka 10 ijayo.
“Tusilete ushabiki. Nawaombeni sana tusilete ushabiki katika jambo hili. Hili ni jambo zito. Hili ni jambo tunalolifanya kwa niaba ya Watanzania milioni 45 na sisi tumepata bahati tu; ni Mungu ametusaidia,” alisema.

 6. Profesa Jumanne Maghembe (Waziri wa Maji)
Profesa Maghembe alifananisha upigaji wa kura kwa siri  kuwa sawa na ule uliofanyika nchini Marekani wakati wa kashfa ya ufuska iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa rais wakati huo, Bill Clinton.
“Kule Marekani walikuwa wakipiga kura ya kumwondoa madarakani Clinton kwa madai ya kushikwa ugoni. Walipiga kura ya wazi kwa sababu lilikuwa jambo kubwa la kumwondoa mtu madarakani,” alisema.
 Profesa Maghembe, ambaye pia ni Waziri wa Maji, aliwasihi wajumbe kutofautisha upigaji kura wa mwenyekiti wa kijiji, diwani, mbunge na rais ambao alisema wananchi hupiga kura za siri.
“Humu ndani tunatafuta sheria mama ya nchi. Tumepewa jukumu hilo kwa niaba ya Watanzania wote. Wao watapata nafasi ya kusema ndiyo au hapana. Sasa tunajificha ili iweje, tunamficha nani?” alihoji.
7. Sheikh Hemed Jengo
Sheikh Jongo alishauri Bunge Maalumu la Katiba kuwapa nafasi wajumbe wanawake watakaokuwa katika hedhi, waruhusiwe kuapa bila kushika kitabu kitukufu, Quran.
“Siku nyingine kinamama wanakuwa katika siku maalumu (hedhi). Ni haramu kwa mujibu wa dini kushika msahafu. Atakapojieleza kuwa hali yangu si nzuri, basi aruhusiwe kuapa hivyo hivyo kwa heshima,” alisema na kuongeza:
“Hata kwa wanaume wa Kiislaamu wakitaka kuapa wachukue udhu kwa sababu kitabu chenyewe kinakataza kukishika bila ya udhu. Ndiyo yamini. Ndiyo maana watu wengine hatuoni wanafanya vizuri kule nje kwa sababu wanajua waliapa bila udhu na haikuwa yamini.”

 8. Maria Sarungi Tshehai
Mwanaharakati huyo alitumia fursa aliyopewa kuwaponda wajumbe wenzake waliokwenda katika Bunge hilo kwa ajili ya kuwasilisha masilahi ya vyama.
“Hatuko hapa kwa ajili ya kuwasilisha vikundi mbalimbali. Tukianza hivyo itakuwa ni hatari sana katika Bunge hili,” alisema.
“Nianze kwamba kitu kilichonifanya nitoke nje nilifutwa (na mtu ambaye hakumtaja jina). Aliniambia wewe mbona unaonekana upo kwenye upande wa chama fulani.” 
9.Richard Ndassa (Mbunge wa Sumve)
Yeye alionekana kukerwa na baadhi ya taarifa za vyombo vya habari kuhusu suala la posho na kuvishtaki vyombo hivyo kwa mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho.
 “Wabunge wanachota milioni 129 kwa kikao cha dakika 30” na kingine kikisomeka, “Wabunge walipwa milioni 130 kwa dakika 25; Bunge la Katiba vipande vipande; wapewa posho kwa kusoma magazeti,” alisema akikariri vichwa vya habari vya baadhi ya magazeti na kudai vinamkera.
10. Dk. Zainab Gama
Naye mwanasiasa mkongwe, Dk. Zainabu Gama alikwenda mbali na kudai kuwa baadhi ya wanaotaka kura ya siri wametumwa na watu ama wamekula rushwa ndiyo maana hawataki kupiga kura ya wazi.
“Hatukuletwa hapa kimchezo mchezo.  Simama, sema mimi uamuzi  wangu huu kila mmoja akuone,” alisema.
MWANANCHI

Obama wants win for Museveni

  

Ugandan President Yoweri Museveni signs before the media the controversial anti-gay bill into law in Kampala last week before

