Wednesday 26 February 2014

Asasi za DRC zataka el Bashir ashikwe.

Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, yamesema kuwa Serikali ya nchi hiyo itachukuliwa kuwa dhaifu iwapo hamkamati Rais wa Sudan, Omar el Bashir.

 

Rais wa Sudan Omar el bashir

Mashirika yapatayo 90 yalitoa wito Serikali ya DRC imkamate el Bashir ambaye alikuwa mjini Kinshasa kushiriki katika vikao vya muungano wa COMESA.
Mmoja wa waandalizi wa maandamano ya kushinikiza Serikali imkamate kiongozi huyo wa Khartoum, Bwana Andre Kito Masimango, amesema:
"kuna barua ambayo inasema kuwa mahali po pote ambapo El Bashiri anapatikana anapaswa kukamatwa na kupelekwa kwenye mahakama ya kimataifa."
Mkerektwa huyo wa haki za kibinadamu anasema kuwa Rais El Bashir anapaswa kukamatwa kwa heshina ya waathirika wa dhuluma inayodaiwa kufanywa nchini Sudan na hata DRC yenyewe.
Watu kadhaa ambao wametoa maoni kwenye mtandao wa BBC wamesema kuwa lilikuwa kosa kwa Serikali ya DRC kumkaribisha Rais El Bashar kwa mkutano wa COMESA huku ikijua kuwa anatafutwa.
Hata hivyo kuna wale wanaosema kuwa msimamo wa Umoja wa Afrika (AU) ambao unasema kiongozi anayetawala hapaswi kukamatwa unapaswa kuzingatiwa ili El Bashir asikamatwe ugenini DRC.

 

No comments:

Post a Comment