Miyeyusho ayayushwa
Dar es Salaam. Pambano la bondia Francis Miyeyusho na Ronald
Pontillas wa Ufilipino lililokuwa lifanyike leo limeahirishwa hadi
Aprili 12, kutokana na sababu ambazo ziko juu ya uwezo wa waandaaji.
Katibu Mkuu wa Chama cha Ngumi za Kulipwa Tanzania
(PST), Anthony Lutha, alisema pambano la Miyeyusho limeahirishwa
kutokana na sababu ambazo ziko juu ya uwezo wao.
Promota wa pambano hilo, Mussa Kova alisema,
pambano la Miyeyusho na Pontillas limeahirishwa baada ya kocha wa
bondia huyo kupewa taarifa tofauti kutoka hapa nchini.
“Pontillas aliambiwa pambano halitakuwepo na
kiongozi wa ngumi (alimtaja jina) na alimwambia kuwa Miyeyusho ana
pambano Aprili 26, hivyo hawezi kucheza Aprili 5 na kweli walipoangalia
kwenye mtandao boxrec wakaliona hilo pambano hivyo wakaghairi kuja,”
alisema Kova.
Alisema pambano hilo limesogezwa mbele hadi
Jumamosi ijayo ambapo sasa Miyeyusho atapigana na bondia mwingine wa
Ufilipino, Angelito Merin.
No comments:
Post a Comment