Monday 10 March 2014

Syria yawanyima chakula wakimbizi

 

Serikali ya Syria inadaiwa kutumia mbinu zisizofaa kuwanyima chakula, raia, wasio na hatia na ambao pia ni wakimbizi.
Shirika la kimataifa la Amnesty International linasema kuwa serikali inatumia njia ya kuwanyima chakula raia kama silaha dhidi ya wakimbizi ambao wako katika kambi za wakimbizi na ambao wanahitaji msaada wa dharura.
Kwa mujibu wa shirika hilo wakimbizi 128 wamefariki katika kambi ya wakimbizi ya Yarmouk mjini Damascus kutokana na kukosa chakula.
Shirika hilo linasema kuna hali ngumu ya kibinadamu inayowakabili wakimbizi hao.
Shirika la Amnesty linasema kuwa familia nyingi zimelazimika kutafuta chakula katika jaa za takataka na kuhatarisha maisha yao.
Kulikuwa na ripoti za mapigano mapya kuzuka karibu na kambi hiyo mapema wiki hii.
Mwandishi wa BBC Rami Ruhayem, anasema kuwa mapigano yalisitishwa kwa muda ili kuweza kuwafikishia chakula wakimbizi mjini Damascus
Kambi ya Yarmouk ambayo inawahifadhi wakimbizi 17,000 hadi 20,000 wa kipalestina na wengine raia wa Syria, imeshuhudia vita vikali mno katika siku za hivi karibuni.
Kambi yenyewe imekuwa bila stima tangu Aprili mwaka 2013 na nyingi ya hospitali za mji huo zimefungwa baada ya kukosa vifaa muhimu.

 

POLISI YAAGIZWA KUSAKA DAWA ZA SERIKALI ZENYE NEMBO YA MSD KATIKA MADUKA YANAYOUZA DAWA BARIDI NCHINI KOTE.

Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini ambaye ni Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka akisindikizwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya MSD (Kulia) Prof. Idris Alli Mtulia na Kushoto kabisa ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Madawa nchini (MSD) Bw. Cosmas Mwaifwani wakati wa sherehe za uzinduzi wa Kituo cha kuhifadhi na usambazaji dawa Wilayani Muleba Mkoani Kagera. 

Kituo kipya cha muda cha Kutunza na Usambazaji Dawa cha Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kilichozinduliwa Jumamosi na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Akimwakirisha Makamu wa Rais Dk. Mohamerd Ghalib Bilal ) kilichopo eneo la Mahalahala Wilayani Muleba Mkoa wa Kagera. 
MKurugenzi wa MSD Kanda Makao Makuu Dar es salaam Mr Tell akiteta jambo na Meneja wa MSD Kanda ya Mwanza Tabula Byekwaso kabla ya kuanza kwa sherehe za uzinduzi wa Kituo kipya cha muda cha Kutunza na Usambazaji Dawa cha eneo la Mahalahala Wilayani Muleba March 8 Mwaka huu.
Wanawake ambao ni wananchi wa Wilaya ya Muleba na maeneo ya jirani na Kituo kipya wakijumuika na baadhi ya watumishi wa MSD kusakata dansi la Bendi ya Muziki ya Kakao eneo la uzinduzi Mahalahala Wilayani Muleba.
Waibaji na wacheza show wa Bebdi ya Kakao wakitumbuiza kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo kipya cha MSD eneo la Mahalahala Muleba.
Viongozi Jukwa Kuu wakishiriki kusakata rumba la Kakao Bandi
Afisa Habari wa MSD Makao Makuu (Mwenye Kipeperushi cha Bendera ya MSD) na Baadhi ya watumishi wakifuatilia kwa umakini shughuli za uzinduzi wa Kituo kipya 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Madawa nchini (MSD) akitoa taarifa fupi ya MSD kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo kipya.
Zamu ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Prof. Idris Alli Mtulia akitoa hutuba yake wakati wa uzinduzi wa Kituo hicho.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk Stephen Kebwe Aliyemwakirisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamerd Ghalib Bilal akihutubia viongozi, watumishi wa MSD na wananchi wakati wa uzinduzi wa kituo kipya cha MSD Wilayani Muleba
Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka  ambaye ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi akitoa hotuba ya shukurani za wananchi wa Wilaya ya Muleba na Mkoa wa Kagera kwa kuzinduliwa kwa kituo kipya cha MSD Wilayani Muleba.
Baadhi ya wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali ya uzinduzi wa kituo kipya cha MSD Muleba.
Kakao Bandi wakiwa kazini kutumbuiza wakati wa sherehe 
Baadhi ya wanawake wakifuatilia tukio la uzinduzi 
Kazi ni moja tu kushambulia ndani ya viwanja vya uzinduzi wanamuziki wa Kakao Bandi.
"Haya Mheshimiwa Mbunge sasa nakata utepe kuzindua rasmi usambazaji dawa za serikali ulio chini ya MSD" ni Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Kebwe akishuhudiwa na Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Tibaijuka (Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini)  
"Haya tupige makofi kwa pamoja kuashiria kukubali uzinduzi huu" Naibu Waziri Dk. Kebwe (Kulia), Waziri Prof. Tibaijuka (Katikati) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu MSD Bw. Mwaifwani
Meneja wa MSD Kanda ya Mwanza Tabula akiwa na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Prof. Tibaijuka ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD Prof. Mtulia (Mwenye suti) wapili Kulia, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Kebwe (Nyuma mwenye suti) na Mkurugenzi MSD Kanda Makao Bw. Tell (Mwenye miwani aliyevaa shati nyeupe nyuma) 
Ramani kuonyesha Mfumo wa Usambazaji Dawa kutoka MSD kwa kauli mbiu yake kufikisha dawa moja kwa moja hadi vituo vya kutolea huduma za afya ikiwa ni Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya na Teule, Mkoa na Rufaa maeneo yote nchini.
Baada ya kumalizikehe kwa sherehe za uzinduzi Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini alianzisha maandamano ya Amani kuunga mkono juhudi za serikali kufikisha huduma ya dawa na vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Madawa (MSD) nchini kote ili kupunguzi vifo vya mama na watoto, mapambanaona ugonjwa  wa UKIMWI na Malaria.
Na Peter Fabian.
ALIYEKUWA MULEBA.

