Saturday, 12 April 2014
Raia wa Guinea Bissau kuchagua rais mpya
Uchaguzi wa urais na maeneo bunge unafanyika katika taifa dogo la afrika magharibi Guinea Bissau.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Antonio Indjai aliikabidhi mamlaka serikali ya raia mnamo mwaka 2012 iliopewa wajibu wa kuandaa Uchaguzi huo.
Indjai alifunguliwa mashtaka nchini marekani kwa madai ya kufanya biashara ya mihadarati pamoja na kuwauzia silaha waasi wa Colombia.Wagombea 13 wanawania wadhfa wa urais.
Iwapo mmoja wao hatashinda kwa wingi wa kura basi uchaguzi huo utaenda kwa awamu ya pili mnamo mwezi May.
Boko Haram ladaiwa kuwaua watu laki moja
Sasa imebainika kuwa wanamgambo wa kiislamu kazkazini
mwa Nigeria wamewaua zaidi ya watu laki moja na arubaini na tano katika
misururu ya mashambulizi juma lililopita.
Sineta wa jimbo la kazkazini mashariki la Borno
Ahmed Zannah ameiambia BBC kwamba mauaji hayo yalifanyika katika maeneo
matatu tofauti yaliopo mashambani.Amesema kuwa taassi moja ya kutoa mafunzo ya elimu ndio iliokuwa ya kwanza kulengwa ambapo wanamgambo hao waliwaua walimu watano kabla ya kuwatekanyara wake zao kadhaa.
Wapiganaji hao wanaoshukiwa kutoka katika kundi la wanamgambo wa Boko haram baadaye walivamia vijiji viwili katika eneo la mashambani karibu na mpaka na Cameroon.
Iran haitabadili balozi wake katika UN
Makamo wa waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Iran
amesema nchi yake haifikirii kumteua mtu mwengine kuiwakilisha nchi
katika Umoja wa Mataifa.
Taarifa iliyotolewa na Abbas Araqchi imesema
Iran itatumia sheria kupinga uamuzi wa Marekani wa kumkatalia visa Hamid
Abutalebi kuingia Marekani, ili kuwa mwakilishi mpya wa Iran katika
Umoja wa Mataifa mjini New York.Bwana Abutalebi amehusishwa na kundi lilovamia ubalozi wa Marekani mjini Teheran mwaka wa 1979, na nchini Marekani baadhi ya wanasiasa wamepinga vikali uteuzi wa mwanabalozi huyo.
Marekani haikuwahi kumkatalia visa mwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wenye makao yake makuu mjini New York.
Wednesday, 9 April 2014
Miyeyusho ayayushwa
Dar es Salaam. Pambano la bondia Francis Miyeyusho na Ronald
Pontillas wa Ufilipino lililokuwa lifanyike leo limeahirishwa hadi
Aprili 12, kutokana na sababu ambazo ziko juu ya uwezo wa waandaaji.
Katibu Mkuu wa Chama cha Ngumi za Kulipwa Tanzania
(PST), Anthony Lutha, alisema pambano la Miyeyusho limeahirishwa
kutokana na sababu ambazo ziko juu ya uwezo wao.
Promota wa pambano hilo, Mussa Kova alisema,
pambano la Miyeyusho na Pontillas limeahirishwa baada ya kocha wa
bondia huyo kupewa taarifa tofauti kutoka hapa nchini.
“Pontillas aliambiwa pambano halitakuwepo na
kiongozi wa ngumi (alimtaja jina) na alimwambia kuwa Miyeyusho ana
pambano Aprili 26, hivyo hawezi kucheza Aprili 5 na kweli walipoangalia
kwenye mtandao boxrec wakaliona hilo pambano hivyo wakaghairi kuja,”
alisema Kova.
Alisema pambano hilo limesogezwa mbele hadi
Jumamosi ijayo ambapo sasa Miyeyusho atapigana na bondia mwingine wa
Ufilipino, Angelito Merin.