The minister’s maid was in buoyant spirits and I could not help asking what was happening. “We have already won the 2016 elections,” she said cheerfully. “These days it is party mood at our house and my honourable is no longer depressed.”
“How can you win the elections a whole two years before they are held?” I asked.
“We thank President Barrack Obama for the victory,” she burst out. “Honourable says the moment Obama threatened us over the homosexuality law and other Western donors started following suit, Mzee’s victory was sealed. Unless something goes terribly wrong, we shall win with a landslide margin.”
“Are you sure?” I challenged.
“Positive!” She swore as she pointed her finger to the ceiling. “Honourable says Obama must have issued the warning in appreciation for our President’s role as a valuable ally in the war against terror.”
“I am not sure I understand,” I confessed. “Well the Americans are very clever,” she explained. “You should know that they collect a lot of intelligence information in the country all the time. Honourable says the US embassy spends colossal sums of money buying all types of information from government officials and careless politicians.
They know what everybody thinks from ministers to peasants in the villages. And since they have advanced systems of processing and sorting data, they can call up information on any subject in Uganda faster than our own government.
So they must have worked it out that since the last three general elections were quite gruelling and had to be fought bitterly, they decided to reward Mzee with a landslide win in the next elections so that he continues undisturbed.”
“I agree the Obamas may want Mzee to win, but what has the warning over the ant-homosexuality Act got to do with it?” I asked, still puzzled. “I have told you they gather all sorts of information,” she said becoming a bit impatient. “They needed to create something that can passionately touch the majority of the voters today, according to honourable.
So the anti-homosexuality Bill was not an accident. Some of the people arguing so passionately against or in favour do not even know this. By issuing the stern warning to Uganda over an issue that does not give Ugandans even one sleepless night, Mr Obama aroused interest in the phenomenon – and made an election issue out of it.
For unlike America, Uganda’s elections are not issue driven, unless you call the packets of sugar and soap that the honourables distribute to the voting villagers issues. Previously, the big issue of the elections was security, and Mzee won big because he was seen as its guarantor after ending insecurity in the country.
But now, most voters have been born under his rule the security question is taken for granted by them. Honourable said that the young people’s big concern which could have turned into an election issue is unemployment.

Ngome ya al-Shabaab yadhibitiwa Somalia

 

Vikosi vya serikali ya Ethiopia na Somalia vimedhibiti mji ulio katikati ya Somalia uliokuwa mikononi mwa wanamgambo wa al-Shabaab, maafisa wameeleza.

Takriban watu 12 waliuawa katika mapigano makali katika mji wa Radboore lililokuwa likizozaniwa lililo mjini Bakol, wakazi wa eneo hilo wameshuhudia.
Vikosi vya Ethiopia ni sehemu ya Wanajeshi 22,000 wa Umoja wa Afrika (AU) wanaopambana na wanamgambo nchini Somalia.
Imeelezwa kuwa kudhibitiwa kwa mji wa Radhoore ni hatua muhimu kwa kuwa ilikua ngome kuu ya al-shabaab katika kutekeleza mashambulizi mjini humo.
Huu ni mji wa kwanza ambao al-Shabaab walipoteza tangu mwezi Septemba, mji wa Mahaday ulipodhibitiwa toka mikononi mwa al-shabaab.
Hivi sasa vikosi vinaelezwa kuwa vinaelekea mji wa Hudur ambao pia unadhibitiwa na al-Shabaab.
Wanamgambo hao wenye uhusiano na al-Qaeda, wanadhibiti eneo kubwa la katikati mwa Somalia.

Crimea:kura yapigwa kujiunga na urusi

Wabunge wa Mji ulio kusini mwa Ukraine,Crimea wamepiga kura ili kuwa sehemu ya Urusi.
Bunge limesema uamuzi huo utaachwa mikononi kwa watu wa Crimea kwa ajili ya kupiga kura ya maoni tarehe 16 mwezi Machi.

Serikali ya Kiev imesema inaamini kuwa Crimea kujiunga na Urusi ni kinyume na Katiba.
Crimea, ambayo wakazi wake walio wengi wana asili ya Urusi, imekua katika malumbano baada ya kuanguka kwa Rais wa taifa la Ukraine.
Taarifa ya Bunge la Crimea imekuja wakati viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Brussels kujadili hatua ya kupeleka vikosi vya Urusi katika ardhi ya Ukraine.

