Friday 28 February 2014

Viwanja vya ndege vyadhibitiwa Crimea

Waziri wa mambo ya ndani wa Ukraine amesema majeshi ya Urusi yamekuwa yakiweka vizuizi katika uwanja wa ndege wa Sevastopol uliopo katika jimbo la Crimea.

 

Watu wenye silaha wakilinda doria uwanja wa ndege Simferopol, Crimea, Ukraine

Waziri huyo wa Ukraine, Arsen Avakov ameita uwepo wa majeshi ya Urusi katika jimbo hilo kuwa "uvamizi wa kijeshi".
Watu hao wenye silaha pia wameutwaa uwanja mwingine mkubwa wa ndege wa Simferopol, uliopo pia Crimea Ijumaa asubuhi.
Uhusiano kati ya Urusi na Ukraine umeyumba tangu kuondolewa madarakani kwa Rais wa Ukraine, Viktor Yanokovych, ambaye kwa sasa yuko nchini Urusi.
Uhasama huu umedhihirika zaidi katika jimbo la Crimea, nchini Ukraine, ambalo wakaazi wake wengi ni Warusi.
Siku ya Alhamisi, watu wenye silaha wenye mwelekeo wa Urusi, walivamia ofisi za bunge la Simferopol, na kuliondoa baraza la sasa la mawaziri na kumchagua waziri mkuu mpya.
Bado haijafahamika watu hawa wenye silaha katika mji wa Simferopol waliowasili katika uwanja wa ndege mapema ni kina nani.
Licha ya kuwepo kwao, inasemekana shughuli zinaendelea kama kawaida katika uwanja wa ndege wa Simferopol.
Watu walioshuhudia tukio hilo wameliambia shirika la habari la Ukraine, Interfax, kuwa watu wapatao 50 waliwasili katika uwanja wa ndege wa Simferopol wakiwa wamebeba bendera za jeshi la wanawamaji la Urusi.

 

Kenya: Wajumbe wa ODM wazua vurugu

Vurugu zimezuka katika uchaguzi wa kuwachagua maafisa wapya wa chama kikuu cha upinzani cha ODM nchini Kenya, chake aliyekuwa waziri mkuu wa taifa hilo Raila Odinga.

 

Bwana Odinga anatarajiwa na wengi kuwa atagombea kiti cha urais 2017

 Polisi waliwasili katika ukumbi wa uwanja wa michezo wa kimataifa wa Kasarani viungani mwa jiji la Nairobi kurejesha utulivu baada ya baadhi ya wafuasi wa chama hicho waliodaiwa kuwa walinda usalama kurusha vita pamoja na masanduku ya kupigia kura wakijaribu kuvuruga uchaguzi huo.

Ugomvi ulizuka baada ya kuzuka madai kuwa kulikuwa na orodha ya wajumbe bandia iliyokuwa ikisambazwa pamoja na makaratasi bandia ya kupigia kura. Mbunge maalum Isaac Mwaura ambaye anaishi na ulemavu wa ngozi-Albino-alionekana akisukwasukwa na wajumbe baada ya kuzua zahama kuhusu madai hayo ya udanganyifu katika zoezi hilo la upigaji kura.
Chama cha ODM ndicho chama kikubwa zaidi cha kisiasa nchini Kenya kikiwa na idadi kubwa ya wabunge katika bunge la kitaifa pamoja na Senate. Chama hicho kimemudu mgao mkubwa zaidi wa pesa za kufadhili shughuli za vyama vya kisiasa kutoka kwa serikali ya Kenya.
Kutokana na raslimali za chama hicho uchaguzi wa leo umeonekana kuzua msisimko mkali pamoja na patashika baina ya wanasiasa mashuhuru ambao wanagombania vyeo mbali mbali.
Bwana Odinga ambaye alishindwa na rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliokumbwa na madai ya udanganyifu mwezi Machi mwaka uliopita anatetea kiti chake kama kiongozi wa chama, dalili kwamba huenda akagombea tena kiti cha urais mwaka 2017.
Akizungumza kabla ya kuanza kwa zoezi la upigaji kura Bwana Odinga alizungumzia maswala mbali mbali yanayohusiana na usalama nchini Kenya pamoja na kuiponda serikali ya mpinzani wake Rais Uhuru Kenyatta kwa kushindwa kuleta suluhu ya matatizo ya kiuchumi yanayowakabili wakenya.

 

Shambulizi lawaua 12 Mogadishu

Mshambuliaji wa kujitoa muhanga amejilipua ndani ya gari na kuwauwa watu 12 na kujeruhi wengine wanane mjini Mogadishu Somalia.

 

Mogadishu imeshuhudia mashambulizi ya mara kwa mara hivi karibuni

Mlipuko huo umetokea nje ya makao makuu ya maafisa wa usalama .
Mwandishi wa BBC anasema kuwa waliofariki ni maafisa usalama na wengine raia wa kawaida waliokuwa katika mkahawa karibu na hapo.
Kumekuwa na ongezeko la mashambulizi huku vikosi vya nchi hiyo vikipambana na wanamgambo wa al shaabab.
Kundi la wanamgambo la Al Shabaab limekiri kufanya shambulizi hilo ambalo limetokea chini ya wiki mbili baada ya kundi hilo kushambulia ikulu ya Rais mjini Mogadishu
Msemaji wa kijeshi wa kundi hilo amenukuliwa na shirika la habari la Reuters akisema kuwa huu ndio mwanzo tu wa kundi hilo kushambulia Mogadishu na kwamba operesheni yao itaendelea.
Alisema kuwa shambulio hilo lililenga maafisa wa usalama waliokuwa wameketi katika mkahawa mmoja na kuwaua watu 11 huku 15 wakijeruhiwa.