Tuzo za Kili zichague muziki bora siyo maarufu
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Banana Zorro (kushoto) na Ray C
(kulia) baada ya kutwaa tuzo za Kili Music Awards mwanzoni mwanzoni mwa
mwaka 2007
Tuzo maarufu za muziki nchini ‘Kilimanjaro Music Award’
zinazoratibiwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwa kushirikiana na
kampuni ya bia (TBL) zinatarajiwa kufanyika Mei 3 kwenye Uukumbi wa
Mlimani City, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Basata na TBL, tuzo za mwaka huu
zimefanyiwa mabadiliko katika mchakato wa kupata wateule watakaoingia
katika vipengele mbalimbali.
Mabadiliko hayo ni kwamba wananchi wa kawaida
walipewa fursa ya kupendekeza wanamuziki, nyimbo, vikundi,
watayarishaji, video na vitu vingine wanavyodhani vinastahili kuwapo
katika mchakato wa kuwapata wateule wa tuzo za muziki Tanzania tangu
mwezi Februari.
Wananchi hao wa kawaida tangu Februari walipewa
nafasi ya kutoa mapendekezo yao kwa kutumia mfumo wa SMS, na mtandao
yaani tovuti na barua pepe.
Baada ya wananchi kutoa mapendekezo hayo, Basata,
TBL na jopo la wataalamu wa tuzo hizo waliyachuja majina katika kila
kipengele na kubakizsha majina matano ambapo hivi sasa wameyarudisha kwa
wananchi kwa ajili kupigia kura washindi wa kila kipengele.
Washindi watakaopata kura nyingi baada ya
kuchaguliwa na wananchi katika kila kipengele ndiyo watakaopewa tuzo zao
katika hafla itakayofanyika Mei 3 kwenye Uukumbi wa Mlimani City, Dar
es Salaam.
Siku zote sisi tunaamini kwamba mabadiliko ni kitu
cha muhimu katika maisha ya mwanadamu au katika shughuli tunazozifanya,
lakini mabadiliko yasiwe katika kukwepa majukumu.
Tunasema hivyo kwa sababu tunaona utaratibu huu
mpya umesahau kufikiria jambo moja kubwa la msingi kwa hizi ni tuzo za
kutafuta muziki bora na siyo tuzo za kutafuta muziki maarufu.
Ni wazi kuwa siku zote wananchi wa kawaida huwa
wanasikiliza nyimbo zinazopigwa kwenye vituo vya redio na televisheni
mara kwa mara na wengi hawana utaalamu wa muziki.
Nyimbo nyingi zinazopigwa kwenye radio au
kuonyeshwa kwenye televisheni ni nyimbo maarufu na siyo lazima ziwe ni
nyimbo bora kwa sababu siku hizi wanamuziki hutoa fedha ili nyimbo zao
zipigwe kwenye radio na kuonyeshwa kwenye televisheni.
Ndiyo maana tunasema mabadiliko ya kukimbia wajibu
siyo mazuri kwani suala hili la kuchagua muziki bora linahitaji
utaalamu kwa sababu kuna nyimbo nyingine ni bora, lakini hazipati nafasi
ya kupigwa kwenye radio au kuonyeshwa kwenye televisheni kwa sababu
wanamuziki wenye nyimbo hizo hawatoi fedha.
Hii inamaanisha katika tuzo za mwaka huu washindi
watakaopatikana watakuwa ni wanamuziki, nyimbo au vikundi vinavyopata
nafasi ya kupigwa kwenye readio au kuonyeshwa kwenye televisheni.
Yala: Shule iliyogeuka ‘kisiwa’
Sehemu ya Shule ya msingi Yala ikiwa imejaa maji.
Yala ni shule ya msingi iliyopo katika Kijiji cha Yala Kata ya
Luhanga Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya na ipo umbali wa kilomita 40
kutoka Barabara Kuu ya Mbeya-Iringa, ili kufika shuleni hapo inakulazimu
kutembea kwa mguu kutokana na magari na pikipiki kushindwa kufika.
