Tuesday 4 March 2014

Mamilioni ya Airtel ‘Mimi ni Bingwa’ yaenda Bukoba

Dar es Salaam. Promosheni ya ‘Mimi ni Bingwa’ imemtangaza Rashid Jacob Kagombola, mkazi wa Bukoba mkoani Kagera kuwa mshindi wa Sh50 milioni katika droo kubwa ya bahati nasibu iliyochezeshwa na Kampuni ya Mawasiliano ya Airtel Tanzania mwishoni mwa wiki Dar es Salaam.
Akimtangaza mshindi huyo, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema: “Leo hii tumefikia mwisho wa Promosheni yetu ya ‘Mimi ni Bingwa’ ambayo imewanufaisha Watanzania wengi. Limekuwa ni zoezi la mafanikio likishirikisha idadi kubwa ya wateja waliojiunga katika promosheni hii iliyokuwa na vipengele tofauti.”
“Ningependa kuwashukuru wateja wetu kwa kushiriki promosheni hii tangu ilipoanza mwishoni mwa Novemba mwaka jana. Airtel bado ina mipango mingine mingi inakuja, tukilenga kuendelea kurudisha kile tulichonacho kwa wateja wetu na kuisaidia jamii inayotuzunguka kukuza viwango vyao vya maisha.”
Alisisitiza kuwa mbali na zawadi hiyo ya Sh50 milioni kutolewa, washindi wa awamu ya pili na ya tatu wa safari iliyogharimiwa kila kitu ya kwenda kuangalia mechi ya Klabu ya Manchester United wataondoka nchini mwezi huu pale klabu hiyo itakapocheza tena kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Naye mshindi wa Promosheni hiyo, Rashid Jacob, akizungumza kwa njia ya simu kutoka Bukoba, aliipongeza Airtel Tanzania kwa kuanzisha promosheni hiyo ambayo amedai imesaidia kubadili maisha ya wateja wake na kuwa na mabadiliko chanya katika jamii na nchi nzima kwa jumla.
“Hii ni miujiza inayotokea maishani mwangu. Siwezi kuamini nami nimeingia katika orodha ya mamilionea Tanzania. Kwangu ni kama kutimia kwa ndoto kwa sababu ya Airtel. Naishukuru Airtel Tanzania. Hakika hizi milioni 50 zitabadilisha maisha yangu kabisa na zawadi nitakayoipatia Airtel ni kubaki kuwa mteja wao mwaminifu wakati wote,” alisema Kagombola.
Wakati wa promosheni hiyo, washiriki wawili wa Mimi ni Bingwa wa kila siku walizawadiwa Sh2 milioni , wawili wa Sh5 milioni katika droo za kila wiki na mmoja tiketi mbili za safari iliyogharimiwa kila kitu kwenda jiji la Manchester.

 

No comments:

Post a Comment