Bunge la Crimea litatoa fursa kwa raia kukubali kujiunga na Urusi au la

 

PROIN PROMOTIONS LIMITED KUANZA KUSAKA VIPAJI VYA UIGIZAJI NCHINI TAREHE 1 APRIL 2014

Meneja wa Mradi wa Kusaka Vipaji Vya Uigizaji Tanzania (Tanzania Movie Talents) Bw Joshua Moshi akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wakutambulisha kampeni mpya ya kusaka Vipaji vya uigizaji kutoka kampuni ya Proin Promotions Limited mapema leo katika Ofisi za Proin Promotions Limited, Mikocheni, Mtaa wa Ursino, Pembeni ni Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited Bw Evance Stephen
Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited, Bw Evance Stephen (katikati) akielezea jinsi ya Kampuni ya Proin Promotions itakapozunguka katika Mikoa ya Tanzania Kwaajili ya Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania kwenye Mkutano na waandishi wa Habari mapema leo katika Ofisi za Proin Promotions Limited, Mikocheni, Mtaa wa Ursino,, Shindano litaendeshwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited.
 Meneja Mradi wa Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania (Tanzania Movie Talents) Bw Joshua Moshi (wa kwanza Kushoto) pamoja na Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited, Bw Evance Stephen wakisikiliza Maswali kutoka kwa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika Ofisi za Proin  zilizopo Mtaa wa Ursino Mikocheni
Muigizaji wa Filamu za Kitanzania Single Mtambalike almaarufu Rich Rich ambae pia ni mmoja wa majaji katika Shindano la kusaka vipaji vya uigizaji lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents lililopo chini ya Kampuni ya Proin Promotions Limited akiongelea jinsi washindi watakavyopatikana katika shindano hilo linalotarajia kuanza tarehe 1 Aprili 2014
 Mwandishi wa habari kutoka kituo cha Runinga Cha Channel Ten, Bw Fredy Mwanjala akiuliza swali kwa Meneja Mradi wa Tanzania Movie Talents, Bw Joshua Moshi (hayupo pichani) kuhusiana na Shindano la kusaka vipaji vya uigizaji nchini
 Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited, Bw Evance Stephen (wa kwanza kushoto) akionyesha stika za TRA ambazo zinaonyesha Uhalali wa filamu za Proin Promotions lakini Pia Wateja watakaonunua Filamu kutoka Proin Promotions wanatakiwa kutuma namba zilizopo kwenye stika hizo za TRA kwaajili ya kuweza kujishindia zawadi mbalimbali kutoka Proin Promotions kama Vile TV za Samsung na deki zake
 Meneja Masoko Wa Proin, Evance Stephen akionyesha Muhuri wa Moto uliopo kwenye Kasha la Filamu kutoka Proin Promotions, Muhuri wa Moto, Kasha jembamba na Stika za TRA ndio vitu vitatu vinavyooshesha Uhalali wa Filamu kutoka Proin Promotions Limited
Wakijibu Maswali Kutoka Kwa Waandishi wa Habari

Mapigano mapya mjini Juba


Wanajeshi wa waasi nchini Sudan Kusini
Wanajeshi watano wa serikali ya Sudan Kusini wameuawa kufuatia mapigano makali ndani ya kambi moja ya kijeshi mjini Juba.
msemaji wa jeshi la nchi hiyo amesema kuwa wanajeshi wengine watatu walijeruhiwa kwenye mapigano hayo iliyotokea katika kambi ya jeshi ya Jebel.
Mapigano kama hayo ndani ya kambi hiyo kati ya makundi hasimu yalisababisha mgogoro mkubwa wa kisiasa nchini humo.
Mkaazi mmoja wa Juba ameiambia BBC, kwamba moshi mweusi ulionekana ukitapakaa angani juu ya kambi hiyo karibu na chuo kikuu cha Juba na kwamba watu wameonekana wakilitoroka eneo hilo.
Akiongea muda mfupi kwenye runinga ya taifa muda mfupi baada ya mapigano hayo kuanza, Brigadier General Malak Ayuen Ajok amesema kuwa waliouwa ni wanajeshi waatiifu kwa serikali.
Amesema mapigano hayo yalisababisha na mvutano kati ya wanajeshi ambao walikuwa wakizozana kuhusu kucheleweshwa kwa mishahara yao.
Ajok, ameongeza kuwa hakuna dalili yoyote ya mapigano hayo kusambaa katika maeneo mengine ya mji huo.
Lakini watu wengi wanaoishi karibu na kambi hiyo ya wamekimbia makwao na kutafuta hifadhi katika piga makanisa na shule.
Mzozo wa Sudan kusini ulianza mjini Juba, mnamo mwezi Disemba mwaka uliopita kufuatia hali ya wasiwasi kati ya Rais Salva Kiir na aliyekuwa makamu wake wa rais Riek Machar lakini ukaenea kote nchini humo.Chanzo BBC Swahili