 

Marekani kuleta umeme Afrika

Wabunge nchini marekani wameidhinisha mpango wa kuleta umeme kwa zaidi ya watu millioni hamsini katika jangwa la Sahara barani Afrika na hivyo basi kutoa fursa kwa mradi huo wa serikali ya Obama kuanza kutekelezwa.

      

Mswada huo uliopitishwa na kamati ya maswala ya kigeni nchini humo unalenga kujenga megawati elfu ishirini barani Afrika ifikiapo mwaka 2020 na kuwafikia watu elfu hamsini ambao wanaishi bila umeme.

Mpango huo ulitangazwa na rais Obama wakati wa ziara yake barani afrika mnamo mwezi juni mwaka jana.
Mswada huo utahitajika kupitishwa na bunge la wawakilishi pamoja na lile la sineti lakini hatua hiyo ya kamati ya maswala ya kigeni ni dhihirisho tosha kwamba unuangwa mkono na pande zote za kisiasa.

 

Wanafunzi wa Tanzania Thailand Waizungumzia sekta ya Madini.

                    

1 
Kamishna Msaidizi wa Madini  Mhandisi Hamis Komba katikati akiwa pamoja na Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand. Wa kwanza kulia ni Agatha Mwinuka, anayefuata ni Emmanuel Minja na wa kwanza 

kushoto ni Doricas Moshi. Wanafunzi wa Kitanzania nchini Thailand, wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenzao kutoka mataifa mbalimbali , ambao wamelitembelea  banda la Tanzania.
   
Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini katika picha ya pamoja na wanafunzi hao katika banda la Tanzania.
2
3 (2)
……………………………………………………………………………………
Na Asteria Muhozya, Bangkok
Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand, wamewataka wadau wa tasnia ya madini ya vito na usonara nchini Tanzania kuichukua sekta hiyo kwa umakini mkubwa kutokana na  mchango wake kiuchumi.
Aidha, wameeleza kuwa, nchi ya Thailand imepiga hatua kubwa katika sekta ya madini ukilinganisha na Tanzania lakini bado Tanzania inaweza kufaidika zaidi katika sekta hiyo ikiwa kila mdau atatimiza wajibu wake kikamilifu ili madini ya vito yaongeze mchango katika pato la taifa.
Wameongeza kuwa, Tanzania bado ina nafasi ya kujipanga upya kuhusu kuboresha zaidi sekta hiyo kama ilivyo kwa nchi nyingine  endapo mipango mikakati ya maboresho itatekelezwa  na kusimamiwa kikamilifu.
Wanafunzi hao wameyasema hayo, wakati walipolitembelea banda la Tanzania katika maonesho ya 53 ya Vito vya Usonara na Madini yanayoendelea katika jiji la Bangkok ambapo nchi zaidi ya 150 zinashiriki maonesho hayo.
“Thailand wamejipanga vizuri katika sekta ya madini. Wafanyabiashara wa madini wana umoja. Wadau wa madini wanatakiwa kuelewa  kuwa madini yanawakilisha utajiri wetu tulionao”. Amesema Agatha Mwinuka.
Aidha, wameitaka serikali na  wadau wa Tanzania  wanaoshiriki maonesho hayo kujifunza kutokana na changamoto wanazozipata kutoka kwa nchi nyingine, jambo ambalo litasaidia kuboresha sekta ya madini na vito, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kuhakikisha  kuwa wanafuata sheria na taratibu zilizopo.
“Tunaiomba serikali iendelee kuendeleza viwanda vya kukata madini. Ni jambo zuri kama shughuli hizi za kukata madini zitafanyika ndani ya nchi badala ya nje. Jambo hili linasaidia sana kuongeza thamani ya madini.  Ameongeza, Emmanuel Minja.
Akiongelea kuhusu umuhimu wa kuendeleza na kuboresha kituo cha Tanzania Geomological Center,  Doricas Moshi, ameeleza kuwa,  kituo hicho kinaweza kutoa mchango mkubwa katika tasnia hii hasa katika nyanja ya ukataji madini  na uthamini wa madini hivyo, ameitaka Serikali kukiongezea nguvu kituo hicho kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya  Tanzania.
“Chuotunachosoma hapa kinatumia sana mifano ya madini ya Tanzania katika kufundisha.  Mengi yametoka nyumbani, hii ni ishara nzuri. Serikali iliangalie hili. Ameongeza Doricas.
Aidha, wameeleza kuwa, soko la kimataifa kwa madini ya Tanzania lipo, hivyo, wamewataka wadau wote kuhakikisha wanashirikiana vizuri na serikali kuendeleza sekta hiyo kutokana na umuhimu na mchango wake kwa taifa. 
Akizungumzia  mipango iliyopo ya kuboresha sekta hiyo, Kamishna Msaidizi wa Madini, Mhandisi Hamis Komba, amesema kuwa, Serikali kupitia Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), inatekeleza mikakati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo na wa kati  ili waweze kuendana na   mahitaji ya soko la kimataifa kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali yakiwemo ya kukata madini, kuyaongezea thamani na  kuwapatia mikopo kupitia Benki ya TIB.
“STAMICO imepewa jukumu la kuwaendeleza wachimbaji wadogo katika sekta ya madini hususani katika masuala ya uchimbaji, uongezaji thamani madini na biashara ya madini. Serikali imejipanga vizuri katika hilo”. Ameongeza Kamishana. 
Ameongeza kuwa, Serikali inatambua kwamba wachimbaji wengi wapo katika sekta ya madini ya vito na usonara hivyo, jitihada za kuwaendeleza  zitasaidia kufikia kiwango bora cha utendaji wao wa kazi.
Vilevile, ameongeza kuwa, kutokana na kuboreshwa kwa Sheria ya madini ya mwaka 2010 ambayo inaiwezesha STAMICO kumiliki asilimia 50 ya hisa katika mgodi wa Tanzanite One, jambo ambalo linaifanya Serikali kuwa mmiliki katika mgodi huo

