Monday 19 May 2014

5 wauawa katika mlipuko Nigeria

Bomu lililolipuka katika mji wa Kano kaskazini mwa Nigeria limewaua watu 5 na kuwajeruhi wengine wengi.
Shambulio hilo limefanywa katika eneo linaloaminiwa kuwa na waumini wengi zaidi wa dini ya kikristu, ambao wamekuwa wakilengwa mara nyingi na wapiganaji wa Boko Haram.
Mwandishi wa BBC mjini Abuja Will Ross anasema kuwa eneo hilo lililolengwa linajulikana kama Sabon Gari. Watu wengi walikuwa kwenye migahawa ya vileo na kwenye barabara. Amesema kuwa kilichosalia kwenye gari lililokuwa na bomu hiyo ni injini pekee.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja mji wa Kano umepumzika kutokana na mashambulio, hasa kwasababu ya oparesheni kali iliyofanywa na maafisa wa usalama kuwasaka wanamgambo hao wa Boko Haram.


Mlipuko wa bomu Nigeria 

Mashambulio ya awali

Mnamo mwezi Machi mwaka uliopita kituo cha basi kilishambuliwa kwa bomu na awali mwaka wa 2012, Boko Haram walifanya shambulio baya zaidi lililowaua zaidi ya watu 150 katika msururu wa milipuko.
Kundi hilo bado linawazuilia wasichana zaidi ya 200 wa shule, lililowateka kutoka kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa Nigeria mwezi mmoja uliopita.
Nchi kadhaa zikiwemo Uingereza, Ufaransa na Marekani wameahidi kutuma wanajeshi kusaidia kuwakomboa wasichana hao.
Nao viongozi wa Afrika wanaokutana mjini Paris wametangaza 'vita' dhidi ya Boko Haram na kuahidi kushirikiana ki-intelijensia na kijeshi, kupambana na Boko Haram.


 

Wednesday 7 May 2014

Rais Kikwete afungua mkutano wa Majaji Wanawake Arusha

      
mpya 
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Katiba na Sheria Dkt.Asha Rose Migiro,Jaji Mkuu Mohamed Othman Chande,pamoja na Rais wa Chama Cha Kimataifa cha Majaji Wanawake wakiimba wimbo wa taifa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 12 wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Arusha AICC.Mkutano huo ulifunguliwa na Rais Kikwete.22bh nhnmhjm
Baadhi ya majaji wanawake wanaoshiriki Mkutano wa 12 wa Chama Cha Kimataifa cha Majaji  wanawake unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano mjini Arusha

TANKI LA MAFUTA LALIPUKA NA KUSABABISHA ADHA KUBWA KWA WASAFIRI MAENEO YA SHELUI SINGIDA

       
7
Baadhi ya wananchi wakipiga picha wakati tanki la mafuta la kampuni ya B. Clarke Haulege Construction, Tanki hilo ni mali ya Bw. Bundala Kapela wa Igunga ni namba T634 BCZ lenye vyumba vinne na uwezo wa kubeba lita 40.000 za mafuta ya Petroli lililipuka majira ya Saa 11:00 katika barabara kuu ya Dodoma Mwanza eneo la Shelui mkoani Singida wakati breki za tanki hilo upande wa kushoto zilipojam na kusababisha moto, Jambo lililomfanya dereva wa roli lenye namba za usajiri T 164 CGF aina ya Scania lililokuwa likivuta tanki hilo kusimamisha na kukata haraka tanki hilo huku akiondoa haraka injini ili kuepusha madhara zaidi ambayo yangeweza kutokea, Katika tukio hilo lililosababisha usumbufu mkubwa kwa abiria  na msururu wa magari kushindwa kupita  kutokana na moto mkubwa uliochanganyika na moshi kutishia usalama wa watumiaji wengine, hata hivyo  baada ya moto kupungua kiasi askari wa usalama barabarani waliamuru magari yaanze kupitia pembeni mwa barabara hiyo ili kuendelea na safari, Hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo, Angalia matukio zaidi ya picha hapo chini. (PICHA NA FULLSHANGWE) 
 5 4 111
Msururu wa magari ukiwa mkubwa katika eneo hilo baada ya kushindwa kupita kutokana na moto mkubwa uliokuwa ukiwaka. 10
Wananchi na wasafiri mbalimbali wakitoka kuangalia tukio hilo. 8
Askari wa usalama barabarani akihakikisha mambo yanakwenda sawana usalama unaimarishwa katika eneo hilo.

Airtel yazindua duka la kisasa Mlimani City

      
pic 1a
Afisa mtendaji Mkuu Airtel Africa Christophe Soulet akikata utepe kuzindua
duka la  Airtel  lililopo mlimani city  jijini Dar es Saalam.wakishuhidia,
wapili ni Andre Beyers Afisa mkuu wa masoko Airtel Afrika akiwa na meneja
wa duka Wahida Saleh na Sunil Colaso Mkurugenzi Mkuu Airtel Tanzania
pic 1b
Afisa mtendaji Mkuu Airtel Africa Christophe Soulet akikata utepe kuzindua
duka la  Airtel  lililopo mlimani city  jijini Dar es Saalam.wakishuhidia,
wapili ni Andre Beyers Afisa mkuu wa masoko Airtel Afrika akiwa na meneja
wa duka Wahida Saleh na Adriana Lyamba Mkurugenzi wa kitengo cha huduma kwa
wateja Airtel Tanzaania
pic 5b
Afisa mtendaji Mkuu Airtel Africa Christophe Soulet na  Afisa mkuu wa
masoko Airtel Afrika Andre Beyers wakiwa katika picha ya pmaoja na
wafanyakazi wa Airtel katika duka la mlimani City mara baada ya uzinduzi wa
duka hilo baada ya kufanyiwa matengenezo na kuwa la kisasa zaidi
pict 5
pic 10