Shule hiyo ina muda wa zaidi ya miaka 20 tangu
kuanzishwa kwake, imezungukwa na mito minne ambayo imekuwa ikijaa maji
kipindi cha masika na kusababisha kukatika kwa mawasiliano na ukosefu wa
huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu.
Kutokana na tatizo hilo la mito kujaa maji shule
hiyo imekuwa ikigeuka kuwa kisiwa na kusababisha wanafunzi na walimu
kushindwa kufika shuleni kwani mito hiyo haina madaraja ya kuwawezesha
kupita na kufika shuleni hapo.
Wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo wamekuwa
wakitoka katika Vitongoji vya Mwashikamile, Ruaha, Waninyika, Mtakuja,
Yala na Lusaka na wote hushindwa kuvuka mito hiyo na kufika shuleni huku
walimu pia wakikumbwa na adha hiyo kutokana na shule hiyo kutokuwa na
nyumba za kuishi Walimu.
Jairos Mpale ni Mwenyekiti wa serikali ndogo ya
maendeleo ya Mwashikamile katika Kijiji cha Yala anasema kuwa tatizo
hilo limekuwa kubwa zaidi kwa mwaka huu ukilinganisha na miaka
mingine.Hii ni kutokana na mvua zinanyesha kwa wingi na wanafunzi
wamekaa nyumbani muda mrefu bila kwenda shule.
“Watoto wetu wameshindwa kwenda shuleni hapo tangu
shule zote zilipofunguliwa Januari, kutokana na mito kujaa maji na kuna
mamba wengi na viboko hivyo ni vigumu kuvuka kwenda katika Shule ya
Yala na watoto wetu wamekosa masomo na hatujui ni lini wataanza masomo,”
anasema.
Naye Mtendaji wa kijiji cha Yala shule ilipo,
Isaac Ngera anasema kuwa tatizo hilo huwa linajitokeza mara kwa mara
katika msimu wa mvua na mito hiyo imekuwa ikijaa na kusababisha wananchi
kushindwa kupata huduma mbalimbali za kijamii ikiwa ni pamoja elimu,
afya na majisafi na salama.
Aliitaja mito iliyojaa maji kuwa ni Itambo na
lwashimala na vitongoji vilivyopo ng`ambo ya mito hiyo ni Ruaha na
Woninyika kwa upande wa Kusini kuna vitongoji vya Mtakuja na Lusaka
ambavyo vipo ng`ambo ya Mto Itambo na yote imejaa maji hakuna
mawasiliano na upande wa pili.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Stephano Mlewa anasema
kuwa kwa sasa hali ni mbaya katika shule hiyo kwani hakuna mwanafunzi
anayefika shuleni hapo.
“Siyo kwa wanafunzi pekee hata kwa Walimu ni
tatizo kubwa kwani wanaishi katika kitongoji ambacho kipo mbali na shule
hiyo na inawalazimu wavuke mito miwili ambayo kwa sasa imejaa maji
hivyo hakuna masomo,” anasema.
Anasema kuwa shule hiyo pia ina changamoto ya
madarasa kwani ina jumla ya vyumba vya madarasa vinne pekee na wanafunzi
wapo kuanzia darasa la kwanza hadi la saba hivyo husoma kwa kupokezana.
Ofisa Elimu Wilaya ya Mbarali, Henerico Batinoluho
anasema kuwa shule ina wanafunzi zaidi ya 400 na kwamba mwaka huu shule
ilifunguliwa Januari 6, lakini wamefanikiwa kuingia darasani katika
kipindi cha wiki moja pekee.
WHO: uvumi wa maambukizi ya Ebola ukome
Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema kuwa kuzuka
kwa Homa ya Ebola Magharibi mwa Afrika ni mojawapo ya changamoto kubwa
zaidi ambazo limewahi kukabiliana nayo.