Mtikila akwaa Kashfa ya Kuwatunza Viongozi wa FDLR Jijini Dsm




Nilikuwa nasoma ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliyowakilishwa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa January 2014. Ripoti inaongelea masuala mengi, lakini nimeona siyo vibaya ku-share nanyi sehemu inayohusiana na Mchungaji Mtikila kukubali kuwa-host rebels wa FDLR nyumbani kwake Dar Es Salaam na masuala mengine kuhusiana na Tanzania.
Pia ripoti inadai kuwa vyombo vya usalama vya Tanzania vilimweka under house arrest Dar Es salaam mmoja ya viongozi wakuu wa FDLR anayejulikama kama Stanislas Nzeyimana (Bigaruka). Kwa wale wafuatiliaji wa mambo kwenye eneo la maziwa makuu watakumbuka kuwa kiongozi huyo alikuwa amepigwa ban ya kusafiri.

Serikali ya Tanzania ilipoulizwa na kundi hilo la wataalam wa Umoja wa Mataifa kuhusiana Bigaruka kusafiri na kukaa Tanzania, ilidai haikuwa na taarifa za kiongozi huyo kusafiri na kuishi Tanzania na hatimaye kupotea kwake ghafla. Inasemekana mpaka sasa hajulikani alipo kiongozi huyo huku taarifa nyingine zikidai kuwa wamekamatwa na serikali ya Rwanda. Wataalam hao wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuchunguza kuhusiana na kutoonekana kwa Bigaruka. Kwa wale ambao siyo wavivu wa kusoma, link ya ripoti nzima ya UN ipo hapo chini.

============================== ==============



A UN photo of Reverend Christopher Mtikila’s residence in
Dar Es Salaam, Tanzania, where FDLR second in command, Gen. Deogratias Nzeyimana, alias Bigaruka, stayed.
Reverend Christopher Mtikila has on several occasions hosted senior commanders of Rwandan FDLR rebels transiting through Dar es Salaam Tanzania in efforts to link them up with the outside work, the UN and the politician himself have confirmed. While in Dar es Salaam, they stayed at the personal residence of Rev. Mtikila which is identified in the photo above. According to UN Group of Experts report on DRC released on 24 January 2014, Reverend Mtikila confirmed to them that he had indeed hosted the FDLR political and military officials.

Disappearance of sanctioned FDLR leader Stanislas Nzeyimana (Bigaruka)
Early in February of 2013, one of the FDLR commanders from DRC disappeared. The UN experts say that while FDLR officers and intelligence sources from the region had told the Group that Rwandan officials were detaining Bigaruka, other FDLR sources alleged that Tanzanian security services placed Bigaruka under house arrest in Dar Es Salaam. The UN Group attempted to confirm this allegation with the Tanzanian authorities, which told the Group they were not aware of Bigaruka’s travel and stay in Dar Es Salaam, and had no information about his disappearance or whereabouts.

The UN Group however documented Bigaruka’s travel to Tanzania in violation of the travel ban imposed upon him. Three individuals, including Joseph Nzabonimpa (see S/2012/843, para. 101; Annex 40), told the Group that they – along with Faustin Murego – travelled to Dar es Salaam in January 2013 and met Bigaruka to discuss demobilization and disarmament as well as the issue of child soldiers (see annex 41).

At the beginning of his stay in Dar es Salaam, Bigaruka stayed in the house of Tanzanian reverend Christopher Mtikila, which the reverend acknowledged to the UN Group (see annex 42). In early February, after these meetings, Bigaruka disappeared. The Group continues to investigate the matter.

TOTAL YAZINDUA AWANGO KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME


Mgeni rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua.
Waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia tukio mojawapo katika hafla hiyo.
Kikundi cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini na pembezoni mwa miji.
Meneja wa Maswala ya Kisheria na Ushirika wa kampuni ya TOTAL Tanzania Bi. Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.

DTBi - COSTECH WATILIANA SAINI YA USHIRIKIANO NA SILION VALLEY YA MAREKANI

Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi sign MOU copy  Bw.Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi (kulia) wakisaini MOU.

