Tuesday 4 March 2014

Kirusi bwete chazinduka

Taarifa ya kirusi aina ya Pithovirus sibericum ambacho kimekuwa bwete kwa miaka zaidi ya 30,000 hadi kilipopelekwa tena kwenye mabara nchini Ufaransa imeendelea kuwa taarifa kuu.

kirusi cha Pithovirus sibericum 

Kirusi hicho cha kale kimerejesha uhai wake baada ya kukaa bwete kwa miaka zaidi ya elfu 30,000 , walieleza wanasayansi .
Kilipatikana kikiwa kimezama kwenye utando wa barafu katika eneo la Siberia, lakini baada ya kuzinduliwa kikawa tena na uwezo wa kusababisha maambukizi .
Wanasayansi wa Ufaransa wanasema hata hivyo kirusi hicho si hatari kwa maisha ya binadamu na wanyama , lakini hii inaonyesha kuwa virusi wengine wanaweza kuzinduka hata baada ya kuwa bwete kwa muda mrefu.
Taarifa ya utafiti huo ilichapishwa katika kituo cha kitaifa cha sayansi nchini Ufaransa (PNAS).
Professor Jean-Michel Claverie, wa kituo cha utafiti (CNRS) katika chuo kikuu cha Aix-Marseille nchini France, alisema: " Hii ni mara ya kwanza tumeona kirusi ambacho bado kina maambukizi baada ya kipindi kirefu kama hiki.
Kirusi hiki ambacho ni kikubwa kinaweza kuonekana kwa macho tofauti na virusi vingine vinavyoonekana tu kwa kutumia microscope, na kilipatikana kikiwa kimezikwa mita 30 chini kwenye barafu iliyoganda.
Wanasayansi wanasema kubainika kwa kirusi cha Pithovirus sibericum kunaonyesha hatari kwamba virusi vya maambukizi vinavyodhaniwa kuwa vimekufa vinaweza kuibuka tena baada ya miaka mingi na kusababisha maambukizi kutokana na shughuli za binadamu.

 

No comments:

Post a Comment