Monday 10 March 2014

Profesa Ibrahim Lipumba aifunda Chadema Dar

 

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetakiwa kuweka kando tofauti za kisiasa na kuunganisha nguvu zao, hasa katika kipindi hiki ambacho taifa lipo katika mchakato wa uundaji wa Katiba Mpya.
Wito huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba alipokuwa akifungua mkutano wa baraza kuu la chama hicho.
Alisema kuwa chama hicho chenye wabunge wengi kinapaswa kutafakari na kuweka kando itikadi za vyama na kuangalia mustakabali wa nchi katika kipindi muhimu.
“Ningependa kuwashauri Chadema kama chama chenye wawakiishi wengi bungeni kinapaswa kuweka kando tofauti za kisiasa na kuunganisha nguvu katika kwa kuangalia masilahi na mustakabali wa taifa,” alisema
“Licha ya changamoto tulizonazo hakuna sababu ya kukata tamaa mapema kiasi hiki, tunapaswa kuondoa tofauti zetu za kisiasa a.”
Kauli hiyo ya Lipumba inakuja kutokana na vuguvugu la mgogoro ulioibuka hivi karibuni ndani ya Chadema ambao ulisababisha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe kuvuliwa nafasi zake zote za uongozi.
Uamuzi huo pia ulimkumba aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho Dk Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

 

No comments:

Post a Comment