 

Na Mwandishi Wetu, MOblog Tanzania
KAMPUNI tanzu ya Tume ya sayansi na teknolojia ya DTBi-COSTECH na Silicon Valley Black Chamber of Commerce’s Center for Entrepreneurial Development (SVCED) wametiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano (MoU) ambapo pande zote mbili zitashirikiana kwa njia mbalimbali kwa ajili ya ukuaji wa wajasiriamali.

Mkataba huo, kati ya DTBi na SVCED utawezesha pande hizo mbili kukuza ujasiriamali na kujenga uwezo katika Habari, Teknolojia na Mawasiliano kwenye sekta zote za kiuchumi.

Mkataba huo wa MoU utawafanya wadau kufanya shughuli za biashara kwa kuanza na mfumo wa teknolojia ya habari na mawasiliano kwa kupitia njia ya mtandao na kusaidia wale walio na ubunifu katika nyanja mbalimbali za biashara.

 

 Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi shake hands after signing MOU copy

Bw. Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi kupeana mikono baada ya kusaini MOU.

Mkataba huo pia utasaidia wajasiriamali kuweza kukua na kufanya biashara kwa kutumia mifumo habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ujasiriamali na kuanzisha mfumo wa kubadilishana uzoefu katika kuendeleza biashara na ukuaji wa ujasiriamali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi, Injinia. George Mulamula amesema mkataba MOU utatoa ushirikishiano ambao utaruhusu wajasiriamali wa Tanzania kufaidika na ujuzi, maarifa ya Silicon Valley ya ujasiriamali.

Amesema hii itasaidia nchi ya Tanzania kuruhusu uanzishwaji wa biashara kupitia njia ya mtandao na mifumo ya Habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ajira na kuchangia pato la taifa.
Mr Mulamula explains the partnership to the press copy 
Eng.George Mulamula akielezea ushirikiano kwa vyombo vya habari.
Baada ya kutiliana saini ya MOU, Bw Carl Davis Jr, alikuwa na semina kwa wajasiriamali yenye jina la “The Mindset of the Silicon Valley Entrepreneur: Lessons for the Tanzania Entrepreneur/Innovator”.

Mr Davis Jr amesema anaweza kuwasaidia “wajasiriamali kuelewa jukumu la uzinduzi na ujasiriamali na jinsi Wajasiriamali hapa nchini jinsi wanavyoweza kujiinua katika kufikiri chanya kwenye maeneo ya biashara.

Bw. Carl Davis Jr, akitoa majadiliano DTBi kwa wajasiriamali wa Tanzania juu ya jinsi ya kuwa mwekezaji mwenye mafanikio.
Attendee contributing to the discussion copy
Mshiriki akichangia mjadala.

Tanzania tunapaswa kuiga hili: Roboti zatumika Kuongoza magari DRC

 

Roboti barabarani DRC

Je Roboti kubwa zenye sauti nzito na mikono mikubwa zinaweza kuwa jibu kwa kupunguza msongamano wa magari barabarani?
Hili ndilo suluhu abalo serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imebuni ili kupunguza foleni ya magari mjini Kinshasa.
Mbinu hii ya kupunguza foleni ya magari inafanyiwa majiribio mjini Kinshasa.
Roboti mbili zilizotengezwa na kikundi cha watu zimepata kuungwa mkono na wananchi na maafisa wakuu, wanasema kuwa zinasaidia kupunguza msongamano wa magari barabarani.
Mji wa Kinshasa una wakazi milioni 10 na sifa yake kuu ni uendeshaji ovyo wa magari pamoja na msongamano mkubwa wa magari.
Licha ya kuwepo roboti, kuna pia taa za kawaida ambazo hutumiwa kurahisisha kuelekeza magari barabarani. Magari makuu kuu na madereva wasiojali sana sheria za barabarani.
Polisi wa trafiki pia wamekuwa wakituhumiwa kwa kuchukua hongo kutoka kwa wakiukaji wa sheria za barabarani hasa kutokana na kupokea mishahara midogo.
Mmoja wa wakazi wa Kinshasa anasema kuwa wakati Roboti hizo zinaposimamisha magari, unaona madereva wanatii huku watu wakivuka barabara bila matatizo yoyote.
Wengi wanalaumu polisi wa trafiki kwa kuwahangaisha . Wanataka Roboti waachwe zifanye kazi hiyo ya polisi.
Roboti hizo zina urefu wa mita 2.5 na zilianza kutumika mwezi Juni mwaka jana katika barabara yenye shughuli nyingi sana mtaa wa Lumumba Boulevard.
Roboti hiyo husema kwa sauti kubwa: ''Madereva mnahitaji kutoa nafasi kwa watu kuvuka barabara,'' huku ikiinua mkono mmoja ukionyesha taa nyekundu na kijani kama ishara ya kuenda au kusimama.CHANZO BBC SWAHILI

 

World Bank defers $90m loan to Uganda due new anti gay law.