MAKAMU wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal ameiagiza Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kushirikiana na Jeshi la Polisi nchini kufanya msako endelevu ili kuwafichua, kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaopatikana na Dawa za Serikali kinyume cha taratibu na sheria zilizopo.

Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Stephen Kebwe (MB) wakati wa ufunguzi rasmi wa Kituo cha Kutunza na Usambazaji Dawa (Bohari ya MSD) cha muda kilichopo eneo la Mahalahala kwenye Hospitali inayojengwa ya Wilayani Muleba juzi alisema wizi na upotevu wa dawa hizo zinazotolewa na serikali hufanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu.

Alieleza kwamba Kituo cha Muleba (Bohari ya Madawa ya MSD) cha muda kitakuwa na jukumu kubwa la kusambza dawa na vifaa tiba kwa ajili ya Hospitali na Vituo vya Afya katika maeneo yote ya Wilaya za Mikoa ya Kagera (Vituo 270 ) na Geita (Vituo 64) kuanzia mwezi julai mwaka 2013 mfumo huu wa usambazaji dawa ulianza kabla ya kufunguliwa rasmi.

Makamu wa Rais Dk. Katika hotuba hiyo ameipongeza Bohari Kuu ya Madawa (MSD) nchini kwa kuanzisha utaratibu wa kuweka alama ya Government Of Tanzania (GOT) katika dawa zinazosambazwa na kusema kuwa hatua hiyo itasaidia dawa za serikali kutambulika kiurahisi kwa wananchi pamoja na kuthibiti wauzaji wa maduka ya dawa baridi wanaopelekewa zinazoibiwa na watumishi wa serikali.

“Lengo kubwa la kufunguliwa kituo hichi ni kupunguza vifo vya akina mama na watoto, kupambana na ungonjwa wa UKIMWI na Malaria ikiwa ni kuanza kutumia mfumo wa fikisha dawa karibu na wananchi na kwa wakati ili kufanikisha lengo mahususi la serikali ya awamu ya nne huku ufatiliaji wake uwe chini ya usimamizi wa karibu na matumizi ya dawa zinazosambazwa kwenye vituo vya huduma ” alisisitza

Kwa upande wake Naibu Waziri Dk. Kebwe amesikitishwa na taarifa ya kasi ya wizi na upotevu wa dawa zinazopelekwa na serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) katika Wilaya za Ngara, Kerwa, Biharamulo na Muleba huku akizipongeza Wilaya za Karagwe na Bukoba vijijini kwa kuweka jukumu la udhibiti wizi na upotevo wa dawa hizo kutoka kwa watumishi wasio waadilifu.

