Singapore mji ghali zaidi duniani
Singapore umetajwa kuwa mji ghali zaidi duniani kuishi kwa mwaka 2014 na kuipiku miji mingine 131 kwa mujibu wa taarifa ya Economist Intelligence Unit (EIU).
Singapore imechukua nafasi ya mji wa Tokyo, amao ulikuwa unaongoza kwa ughali wa maisha mwaka 2013.
Miji mingine mitano inayoongoza kwa gharama kubwa za maisha duniani ni pamoja na Paris, Oslo, Zurich na Sydney, huku Tokyo ukiporomoka hadi nafasi ya sita.
Mji wa New York unatumiwa kama kigezo cha utafiti wa shirika la EIU kuhusu gharama za maisha katika miji mbalimbali duniani. Wanaangalia zaidi ya bei binafsi 400.
No comments:
Post a Comment