 

President Museveni signed the controversial bill on Monday 

The World Bank has postponed a $90 million loan to Uganda after the country new anti gay law has drawn harsh criticism from across the globe. The loan was due to support and boost Uganda’s health services.
World Bank officials stated that they would not be willing to donate the money unless they could guarantee that projects that the money was destined to support would not be adversely affected by the new law.         
The new law was passed on Monday and is set to strengthen already strict legislation concerning homosexuals in Uganda. The law states that any person ‘promoting’ homosexuality is deemed a criminal and acts of ‘aggravated homosexuality’ are punishable by life imprisonment. The bill originally proposed the death penalty for some homosexual acts, but that was later removed amid international criticism.
The Ugandan government’s move has drawn harsh criticism from the EU with countries such as Denmark and Norway redirecting aid away from the government.
The US has also condemned the move with US Secretary of State John Kerry calling the law “atrocious”. South African Nobel peace laureate Desmond Tutu has compared the law to the anti-Semitic laws in Nazi Germany or the racial abuse seen in apartheid South Africa.
 World Bank President, Jim Yong Kim warned that the restriction of sexual rights through legislation ‘can hurt a country’s competitiveness by discouraging multinational companies from investing or locating their activities in those nations’.
The loan was due to be accepted on Thursday to support a loan given in 2010 focusing on family planning, maternal health and newborn care.
A spokesman for the World Bank said: ‘We have postponed the project for further review to ensure that the development objectives would not be adversely affected by the enactment of this new law.’
Uganda has already incurred huge financial loss due to the law but the World Bank’s withdrawal is by far the largest financial penalty the country has had to sustain. US President Obama has warned the law could ‘complicate’ Washington’s relations with Uganda, which receives a reported $400m (£240m) in annual aid from the US.
Despite vocal international criticism, Ugandan President Yoweri Museveni pushed forward and signed the anti-gay bill earlier this week.
Government spokesman Ofwono Opondo defended Museveni, stating he wanted ‘to demonstrate Uganda’s independence in the face of Western pressure and provocation’.
Homosexuality is illegal in 38 African countries, where most sodomy laws were introduced during colonialism. In Uganda, homosexual acts were punishable by 14 years to life in prison even before the controversial bill was signed into law.

 

Wednesday 26 February 2014

Miili 5 yapatikana mgodini A. Kusini

 

Wachimba migodi waliookolewa wiki jana wanakabiliwa na kesi mahakamani
Miili ya wachimba migodi haramu watano, imepatikana karibu na mgodi ambao ulikuwa hautumiki nchini Afrika Kusini.
Miili ya wanaume wanne na mwanamke mmoja ilipatikana karibu na mgodi huo katika eneo la Roodepoort, Magharibi mwa Johannesburg.
Vifo vyao vimetokea wiki moja baada ya shughuli kubwa ya uokozi wa zaidi ya wachimba migodi 20 haramu waliokuwa wamekwama ndani ya mgodi Mashariki mwa Johannesburg.
Walikamatwa baada ya kuokolewa na sasa wanakabiliwa na kosa la uchimbaji haramu wa migodi.
Afrika Kusini hupoteza mamilioni ya dola katika shughuli za uchimbaji haramu wa madini kila mwaka.
Ardhi inayozingira mji wa Johannesburg ina migodi mingi ambayo haitumiki na ambayo huvutia wachimba migodi haramu kutoka katika eneo hilo na nchi jirani za ,Lesotho, Msumbiji na Zimbabwe.
Mvuto wake hasa huwa ni kwamba zinaweza kuwa na madini ya dhahabu.
Wakati nyingi ya migodi hizo hazina faida za kifedha, bado zina mabaki ya dhahabu kiasi cha kuwavutia watu wengi wasio na ajira.
Waokozi wanasema kuwa bado huenda kuna wachimba migodi haramu zaidi ndani ya migodi hiyo.

 

Uganda yahofia kunyimwa misaada

Waziri wa mambo ya nje nchini Uganda, Sam Kutesa amesema ana wasiwasi kuwa Marekani huenda ikasitisha msaada wake kwa taifa hilo baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria dhidi ya ushoga nchini humo.

 

Bwana Kutesa amesema kuwa watu sharti wawe na maadili na kukubali msaada.
Balozi wa Marekani nchini Uganda Scott DeLisi, awali aliitaka serikali ya Uganda, kubatilisha sheria hiyo.
Alisema alihitaji kufafanuliwa zaidi sheria hiyo, kabla ya Marekani kujua ikiwa itaendelea na mipango yake ya misaada kwa nchi hiyo hasa miradi ya kupambana dhidi ya HIV na Ukimwi..
Sheria hiyo mpya, inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kupiga marufuku kile inachosema kusambaza vitendo vya ushoga.


Asasi za DRC zataka el Bashir ashikwe.

Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, yamesema kuwa Serikali ya nchi hiyo itachukuliwa kuwa dhaifu iwapo hamkamati Rais wa Sudan, Omar el Bashir.

 

Rais wa Sudan Omar el bashir

Mashirika yapatayo 90 yalitoa wito Serikali ya DRC imkamate el Bashir ambaye alikuwa mjini Kinshasa kushiriki katika vikao vya muungano wa COMESA.
Mmoja wa waandalizi wa maandamano ya kushinikiza Serikali imkamate kiongozi huyo wa Khartoum, Bwana Andre Kito Masimango, amesema:
"kuna barua ambayo inasema kuwa mahali po pote ambapo El Bashiri anapatikana anapaswa kukamatwa na kupelekwa kwenye mahakama ya kimataifa."
Mkerektwa huyo wa haki za kibinadamu anasema kuwa Rais El Bashir anapaswa kukamatwa kwa heshina ya waathirika wa dhuluma inayodaiwa kufanywa nchini Sudan na hata DRC yenyewe.
Watu kadhaa ambao wametoa maoni kwenye mtandao wa BBC wamesema kuwa lilikuwa kosa kwa Serikali ya DRC kumkaribisha Rais El Bashar kwa mkutano wa COMESA huku ikijua kuwa anatafutwa.
Hata hivyo kuna wale wanaosema kuwa msimamo wa Umoja wa Afrika (AU) ambao unasema kiongozi anayetawala hapaswi kukamatwa unapaswa kuzingatiwa ili El Bashir asikamatwe ugenini DRC.