Dk. Kebwe ameungana na Makamu wa Rais Dk. Bilal kuzitaka Kamati za ulinzi na usalama za Mikoa ya Kagera na Geita na zile za Wilaya kwa kushirikiana na Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri zote kufatilia kwa ukaribu huku akitaka taarifa za upokeaji dawa na utolewaji kwa wananchi utolewe kwenye Vikao vya Kamati ya Ushauri na Maendeleo (RCC) za Mikoa yote.

“Tusikubaliane na wajanja wachache wa Idara za Afya kutumia mwanya wa kuiba dawa na kuziuza kwenye maduka waliyoanzisha na kisha kujinufaisha kwa kununua magari, kujenga vyumba za kifahari nasi kuwashangilia eti muda mchache jamaa ana gari zuri ambapo makusanyo ya mapato kutoka vituo vya afya kuonyesha ni asilimia 50 tu huku zingine zikiliwa na wajanja wachache” alisema.

Dk. Kabwe alisema kuwa Wizara yake itatumia bilioni 6 kwa mwaka katika Dawa zote zitakazotolewa na kituo hicho na kila mwezi kitasambaza dawa za kiasi cha shilingi milioni 150 huku Bajeti ya Wizara ikionekana kutumia Bilioni 80 za Dawa, Vifaa tiba na Vitenganifu na kupitia kituo hicho ndani ya siku 14 Hospitali na Vituo vya Afya vitapeka oda na kupatiwa dawa.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa MSD, Porfesa Idrisa Mtulia kuzinduliwa kwa kituo hicho ni mkombozi mkubwa wa wananchi wa Mkoa ya Kagera na Mkoa wa jirani wa Geita na Wilaya zake zote ambapo kitawezesha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na viunganifu vya kutolea huduma ya afya kwa Bohari ya madawa kufikisha haraka huduma zake kwa wateja.

Prof. Mtulia alisema kwamba pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili MSD itahakikisha inashirikiana na serikali na wadau wengine kuendelea kutoa huduma bora na kufikisha dawa zenye ubora na bei nafuu wakati wote kwa manufaa ya watanzania wote  huku akihimiza Halmashauri zote nchini kukunua dawa kutoka MSD kwa kutumia vyanzo vyake vingine vya fedha.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) nchini Cosmas Mwaifwani alisema kwamba kutokana na ukubwa wa Kanda ya Ziwa na idadi kubwa ya wingi wa watu zaidi ya milioni 13 kutokana na matokeo ya Sensa ya mwaka 2012 kuwepo na malalamiko ya wadau mbalimbali juu ya huduma za MSD Kanda ya Mwanza kutokidhi kwa wakati huduma ya utoaji wa dawa.

Kaimu huyo alieleza kuwa imefungua kituo hicho cha muda kuhakikisha upatikanaji na usambazaji wa Kituo cha Muleba kinafanikisha lengo la MSD na kupunguza usumbufu wa Mkoa wa Kagera kufata huduma hiyo Jijini Mwanza na Kanda ya Tabora ambapo ilionekana kuchelewesha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba vyenye ubora na kwa bei nafuu kwa watanzania wote.

Ufunguzi wa Kituo hiki cha usambazaji dawa Mkoani Kagera na Mkoa wa jirani wa Geita ni mchango mkubwa wa utekelezwaji wa Malengo ya Millenia hususani kupunguza vifo vya mama na watoto na kupambana na Ukimwi na Malaria ambayo imekuwa ni magonjwa ya mlipuko katika maeneo mengi ya Wilaya za Muleba ” Alisema Mwaifwani.
Mbunge wa Muleba Kusini Porfesa Anna Tibaijuka ambaye ni Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwahakishia Naibu Waziri Dk. Kebwe na uongozi wa MSD kuwa eneo la Ekhali 5 zilizotolewa na Halmashauri Wilaya ya Muleba linaachwa wazi ili kutoa nafasi kwa MSD kujenga Ofisi kuu na Maghala ya kuhifadhiwa dawa Mkoani humo.

“Kituo hiki ni wajibu wetu kukilinda na kukitunza vizuri ili kiendelee kutoa huduma, lakini Mkurugenzi wa Halmashauri naomba utumia sheria za ardhi zilizopo kuhakikisha unawaondosha watu wanaovamia eneo tulilotenga kwa ajili ya shughuli za MSD hili ni agizo natoa kama Waziri nila serikali siyo langu kama Mbunge wa Jimbo hili” alisisitiza.

