Thursday 6 March 2014

Pinda, Werema wabishana utaratibu wa hotuba

Dodoma. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema wamepingana hadharani kuhusu anayepaswa kuwa wa kwanza kuhutubia Bunge kati ya  Rais Jakaya Kikwete au Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,  Jaji  Joseph Warioba.
 Mabishano hayo yalitokea juzi wakati wajumbe wakichangia Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, mjini Dodoma.
Ubishi baina ya vigogo hao wa serikali ulizuka baada ya Jaji Werema kusema kuwa kanuni ya saba inaelekeza Jaji Warioba ndiye anayepaswa kuwasilisha Rasimu ya Pili ya Katiba, lakini Sheria ya Mabadiliko ya Katiba haijasema kama Rais anapaswa kuhutubia kwenye ufunguzi wa Bunge la Katiba.
Pinda aliingilia mabishano hayo kwa kuelekeza kuwa Jaji Warioba atawasilisha rasimu hiyo na kufuatiwa na hotuba ya ufunguzi itakayotolewa na Rais Kikwete.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka.
Hata hivyo, Mjumbe wa Kamati ya Kanuni, Ismail Jussa alisema hakuna kipengele cha sheria kinachozungumzia hotuba ya Rais ambacho katika utungaji wa kanuni kingefanywa kuwa na kifungu cha peke yake.

 

No comments:

Post a Comment