BUNGE MAALUM LA KATIBA LAAHIRISHWA KUTOKANA NA VURUGU

Mwenyekiti wa Muda wa Bunge  la Katiba Mh. Pandu Kificho ameahirisha Semina ya kujadili Kanuni za Bunge Maalum la Katika Kutokana na Vuruguru Kutokana na Hali ya Kutokuelewana Kati ya Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mh Ole Sendeka Kutoleana maneno na Mbunge Mwenzake wakati Mbunge Huyo alipohoji kuhusu Kanuni hizo.

balozi mdogo wa ethiopia amtembelea balozi mdogo wa tanzania dubai

 Balozi Mdogo wa Ethiopia Mhe. Yibeltal A. Alemu akikaribishwa na  Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Mhe. Omar Mjenga alipomtembelea ofisini kwake leo mjini Dubai.
Balozi Mdogo wa Ethiopia Mhe. Yibeltal A. Alemu na Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Mhe. Omar Mjenga katika mazungumzo. 

Katika mazungumzo yao wanadiplomasia hao  walipata fursa ya kuzungumzia njia muafaka na mbali mbali za kufanya kazi kwa karibu ili kuhakikisha wanavutia utalii na uwekezaji katika nchi zao hasa kwa kuwavutia wawekezaji kutoka wakubwa waliopo Dubai.

Mhe. Mjenga alimuomba Mhe. Yibeltal kubadilishana uzoefu wa Ethiopia katika kuvutia wawekezaji kutoka Dubai katika sekta ya kilimo. Alimuomba kuwa Maafisa wa Biashara kutoka Balozi zote mbili wakutane ili kubadilishana uzoefu huo ili Tanzania nayo iweze kuchukua mkondo huo kuwavutia wawejezaji kwenye kilimo.

OPERATION KOKORO YAVUNA WANACHAMA 1800 WILAYA YA MWANGA 

 

Ziara ya Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Mwanga Mkoa wa Kilimanjaro Komredi Japhar Mghamba akiongozana na Katibu Msaidizi wa Mkoa Maalum wa Vyuo Vikuu Komredi Daniel Zenda inaendelea kwa mafanikio makubwa katika wilaya hiyo ambapo mpaka sasa imefanikiwa kuingiza Vijana 1800 katika Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) pamoja na Chama.

Ziara hiyo iliyobeba jina la Operation Kokoro iliyoanza wiki iliyopita ilipata misikosuko hasa baada ya moja ya msafara wake kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana. Operation hiyo inayolenga kuhamasisha Vijana wa Upinzani na wasio na vyama kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhamasisha Vijana wa CCM kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi ujao wa Serikali za mitaa hapo baadae October mwaka huu pamoja na kukagua, kuhamasisha na kuelezea katika matawi na kata juu ya utekelezaji wa Ilani ya chama kwa kauli mbiu "CCM Mwanga Ukimya sasa Basi"

Operation kokoro tayari imeshapita katika kata ya Kisangara, na kuendelea katika milima ya upareni maeneo ya Ugweno, Msangeni, Kifula, Mamba na Kikweni. Viongozi hao wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wametembelea vikundi mbalimbali vya bodaboda, makundi ya wajasiriamali wadogo na wakubwa pamoja na kukagua miradi iliyoainishwa kwenye Ilani ya Chama ambayo inayoendelea kutekelezwa wilayani humo na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.

Viongozi hao wakiwa wanahutubia mkutano wa hadhara katika eneo la Msangeni wamesema kuwa wananchi waendelee kuiamini CCM kwani ndio Chama Bora Cha siasa ambacho kinasikiliza kero za wananchi wake na kuzitafutia ufumbuzi na kutaja kero mbalimbali ambazo tayari zimepatiwa ufumbuzi wa kudumu wilayani humo.

Ziara hiyo inaendelea katika kata na maeneo mengine ya wilaya ya Mwanga.