Mbunge huyo aliongeza kuwa kutokana na waathilika wakubwa ni Kimama na watoto pamoja na Wilaya hiyo kukubwa na magojwa ya mlipuko hususani Malaria ambayo yalipelekea serikali na Wizara ya Afya kutuma wataalamu na kufanya utafiti kisha kuanzisha mkakati wa kupulizia dawa ya Ukoko kwenye nyumba za Wilayah ii ili kudhibiti ugonjwa huo uliokuwa ni janga kwa wananchi

Profesa Ibrahim Lipumba aifunda Chadema Dar

 

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetakiwa kuweka kando tofauti za kisiasa na kuunganisha nguvu zao, hasa katika kipindi hiki ambacho taifa lipo katika mchakato wa uundaji wa Katiba Mpya.
Wito huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba alipokuwa akifungua mkutano wa baraza kuu la chama hicho.
Alisema kuwa chama hicho chenye wabunge wengi kinapaswa kutafakari na kuweka kando itikadi za vyama na kuangalia mustakabali wa nchi katika kipindi muhimu.
“Ningependa kuwashauri Chadema kama chama chenye wawakiishi wengi bungeni kinapaswa kuweka kando tofauti za kisiasa na kuunganisha nguvu katika kwa kuangalia masilahi na mustakabali wa taifa,” alisema
“Licha ya changamoto tulizonazo hakuna sababu ya kukata tamaa mapema kiasi hiki, tunapaswa kuondoa tofauti zetu za kisiasa a.”
Kauli hiyo ya Lipumba inakuja kutokana na vuguvugu la mgogoro ulioibuka hivi karibuni ndani ya Chadema ambao ulisababisha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe kuvuliwa nafasi zake zote za uongozi.
Uamuzi huo pia ulimkumba aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho Dk Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

 

Vurugu bungeni zawakera wasomi

Dar es Salaam. Vurugu na mivutano inayoendelea katika Bunge Maalumu la Katiba imewakera baadhi ya wasomi ambao kwa nyakati tofauti, wamesema kinachoendelea sasa ni matokeo ya mchakato mbovu wa namna ya kupata Katiba Mpya.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally alisema kinachoendelea bungeni ni ugonjwa ulioanza tangu mchakato wa Katiba ulipoanza.
“Ugonjwa hauko bungeni bali mfumo mzima, watu wanakosea lakini tusiwalaumu ni sheria yenyewe haiku vizuri,” alisema Ally.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa George Shumbusho alisema vurugu za bungeni zinatokana na kuwajumuisha wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na wale wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, katika Bunge la Katiba.
“Wabunge wetu ndio chanzo cha vurugu, ndio utagundua wapi tulikosea,” alisema Profesa Shumbusho.
Godfrey Missana wa Dar es Salaam alisema kama wajumbe wa Bunge hilo wanabishana na kutofautiana katika hatua ya kutunga kanuni, hali inaweza kuwa mbaya zaidi wakati wa kuandaa Katiba Mpya.
Alex Charles mkazi wa jijini Mwanza alielezea wasiwasi kama kweli Katiba hiyo inaweza kupatikana Aprili 26 mwaka huu.

 

