Monday 24 March 2014

Zanzibar yashauriwa kurekebisha Katiba

 

 Alisema wakati Katiba ya Zanzibar ikieleza hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sura ya 1 inaelezaa kuwa Tanzania ni nchi moja na eneo lake la mipaka ni kuanzia Tanzania Bara hadi Visiwani

Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeshauriwa kufanya marekebisho ya Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu Mwaka 2015 ili kuondoa vifungu vinavyogongana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ushauri huo umetolewa na mwanasiasa mkongwe wa Zanzibar, Ali Hassan Khamis wakati akiwasilisha mada juu ya hali ya kisiasa na mchakato wa Katiba ya Muungano katika kongamano lililoandaliwa na Jumuiya za CCM, lililofanyika kwenye Ukumbi wa Tawi la Kiembesamaki Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Alisema migongano inayojitokeza katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imetokana na marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 iliyogongana na Katiba ya Muungano na kusababisha mjadala mkubwa katika mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea.
Alisema marekebisho hayo ya Katiba ya Zanzibar yameongeza migongano hasa sura ya 1(1) inayoeleza kuwa Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyozungukwa na bahari yake, ambayo kabla ya Muungano wa Tangayika na Zanzibar ilikuwa ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Alisema wakati Katiba ya Zanzibar ikieleza hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sura ya 1 inaelezaa kuwa Tanzania ni nchi moja na eneo lake la mipaka ni kuanzia Tanzania Bara hadi Visiwani.
Aliwaeleza washiriki hao kuwa kifungu cha 2(a) cha Katiba ya Zanzibar kimempa uwezo Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar katika mikoa na wilaya kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
Alisema marekebisho hayo ya 10 yamechangia kwa kiwango kikubwa kuibua migogoro ndani ya Muungano na kutaka Katiba ya Zanzibar iandikwe upya na wananchi wapewe nafasi ya kuijadili na kuamua.
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Vilevile alieleza katika marekebisho hayo ya 10 kuna vitu viliondolewa lakini havikuwa na ulazima kama wakuu wa mikoa kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi (BLW), wakati ni watendaji wakuu wa shughuli za Serikali katika kuwahudumia wananchi kwenye maeneo yao.
“Wakati umefika katiba yetu ya Zanzibar iangaliwe upya iendane na Katiba ya Jamhuri ya Muungano vinginevyo tutaendelea kuendeleza migogoro na kuathiri msingi mzima wa Muungano na Mapinduzi ya Zanzibar,” alisema Ali Hassan Mkuu wa Wilaya ya Kati wa zamani visiwani humo.
Akifafanua zaidi alisema hata muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), una kasoro Zanzibar kutokana na sera ya CCM kuwa ni moja kati ya Zanzibar na Tanzania Bara lakini mfumo huo wa Serikali umezingatiwa upande marekebisho hayo ya kati mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Chama chetu ni kimoja, ni sehemu gani sera yetu imesema CCM ikishinda itaunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa wakati hilo Tanzania Bara halipo,” alisema.

 

No comments:

Post a Comment