Tuesday 4 March 2014

Keqiang asema mageuzi ni sharti China 


Li Keqiang akihutubia bunge la Uchina.
Waziri mkuu wa China, Li Keqiang, ameuambia mkutano wa kila mwaka, wa bunge la taifa hilo mjini Beijing, kwamba maendeleo ya kiuchumi yanasalia kuwa jukumu kubwa zaidi la serikali, lakini marekebisho ya kimsingi ni sharti yatekelezwa japo ni machungu.
Bwana Li amewaambia maelfu ya wajumbe katika bunge la taifa hilo, Great Hall of the People, kwamba shabaha ya kila mwaka ya ukuaji wa kiuchumi itasalia kuwa asilimia saba nukta tano.
Akizungumzia tatizo la uchafuzi, amesema kuwa moshi mkubwa unaondelea kutanda katika miji mikubwa ya China, ni onyo la kiasili dhidi ya maendeleo yasiokuwa na mpango.
Waziri huyo mkuu wa China kadhalika ametangaza marufuku dhidi ya majengo mapya ya serikali kama sehemu ya kile alichokitaja kuwa mapambano bila huruma dhidi ya ufisadi.

 

No comments:

Post a Comment