Foleni yazua maradhi mapya 


Dar es Salaam. Wakati kukiwa na ongezeko kubwa la ununuzi wa magari na kusababisha idadi kubwa ya vyombo hivyo vya usafiri, foleni za magari nchini, hasa jijini Dar es Salaam, imefikia hatua ya kutisha huku ikisababisha madhara makubwa kiuchumi, kijamii na kiafya, ikiwamo magonjwa ya akili.
Misululu ya magari ilikuwa ni ya kawaida kuonekana nyakati za asubuhi na jioni wakati watu wakielekea na kutoka kazini, lakini sasa foleni zimekuwa ni za kawaida katikati ya jiji na maeneo mengine ambayo ukarabati wa barabara unaendelea wakati wote.
Wakati kukiwa na kasi ndogo ya ukarabati wa miundombinu ya usafiri, kumekuwa na ongezeko kubwa la magari jijini Dar es Salaam. Pia kumekuwapo na ongezeko kubwa la idadi ya watu hadi kufikia milioni 4.3 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002 huku vyombo vya usafiri wa umma (daladala) vikitumia njia zisizo sahihi (kutanua), kufanya foleni kuwa kubwa hali inayosababisha jiji kuwa kero kwa muda wote.
Licha ya jitihada za Serikali kutumia treni kusafirisha abiria ili kusaidia kupunguza msongamano wa magari nyakati za asubuhi na jioni, bado tatizo hilo ni kubwa. Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuri aliagiza Kampuni ya Strabag, inayojenga miundombinu ya mabasi yaendayo kasi, kufungua barabara zilizokamilika ili kupunguza msongamano.
Kutokana na tatizo hilo, wakazi wa Dar es Salaam na maeneo mengine yanayoathiriwa na foleni, wamekuwa wakilazimika ama kusitisha safari au kuchelewa kazini na kwenye shughuli nyingine, huku vyombo vya usafiri vikilazimisha kufanya safari chache na hivyo wamiliki kupata fedha kidogo kuliko matarajio yao.
“Madereva wanapata magonjwa ya akili kutokana na kero za barabarani,” alisema Dk. Innocent Godman, ambaye ni mmoja wa wataalamu wa nyanja tofauti aliyeongea na gazeti hili kuhusu tatizo hilo.
“Kwanza ni msongo wa mawazo kuhusu uchumi kutokana na mafuta mengi kupotea njiani; pili barabara mbovu; tatu hasira za kuchelewa anakokwenda; na nne wanakumbana na askari wa usalama barabarani ambao wanawakamua fedha,” alisema mtaalamu huyo wa magonjwa ya akili na mshauri nasaha kuhusu utumiaji wa madawa ya kulevya.
Tanzania inaelezwa ni nchi inayoongoza kwa kuwa na msongamano mkubwa wa magari katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Zatafuna mabilioni ya shilingi
Katika utafiti wake, Wakala wa Mradi wa Mabasi ya Kasi (DART), Jumbe Katala amebaini kuwa foleni husababisha ajali za barabarani, upotevu wa nishati (mafuta) na muda wa kukaa barabarani mambo ambayo husababisha hasara ya zaidi ya Sh655 bilioni kwa mwaka.
Katika utafiti huo, Katala alibaini kuwa foleni hizo husababisha kudorora kwa uchumi, huku bei ya mafuta ipanda kutokana na mahitaji ya nishati hiyo kuongezeka.
Alisema kuendesha na kuzima gari mara kwa mara kwa sababu ya foleni huongeza matumizi makubwa ya gari na kuongeza kasi ya uchakavu wake, hivyo kusababisha gharama kubwa za matengenezo ya mara kwa mara.

 

Obama amualika Waziri Mkuu wa Ukraine

Rais wa Marekani Barrack Obama, amemualika waziri mkuu wa Ukraine, Arseniy Yatsenyuk, mjini Washington kwa mashauriano kuhusiana na mzozo unaokumba taifa lake.
Ikulu ya White House, imesema kuwa mkutano huo utakaofanyika siku ya Jumatano, utaangazia, mbinu za kutafuta suluhisho la amani, kuhusiana na operesheni za kijeshi zinazoendesha na jeshi la Urussi katika eneo la Crimea.
Waandishi wa habari wanasema kuwa mualiko huo ni ni ishara thabiti kuwa Marekani inaunga mkono utawala wa mpito wa Kiev.
Wakati huo huo, jamii ya kimataifa inaendelea kuishinikiza utawala wa Moscow, kuondoa wanajeshi wake katika eneo la Crimea.
Chansella wa Ujerumani, Angela Merkel, amemueleza rais wa Urussi, Vladimir Putin, kutilia maanani kuwa kura ya maoni kuhusu ikiwa eneo hilo la Crimea, litajiunga na Urussi inakiuka sheria na ni haramu.

Khodorkovsky apinga utawala wa Moscow

Rais Obama
Huku hayo yakijiri, mfungwa wa zamani na mfanya biashara maarufu wa secta ya mafuta na mkoasoaji mkubwa wa rais Putin, Mikhail Khodorkovsky, anehutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
Amewaambia maelfu ya watu waliofurika katika medani ya Uhuru kuwa serikali ya Urussi inawahadaa raia wake kwa kuwahusisha waandamanaji mjini Kiew na watu wanaopinga utawala wake na raia wake.
Mikutano kama hiyo imefanyika katika sehemu kadhaa za nchi hiyo.
Nyingi zikiwa za amani lakini mjini Sevastopol, katika eneo la Crimea, raia wa Ukraine wanaozungumza lugha ya Kirussi waliwapiga watu wanaounga mkono serikali ya Ukraine.
Televisheni zilizo na makao yao mjini Kiev zimezuiliwa kurusha matangazo katika eneo hilo la Crimea.