Shirika hilo limesema kuwa italichukua hadi
miezi minne kuthibiti ugonjwa huo. Wakati huohuo shirika la kutoa
misaada ya matibabu ya bure, Medicins Sans Frontieres, limesema kuwa
linaendelea kufanya mashauriano na viongozi wa kijamii katika Wilaya
moja Kusini mwa Guinea, ambalo lilisimamisha shughuli zake baada ya
vituo vyake kadhaa kushambuliwa na wakaazi wa eneo hilo.Msemaji wa shirika hilo katika mji mkuu wa Guinea wa Conakry - Sam Taylor - amesema inaeleweka kwamba watu wana uoga mkubwa.
"Sio taharuki, kimsingi huu ni uoga. Na tunaelewa hilo. Ni ugonjwa wa kugovya na pia ni mpya nchini Guinea, na kuna uvumi unaosambaa na pia kuna habari za kuotosha zinazoenea; na tunachohitaji kuona kwa wingi sasa ni watu kwenda kwa jamii mbalimbali kueleza ugonjwa huu, jinsi unavyoenea, na jinsi usivyoenea," alisema Bwana Taylor.
Ugonjwa huo umewaua watu 111 katika nchi za Guinea na Liberia tangu uchipuke mwezi uliopita.
Wednesday, 2 April 2014
Mugabe asusia mkutano kuhusu CAR
Maelfu ya waisilamu wametoroka vita CAR na kukimbilia nchi jirani ya CAR
Viongozi wa Ulaya na Afrika wanatarajiwa kuanza
kujadili mgogoro unaotokota katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, katika
mkutano maalum unaofanyika kando na kongamano la viongozi wa Ulaya mjini
Brussels.
Rais Robert Mugabe amesusia kongamano hilo baada ya Muungano wa Ulaya kukataa kumwondolea marufuku ya muda ya Visa mkewe Grace.Zuma alisema kuwa muda umewadia wa Ulaya kukoma kuwaangalia waafrika kama sio watu.
Muungano wa Ulaya tayari umezindua kikosi cha jeshi lake nchini CAR, na kuelezea mipango yake kutuma wanajeshi 1,000 kuwasaidia wanajeshi wa Afrika na wale wa Ufaransa wanaoshika doria nchini humo.
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa waisilamu 19,000 wanakabiliwa na tisho la kuuawa nchini humo.
Maswala ya Uchumi na Uhamiaji pia yatapewa kipaombele kwenye mkutano huo.
Viongozi 30 wanatarajiwa kuhudhuria kongamano lenyewe wakiwemo marais wa Afrika.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon atahudhuria mkutano kuhusu CAR pamoja na viongozi wa Afrika na wale wa Muungano wa Ulaya.
Ameahidi kufAnya kila awezalo kuhakikisha anaimarisha juhudi za kukabiliana na migogoro ya kimataifa.
Zuma kujieleza kuhusu nyumba yake
Rais Jacob Zuma anatarajiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge la A-Kusini kujieleza kuhusu kashfa ya kufuja pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya kifahari.
Ukarabati huo uligharimu dola million 23 na Bw Zuma ameamrishwa na mkaguzi au mlinzi wa mali ya umma nchini humo alipe baadhi ya pesa hizo .
Zuma alisema Jumatatu kuwa sio sawa kwake kutakiwa alipe sehemu ya pesa zilizotumiwa kwa ukarabati wa nyumba yake kwani sio yeye aliayeamuru ukarabati huo.
Alisema kuwa maafisa wa serikali ndio walioagiza ukarabati huo bila ya kumshauri.
Zuma alizungumza kwa mara ya kwanza Jumatatu tangu kashfa hiyo kujulikana akisema kuwa halipi chochote kwani hakuomba ukarabatai kufanywa.
Subscribe to:
Posts (Atom)