Monday 3 March 2014

MADEREVA WA MALORI ZAIDI YA 300 WAGOMA KUENDELEA NA SAFARI KATIKA BARABARA KUU ITOKAYO DODOMA HADI MWANZA BAADA YA MWENZAO KUVAMIWA

 

Madereva wa malori zaidi ya mia tatu wamegoma kuendelea na safari katika barabara kuu itokayo Dodoma hadi Mwanza baada ya dereva mwezao aliyekuwa akiendesha lori kuvamiwa na majambazi katika eneo la kisaki manispaa ya Singida.


Wakiongea na ITV /Radio one madereva ambao wamekutwa katika eneo hilo wameomba jeshi la polisi kufanya doria mara kwa mara eneo hilo kwani kumekuwa na matuki yanayo jirudia ya utekeji wa magari kwa kuweka mawe makubwa barabarani na kuwajeruhi madereva jambo ambalo lina tishia amani kwa watumiaji wa barabara.

Madereva wa malori baada ya kufunga barabara naibu waziri wa Afrika mashariki Dr. Abdulla Abdulla alikumbwa na adha hiyo na kusema ni haki ya kikatiba kwa madereva kugoma kwa kudai haki zao, kutokana na hali hiyo amewahaidi madereva kupeleka kilio chao katika mamlaka husika ili kuweza kutatua tatizo lao na kukomesha vitendo vya uvamizi wa magari katika eneo hilo .

Kwa upande wake kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida SACP Geofrey Kamwela amesema madereva waliamua kusimama barabarani bila sababu yeyote kwa muda wa zaidi ya masaa matatu na kusababisha foleni kubwa ambapo kwamujibu wa sheria za usalama barabarani walikuwa wamefanya kosa ,lakini baada ya viongozi kufika na kuwasikiliza waliamua kuendelea na safari.

Naye dereva wa lori bwana Agustino Mbawala aliye tekwa, akiwa amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Singida akiongea kwa shida huku akiwa na maumivu makali amesema aliona mawe makubwa barabarani na kuamua kusimama na kukimbia lakini wali mvamia na kumpiga hatimaye kumpora fedha na simu 

No comments:

Post a Comment