 

Obama amualika Waziri Mkuu wa Ukraine

Rais wa Marekani Barrack Obama, amemualika waziri mkuu wa Ukraine, Arseniy Yatsenyuk, mjini Washington kwa mashauriano kuhusiana na mzozo unaokumba taifa lake.
Ikulu ya White House, imesema kuwa mkutano huo utakaofanyika siku ya Jumatano, utaangazia, mbinu za kutafuta suluhisho la amani, kuhusiana na operesheni za kijeshi zinazoendesha na jeshi la Urussi katika eneo la Crimea.
Waandishi wa habari wanasema kuwa mualiko huo ni ni ishara thabiti kuwa Marekani inaunga mkono utawala wa mpito wa Kiev.
Wakati huo huo, jamii ya kimataifa inaendelea kuishinikiza utawala wa Moscow, kuondoa wanajeshi wake katika eneo la Crimea.
Chansella wa Ujerumani, Angela Merkel, amemueleza rais wa Urussi, Vladimir Putin, kutilia maanani kuwa kura ya maoni kuhusu ikiwa eneo hilo la Crimea, litajiunga na Urussi inakiuka sheria na ni haramu.

Khodorkovsky apinga utawala wa Moscow

Rais Obama
Huku hayo yakijiri, mfungwa wa zamani na mfanya biashara maarufu wa secta ya mafuta na mkoasoaji mkubwa wa rais Putin, Mikhail Khodorkovsky, anehutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
Amewaambia maelfu ya watu waliofurika katika medani ya Uhuru kuwa serikali ya Urussi inawahadaa raia wake kwa kuwahusisha waandamanaji mjini Kiew na watu wanaopinga utawala wake na raia wake.
Mikutano kama hiyo imefanyika katika sehemu kadhaa za nchi hiyo.
Nyingi zikiwa za amani lakini mjini Sevastopol, katika eneo la Crimea, raia wa Ukraine wanaozungumza lugha ya Kirussi waliwapiga watu wanaounga mkono serikali ya Ukraine.
Televisheni zilizo na makao yao mjini Kiev zimezuiliwa kurusha matangazo katika eneo hilo la Crimea.

 

Obama amualika Waziri Mkuu wa Ukraine

Rais wa Marekani Barrack Obama, amemualika waziri mkuu wa Ukraine, Arseniy Yatsenyuk, mjini Washington kwa mashauriano kuhusiana na mzozo unaokumba taifa lake.
Ikulu ya White House, imesema kuwa mkutano huo utakaofanyika siku ya Jumatano, utaangazia, mbinu za kutafuta suluhisho la amani, kuhusiana na operesheni za kijeshi zinazoendesha na jeshi la Urussi katika eneo la Crimea.
Waandishi wa habari wanasema kuwa mualiko huo ni ni ishara thabiti kuwa Marekani inaunga mkono utawala wa mpito wa Kiev.
Wakati huo huo, jamii ya kimataifa inaendelea kuishinikiza utawala wa Moscow, kuondoa wanajeshi wake katika eneo la Crimea.
Chansella wa Ujerumani, Angela Merkel, amemueleza rais wa Urussi, Vladimir Putin, kutilia maanani kuwa kura ya maoni kuhusu ikiwa eneo hilo la Crimea, litajiunga na Urussi inakiuka sheria na ni haramu.

Khodorkovsky apinga utawala wa Moscow

Rais Obama
Huku hayo yakijiri, mfungwa wa zamani na mfanya biashara maarufu wa secta ya mafuta na mkoasoaji mkubwa wa rais Putin, Mikhail Khodorkovsky, anehutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
Amewaambia maelfu ya watu waliofurika katika medani ya Uhuru kuwa serikali ya Urussi inawahadaa raia wake kwa kuwahusisha waandamanaji mjini Kiew na watu wanaopinga utawala wake na raia wake.
Mikutano kama hiyo imefanyika katika sehemu kadhaa za nchi hiyo.
Nyingi zikiwa za amani lakini mjini Sevastopol, katika eneo la Crimea, raia wa Ukraine wanaozungumza lugha ya Kirussi waliwapiga watu wanaounga mkono serikali ya Ukraine.
Televisheni zilizo na makao yao mjini Kiev zimezuiliwa kurusha matangazo katika eneo hilo la Crimea.