 

Marekani yaonya Urusi kutoivamia Ukraine



 Marekani imeionya serikali ya Moscow isithubutu kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Ukraine.
Hatua hii inawadia siku moja tu baada ya Urusi kuamuru kufanyika kwa mazoezi ya kijeshi yanayoshirikisha askari wapiganaji laki moja na nusu kwenye mpaka wake na Ukraine .
Kujitokeza kwa wanajeshi wa Urusi kwenye mpaka na Ukraine kumeimarisha uhasama ulioko kati ya Urusi na mataifa ya Magharibi.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema kuwa Urusi inapaswa kukubali ushauri ya kwamba mataifa ya kigeni yasiingile mambo ya ndani ya Ukraine.
Alisema kuwa kujiingiza kijeshi katika hali ilivyo nchini Ukraine kwa hivi sasa ni kosa kubwa.
Mawaziri wa ulinzi kutoka mataifa ya muungano wa NATO wametoa taarifa ambapo wamesema kuwa wanachama wake wataendelea kuunga mkono uhuru na hadhi ya taifa la Ukraine.
Serikali ya Marekani imesema kuwa imetenga mbinu mbalimbali inazotazamia kutumia kuimarisha Ukraine kiuchumi, huku kukiendelea kuwa na hofu kuwa huenda taifa hilo likashindwa kuendelea kulipa madeni yake.
Kwa wakati huu msaada wa kijeshi pekee kwa Ukraine hautoshi kwani taifa linalotaka kusaidia lazima kwanza liimarishe hali ya kukubaliwa kwake katika taifa hili ambalo limegawanyika kwa imani yake kati ya Urusi na mataifa ya Magharibi.
Wabunge kadhaa wa Marekani wameonya kuwa Jumuiya ya Ulaya na Marekani wasipotoa msaada wa pesa taslimu Urusi huenda ikafanya hivyo.

 

 

Tuesday 25 February 2014

Wasiwasi wa Ukraine kusambaratika

Rais wa mpito wa Ukraine, Olexander Turchynov, ameonya kuhusu tisho la kusambatarika kwa nchi hiyo kufuatia kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais,

 

 

 

 

 

 

 

Rais wa mpito Olexander Turchynov asema tangazo litatolewa Alhamisi

Viktor Yanukovych.
Matamshi yake yanakuja wakati ambapo upinzani ukitokota katika maeneo ya Ukraine ambapo Kirusi kinazungumzwa dhidi ya serikali ya mpito.
Bunge la Ukraine limechelewa kuiunda serikali ya mseto.
Tangazo lilitarajiwa siku ya Jumanne kufuatia kung'atuliwa mamlakani aliyekuwa Rais Viktor Yanukovych, lakini Rais wa mpito Olexander Turchynov, amesema kuwa litatolewa siku ya Alhamisi ili kuruhusu mashauriano kuendelea.
Turchynov ameelezea wasiwasi wake kwa kile alichokitaja kama hatari ya kugawanyika kwa baadhi ya maeneo nchini Ukraine.
Kumetolewa waranti ya kukamatwa Yanukovych kwa madai ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji, lakini hajulikani aliko.
Wanadiplomasia wakuu wa Umoja wa Ulaya wanakutana katika mji mkuu Kiev kujadili usaidizi wa kifedha kwa serikali ya mpito, huku nchi hiyo ikitishiwa na mdororo wa kiuchumi kufuatia maandamano ya miezi mitatu.
Jumuiya ya Kimataifa
Kumekuwa na wasiwasi katika jumuiya ya kimataifa kuwa huenda Ukraine ikagawanyika mara mbili; upande mmoja ukiwa karibu na Umoja wa Ulaya, na mwingine ukiegemea upande wa Urusi.
 
Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza, William Hague, anasafiri kwenda Washington-Marekani, kulijadili suala hili.
Katika taarifa aliyoitoa bungeni, alisema kuwa Ukraine inahitaji msaada wa dharura wa fedha wa kimataifa ili kuimarisha uchumi wake unaozorota.
Ingawa kumekuwa na msimamo mkali kutoka kwa Urusi, Hague, amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa Umoja wa Ulaya na Urusi kufanya kazi pamoja.
Hague alisema, 'Azimio letu kuu ni kuendeleza demokrasia, kutetea haki za kibinaadam, na kufuatwa kwa sheria nchini Ukraine.
Hii sio kuhusu uamuzi wa Ukraine kuchagua kati ya Umoja wa Ulaya ama Urusi. Ni kuhusu kuielekeza nchi hiyo katika njia ya kidemokrasia katika siku zijazo'.

