Mnyika atishia kuwataja vigogo
Wakati
huohuo, Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika ametishia
kuwataja kwa majina vigogo wa Serikali na CCM aliosema wako nyuma ya
‘kashfa’ kuhusu mgogoro huo ili waweze kuhojiwa kwa umma iwapo Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo hatajitokeza kufafanua
kauli alizozitoa bungeni kutuhumu IPTL.
Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo (Chadema),
alisema hayo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, akimtuhumu
Waziri Muhongo kwa kudai bungeni Mei 25, 2013 kuwa yeye hakutumwa
wizarani kupekua mafaili ili kufuatilia mlolongo wa kesi za IPTL.
Alisema anachukua hatua hiyo kwa kuzingatia kwamba
madaraka na mamlaka ni ya wananchi... “Serikali inafanya kazi kwa niaba
ya wananchi; hivyo pale Serikali inapochelewa kuchukua hatua kutokana
na udhaifu, uzembe, ufisadi au uongo, ni muhimu wananchi wakashiriki
kutaka uwajibikaji.”
No comments:
Post a Comment