 

Ndege ya Malaysia iliyotoweka haijapatikana

Wakati juhudi za kuisaka ndege iliyopotea ilipokuwa ikisafiri kutoka Malaysia kuelekea Uchina zikiendelea, ndege moja ya Vietnam imeripoti kuwa imeona kitu kinachofanana na mlango wa ndege kwenye ufuo wa bahari ya Kusini mwa Uchina kwenye mwambao wa taifa hilo.
Hata hivyo hakuna thibitisho kuwa mlango huo ni wa ndege iliyopotea ya Malaysia, iliyokuwa na abiria mia mbili na thelathini na tisa.
Uchunguzi kuhusiana na kilichosababisha kupotea kwa ndege hiyo mapema siku ya Jumamosi, inawalenga abiria wawili wanaodaiwa kuwemo ndani ya ndege hiyo, waliotumia paspoti iliyoibiwa.
Stakabadhi hizo mbili za kusafiria kutoka Italia na nyingine Australia inaaminika kuibwa nchini Thailand.
Idara ya polisi ya Kimataifa, Interpol, inasema kuwa ni mapema mno kuhusisha pasi zilizoibwa na kutoweka kwa ndege hiyo.
Na huku kushughuli za kuisaka ndege hiyo zikiendelea, Msemaji wa shirika la ndege la Malysia amewaambia jamaa ya watu waliokuwemo katika ndege hiyo, kujiandaa kwa taarifa mbaya.
Maafisa wa Idara ya usafiri wa ndege wa Malaysia
Amesema kufikia sasa hakuna mawasiliano yoyote na ndege hiyo masaa 30 sasa tangu itoweke.
Wakuu wa Malysia wanasema jumla ya meli 30 na ndege 44 kutoka mataifa tisa tofauti duniani, yamejiunga katika shughuli za kuitafuta ndege hiyo.
Kamanda William Marks wa kikosi cha saba cha jeshi la wanamaji la Marekani, ametuma ndege aina ya USS Pinckney kusaidia katika usakaji huo.
''Jambo la kwanza kufanywa ni kukadiria mahala na kwa sasa tunalenga mawasiliano ya mwisho kutoka kwa ndege hiyo kabla ya kutoweka na mawasiliano ya rada. Kutoka hapo tunahesabu mwendo kasi ya upepo na mawimbi. Kutoka hapo tunagawanya na eneo na tunatafuta kutumia kila kifaa tuliyonayo- na hiyo siyo tu kutumia vifaa kutoka Marekani lakini pia kutumia meli na anga kutoka mataifa mengine ya dunia." Alisema kamanda huyo.
Ameonya kuwa shughuli hiyo ya kutafuta ndege hiyo inakumbwa na changamoto nyingi.

 

Wahamiaji haramu 40 wazama Yemen

Maafisa wa serikali nchini Yemen wamesema kuwa zaidi ya wahamiaji arubaini wa Kiafrika wamezama baharini, baada ya mashua walimokuwa wakisafiria kuzama, katika pwani ya kusini mwa nchi hiyo.
Manuwari ya jeshi la Yemen ambalo lilikuwa katika eneo hilo, imefanikiwa kuwaokoa wahamiaji wengine wapatao thelathini.
Wizara ya ulinzi nchini Yemen imesema kuwa mashua hiyo iliyokuwa ikisafirisha wahamiaji haramu, ilizama katika mkoa wa Kusini wa Shabwa, eneo ambako maelfu ya wahamiaji wa Kiafrika huwasili kila mwaka.
Manuwari ya kijeshi ikishika doria katika eneo la Guba
Kwa mujibu wa shirika la Kimataifa la Uhamiaji la IOM, wengi wa wakimbizi wanaojaribu kuvuka guba la Eden, wanatoka Somalia na Ethiopia.
Shirika hilo limesema kuwa wahamiaji hao hufanya safari ndefu na hatari ili kukwepa umasikini, unyanyazaji au vita katika mataifa yao.
Baada ya kuwasili Yemen, wengi wao hutarajia kupata kazi nchini Saudi Arabia na mataifa ya Guba, lakini mamia ya wahamiaji wa Kiafrika hufa kila mwaka wakijaribu kuvuka eneo hilo la Guba wakitafuta maisha bora katika mataifa ya ngambo.