Wanamgambo waua wanafunzi Nigeria

Wanamgambo wa Kiislam wa kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria wametuhumiwa kushambulia shule moja na kuwaua wanafunzi kadhaa.
Polisi nchini Nigeria wameliambia Shirika la Habari la Uingereza, Reuters kwamba wote waliouawa ni wavulana na kwamba baadhi ya miili ya wanafunzi hao imeungua na kubaki majivu.
\
Taarifa ya jeshi la Nigeria imesema shambulio hilo limefanyika katika jimbo la Yobe.
Wakaazi wa mji wa Buni Yadi katika jimbo hilo, wamesema washambuliaji hao walivamia usiku na kuwachinja baadhi ya wanafunzi.
Wamesema baadhi waliuawa kwa kupigwa risasi.
Walimu katika chuo cha serikali ya shirikisho katika mji wa Buni Yadi wameliambia shirika la habari la AP kwamba wanafunzi wapatao 40 waliuawa katika shambulio hilo ambalo lilianza mapema Jumanne asubuhi.
Jeshi limethibitisha kwamba shambulio hilo limetokea katika hosteli za wanafunzi lakini limesema haliwezi kutoa taarifa zaidi kwa sasa.
Kundi la Boko Haram limekuwa likishutumiwa kuendesha vitendo vya mauaji kaskazini mwa Nigeria, yakiwemo mauaji ya mapema mwezi huu katika jimbo la Yobe.
Boko Haram, lina maana ya"Elimu ya Magharibi ni dhambi" katika lugha ya Kihausa, mara kwa mara limekuwa likishambulia shule katika siku za nyuma.
Watu kadhaa wameuawa katika mashambulio mawili yaliyotokea wiki iliyopita. Katika tukio moja, wanamgambo hao wa Boko Haram, waliteketeza kijiji kizima na kuwapiga risasi wakaazi wa eneo hilo waliokuwa wakijaribu kutoroka.

Msaada wa Marekani kwa Uganda

   

John Kerry asema Uganda inakiuka haki za binaadamu

Marekani haikufurahishwa na hatua ya Uganda kuidhinisha sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.
Waziri wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema tangu Uganda iidhinishe mswada huo miaka minne iliyopita, Marekani ilieleza wazi kwamba sheria hiyo inakiuka jukumu la kuhakikisha kuwepo haki za binaadamu ambalo tume ya haki za binaadamu Uganda inatambua linaambatana na sheria ya Uganda.
Kerry amesema,' Baada ya kuidhinishwa sheria hii, tunaanza ukaguzi wa ndani wa uhusiano wetu na serikali ya Uganda, kuhakikisha kwamba pande zote za uhusiano wetu, ukiwemo miradi ya msaada, zinapinga sera na sheria zinazowaonea watu na tuwe na uhusiano unaodhihirisha maadili yetu'.

Tamko hilo limetolewa siku moja baada ya rais Yoweri Museveni kukaidi shinikizo la kimataifa na kutia saini sheria hiyo iliyo zusha mzozo, inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja Uganda, hatua iliyozusha hisia kali.
Baadhi ya mataifa ya magharibi tayari yanatishia kukatiza msaada wa moja kwa moja kwa serikali ya Uganda.

Marekani inasema kuidhinishwa kwa sheria hiyo kunatishia hatari ya kurudi nyuma katika uwajibikaji wa Uganda kulinda haki za raia wake na kutishia jamii ya wapenzi wa jinsia moja Uganda.


WHY TANZANIA WILL SOON OVERTAKE KENYA IN CREATING MILLIONAIRES 

  

Tanzania is creating dollar millionaires faster than any other East African country, a new report says.
This means that East Africa’s newest millionaires are likely to come from Tanzania, as opposed to Kenya, Uganda, Rwanda or Burundi.

According to the African 2013 Wealth Book, the country is ranked third in Africa, after Ethiopia and Angola, with its millionaires’ club growing at a rate of 51 per cent between 2007 and 2013.

While it had 3,700 millionaires in 2007, this number had risen to 5,600 by 2013. Tanzania is followed in the region by Kenya, the only other regional country that features among the top 10 in Africa. Kenya is reported to have had 8,300 millionaires in 2013 against 6,700 in 2007, a growth rate of 24 per cent.

The report, put together by New World Wealth, defines millionaires or high net worth individuals (HNWIs) as those with net assets worth $1 million or more, excluding the value of their primary residences. The survey includes only those countries that had over 800 millionaires in 2013.

On the scale of absolute numbers, Kenya is up there, mixing it up with Africa’s big boys, coming fourth after South Africa (48,700), Egypt (22,800) and Nigeria (15,700).

Tanzania’s faster acceleration must be understood in the context of a country that is coming from a low base.

After decades of a command economy in which the government controlled most of the wealth, the liberalised economy is just warming up and the risk-takers among the population are clearly cashing in. Tanzania is also more resource-rich than its EAC partners.

It is endowed with vast natural gas and oil deposits, besides substantial quantities of gold, diamond and tanzanite. It also has the region’s biggest water and forest resources and is often referred to as the “lungs of the region.”

Thus the newly created millionaires probably individuals who have bet their money on its rapidly developing oil, gas and minerals sector, where massive deposits of offshore gas have made Tanzania a leading investment destination for prospectors and developers. As of June 2013, 42.7 trillion cubic feet of natural gas (about 7.5 billion barrels of oil equivalent) has been discovered in Tanzania.