 

CCM, Chadema, CUF wanavuruga Bunge, asema Dovutwa

 

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Fahmi 

Dodoma. Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Fahmi Dovutwa alichafua hali ya hewa baada ya kuvituhumu vyama vya CCM, Chadema na CUF kuwa ndiyo vinavuruga Bunge kwa sababu ya misimamo yao.
Hali hiyo ilitokea wakati mjumbe huyo akichangia mjadala wa Rasimu ya Kanuni za Uendeshaji wa Bunge Maalumu la Katiba juzi.
Dovutwa alitoa shutuma hizo baada ya mjumbe mwingine, Julius Mtatiro kueleza kuwa amepitia Rasimu ya Kanuni lakini hakuona mahali panapoeleza mpangilio wa ukaaji wakati wa kupiga kura.
Hali hiyo ilimfanya Dovutwa, kusimama na kutoa tuhuma kuwa baadhi ya wajumbe wamehongwa na kwamba kuruhusu mpangilio maalumu ni kukaribisha mgawanyiko.
Alisema kukaa kwa mpangilio huo kutawapa nafasi viongozi mbalimbali kushinikiza wajumbe wao katika maamuzi ya mambo mbalimbali.
“Ukaaji wa sasa umezingatia masilahi ya nchi, utashi na matakwa ya wananchi. Watu wa CCM, CUF na Chadema ndiyo mnaharibu mkutano (Bunge),” alisema Dovutwa.
Dovutwa alisema vyama hivyo vinatofautiana katika masuala mbalimbali na misimamo yao ndiyo imetawala bunge hilo.
“Mnatulazimisha tuwasikilize nyie tu. Kwa hiyo Mwenyekiti usikubali, kikao hiki kizingatie masilahi mapana ya makundi mbalimbali,” aliongeza Dovutwa.
Baada ya kutamka hilo, mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kupitia Kanuni, Amon Mpanju alisimama na kumtaka Kificho kulisaidia Bunge hilo kwenda na utaratibu aliowatangazia juzi wajumbe, ambao wanatakiwa kuwasilisha hoja zao kwenye kamati kisha kutolewa uamuzi.
“Naomba uamuzi ukishafanyika, kiti chako kisiruhusu mtu mwingine kuingilia maana mchakato hautafika mwisho. Nawaomba wajumbe wenzangu tusilete michango inayoweza kuleta hisia za mgawanyiko miongoni mwetu,” alisema Mpanju.
Mtatiro alisema hakupendezwa na mchango wa Dovutwa na kutahadharisha ukweli hauwezi kukwepeka kwa kuwa kuna watu wanaotoka katika makundi mbalimbali.
“Wakati wa kupiga kura tunahitaji theluthi mbili ya wajumbe wa Tanzania Bara na idadi kama hiyo kwa wajumbe kutoka Zanzibar kwa hiyo ili kurahisisha kazi hiyo, wajumbe kutoka Zanzibar wakae upande wao na wale wa Bara wakae upande wao,” alisema Mtatiro.

Pinda, Werema wabishana utaratibu wa hotuba

Dodoma. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema wamepingana hadharani kuhusu anayepaswa kuwa wa kwanza kuhutubia Bunge kati ya  Rais Jakaya Kikwete au Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,  Jaji  Joseph Warioba.
 Mabishano hayo yalitokea juzi wakati wajumbe wakichangia Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, mjini Dodoma.
Ubishi baina ya vigogo hao wa serikali ulizuka baada ya Jaji Werema kusema kuwa kanuni ya saba inaelekeza Jaji Warioba ndiye anayepaswa kuwasilisha Rasimu ya Pili ya Katiba, lakini Sheria ya Mabadiliko ya Katiba haijasema kama Rais anapaswa kuhutubia kwenye ufunguzi wa Bunge la Katiba.
Pinda aliingilia mabishano hayo kwa kuelekeza kuwa Jaji Warioba atawasilisha rasimu hiyo na kufuatiwa na hotuba ya ufunguzi itakayotolewa na Rais Kikwete.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka.
Hata hivyo, Mjumbe wa Kamati ya Kanuni, Ismail Jussa alisema hakuna kipengele cha sheria kinachozungumzia hotuba ya Rais ambacho katika utungaji wa kanuni kingefanywa kuwa na kifungu cha peke yake.

