Ukraine yajizatiti kijeshi
Ukraine imeagiza kuimarisha vikosi vyake katika kukabiliana na Urusi ambayo inaimarisha jeshi lake katika jimbo la Ukraine la Crimea.
Rais wa Marekani Barack Obama ameeleza usambazaji wa majeshi ya Urusi katika jimbo hilo ni "kuingilia uhuru wa Ukraine".
Waziri mkuu mpya wa jimbo la Crimea lenye mamlaka ya kujiamulia mambo yake lenyewe, Sergiy Aksyonov, mwenye mwelekeo wa kuipendelea Urusi, amesema amemwomba Bwana Putin ili kuhakikisha usalama wa eneo hilo.
Hata hivyo serikali ya mpito ya Ukraine haimtambui Bwana Aksyonov na serikali yake ya Crimea.
No comments:
Post a Comment