 

Wanajeshi watano wauawa Afghanistan

Wanajeshi watano wa Afghanistan wameuawa na wengine wamejeruhiwa katika jimbo la Logar.Maafisa wa Afghanistan wamesema kuwa walilengwa kimakosa na Ndege isiyo na rubani ya Marekani.
Majeshi ya jumuia ya kujihami, NATO yametoa salamu za rambirambi kwa familia za wanajeshi na kuanzisha uchunguzi ili kubaini namna tukio hilo lilivyotokea.
Rais wa Afganistan, Hamid Karzai,amekua akikosoa Operesheni na mashambulizi ya anga yanayofanywa na Vikosi vya kimataifa ambavyo vimegharimu maisha ya Raia wa nchi hiyo.
Karzai alikataa kutia saini makubaliano na marekani ya kuridhia kubaki kwa sehemu ya vikosi vya kimataifa nchini Afghanistan, baada ya kumalizika kwa Operesheni yao mwaka huu.

 

Saadi Gaddafi ashikiliwa Tripoli

Serikali ya Libya imesema kuwa mtoto wa Kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Saadi Gaddafi, ameondoshwa nchini Niger hivi sasa anashikiliwa mjini Tripoli.

 

Saadi alitoroka baada ya baba yake, Kanali Muammar Gaddafi kuuawa wakati wa mapinduzi yaliyofanyika mwaka 2011 nchini Libya.
Anashutumiwa kuwafyatulia risasi waandamanaji na anadaiwa kutekeleza uhalifu mwingine wakati wa utawala wa baba yake, yeye alipokuwa Kiongozi wa vikosi maalum vya kijeshi.
Serikali ya Libya imetoa taarifa hiyo mapema siku ya alhamisi kuwa wamempokea akitokea Niger.
awali , Niger ilikataa ombi la Libya ilipotaka imsafirishe Saadi, huku waziri wa sheria wa Niger akihofu kuwa Saadi atahukumiwa adhabu ya kifo.

 

Juhudi za Kerry zagonga mwamba Paris

 

Katika njia Panda: Sergei Lavrov na John Kerry.
Juhudi za marekani kuwakutanisha kwa mara ya kwanza ana kwa na mawaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi na Ukraine kuhusu mzozo unaoendelea katika jimbo la Crimea zimegonga mwamba.
Ingawa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Marekani John Kerry amekanusha kwamba palikuwa na nia ya kumkutanisha mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov na waziri mpya wa mashauri ya nchi za wa Ukraine Andrii Deschchytsia iwapo wawili hao wangekutana mjini Paris ingekuwa ni mafanikio makubwa ya kidiplomasia.
Sergei Lavrov alikataa kukutana na waziri huyo mpya wa Ukraine kwa sababu Urusi haitambui utawala mpya wa mjini Kiev. Akizungumza mjini Paris Bwana Deschchytsia amesema licha ya vuta nikuvute hiyo anaamini kwamba kuna dalili ya mafanikio katika mashauri.
" Kwa hiyo baada ya kuwa hapa siku nzima mjini Paris, inaonekana kwamba tunaendelea na mashauri yetu na tunaamini kwamba tutapata mwafaka. Ninaelekea mjini Brussels kukutana na waziri mkuu kujadili hatua zaidi za kuchukua. Shukran."
Na alipoulizwa na mmoja waandishi wa habari ni kwa nini hakuweza kukutana na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi Sergey Lavrov hivi leo, bwana Deschchytsia alijibu- ''kamuulize Lavrov mwenyewe.''
Mwanajeshi wa Ukraine akilinda meli ya kivita iliyozuiliwa na Urusi katika bandari ya Sevastopol.
Hata hivyo bwana Lavrov alifanya mazungumzo ya kina na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry na mawaziri wengine wa umoja wa ulaya. Bwana Kerry alitaja mkutano huo kuwa mgumu lakini akasema ana ujumbe atakaoupeleka kwa rais Obama na mazungumzo yataendelea.
Waziri wa mashauri ya nchini za kigeni wa Ufaransa Laurent Fabius kadhalika alielezea matumaini ya mazungumzo hayo kufanikiwa.
" Tumekubaliana kuendelea na mashauri kwa sababu mambo bado na hali sio rahisi anasema bwana Fabius. Lakini tunayo furaha kwamba siku ya leo mjini Paris imeturuhusu kuanzisha mikakati.''
Kwa upande mwingine rais wa Urusi Vladmir Putin alifanya mazungumzo kuhusu mzozo huo na chanzela wa Ujerumani Angela Merkel kwa njia ya simu.
Wakati huo huo Mwakilishi mkuu wa Umoja wa mataifa huko Crimea, Robert Serry, amelazimika kukatiza ujumbe wake baada ya kutishiwa na watu waliojihami alipokuwa akitoka katika makao makuu ya jeshi la wanamaji la Ukraine katika bandari ya Simferopol.