Tanzania’s gold sector has also witnessed a boom in the past few years, and it is now the country’s leading export, worth $2.2 billion in 2012, followed by tobacco exports at $223 million and coffee at $187 million.

It recorded a growth of 45 per cent between 2007 and 2012 against Kenya’s 20 per cent. Even then, Kenyans were generally richer than their Tanzanian counterparts at a per capita income of $862 against the latter’s $609 in 2012.

In average terms, the richest Africans are to be found in South Africa ($7,508 per capita income), Angola ($5,485), Algeria ($5,404), Tunisia ($4,237) and Egypt ($3,187). While South Africa is known to have a resource-rich and fairly sophisticated economy, Angola is the beneficiary of its oil. The Maghreb countries’ good fortune is a result of a mix of oil and “welfarist” public policies.

Uganda leads the pack in expanding individual wealth in the region. Closer home, Kenya is expected to have 21,200 dollar millionaires, compared with Tanzania’s 15,200.

Mugabe Aikosoa Afrika kwa Kukosa Shukrani kwa Nyerere...SOMA ZAIDI!

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amesema kushindwa kwa viongozi wa Afrika kumuenzi Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere kwa mchango wake katika ukombozi wa Afrika ni jambo la kufedhehesha.

 Mugabe 

Rais Robert Mugabe
Kiongozi huyo mwenye miaka 90, alikuwa akiongea kwenye sherehe yake ya kuzaliwa iliyofanyika Jumapilii hii nchini Zimbabwe muda mfupi baada ya kuwasili kutoka Singapore alikoenda kufanyiwa upasuaji wa macho. Alisema viongozi wa Afrika wanapaswa kufanya zaidi kumuenzi Hayati Mwalimu Nyerere aliyeifanya Tanzania kimbilio la vuguvugu la ukombozi barani. Nyerere alikuwa na mchango mkubwa kwa kukamata madaraka kwa Mugabe.
Mwalimu Nyerere enzi za Uhai wake 
Mwalimu Nyerere enzi za Uhai wake
Maelfu wa wananchi wa Zimbabwe walijitokeza kwenye uwanja wa Marondera kwenye sherehe hiyo inayodaiwa kugharimu dola milioni 1 za Kimarekani

Mugabe Aelezea Heshima anayonyimwa Nyerere.

“Nataka kusema, wakati ambapo heshima zimekuwa zikimwagwa kwa mashujaa wa Afrika, mtu anayeonewa ni Mwalimu Julius Nyerere,” alisema Mugabe. “Hapa tulipo, vuguvugu za ukombozi, kule tulikokuwepo – tulitegemea msaada wa Tanzania. Lakini hakuna kinachosemwa kuhusu mtu huyu na nchi yake kwenye Jumuiya ya Afrika.”
Mugabe ambaye ni makamu mwenyekiti wa AU, alisema bara la Afrika linapaswa kukumbushwa fadhila inazotakiwa kumlipa Mwalimu Nyerere.
“Nataka sisi Wazimbabwe, kusimama kwaajili ya Nyerere. Afrika inatakiwa kukumbushwa wajibu iliomtupia mtu huyu, mzigo wa kuendesha vuguvugu zote za ukombozi,” alisema. “Mwisho wa siku, hakuna hata mmoja anayesema Tanzania ilistahili japo kutajwa tu kwa kufanikisha mission hii, mission ya kuwa nasi kama marafiki, mission ya kutufanya tuendeshe vuguvugu za ukombozi wa Afrika. Wote tulienda kwa njia tofauti, kwa sura tofauti hadi Tanzania kukomboa nchi zetu na hatujaenda tena Tanzania. Well, naenda kuwa mwenyekiti wa AU, ntashughulikia suala hili,” alisema.
“Hakuna aliyetambua kile Nyerere alichokifanya. Sisi wa Wazimbabwe sio wachoyo wa shukrani, ni taifa lenye shukrani na tutamuenzi mtu huyu.”

 

Watoto milioni moja wauawa katika Vita

 
Watoto wateseka kutoka na vita  
Watoto Milioni moja hufa siku yao ya Kuzaliwa
Shirika la Misaada kwa watoto, Save the Children, linasema kuwa watoto milioni moja hufariki dunia kila mwaka katika siku yao ya kwanza ya maisha.
Katika ripoti mpya ya shirika hilo la misaada kwa watoto linasema vifo vya watoto wachanga vimesalia kuwa moja ya aibu za dunia ya sasa.
Hali ya watoto ni mbaya zaidi hasa katika mataifa yanayokabiliwa na mizozo.
Mwandishi wa BBC aliye Sudan Kusini, Anne Soy, amesema kuwa katika mazingira ya sasa ya Sudan Kusini, watoto na wanawake, hasa wale waja
wazito wanaokabiliwa na athari nyingi za vita vinavyoendelea nchini humo.
Amesema kuwa kutokana na vita watoto, walioandamana na wazazi wengine wakiwa pekee, wanaungana na akina mama kutembelea mwendo
mrefu ili kujiepusha na vita vya kikabila vinavyoendelea nchini.
Miundo msingi katika Sudan Kusini, kama vile hospitali ni chache sana jambo ambalo linatatiza maisha ya wanawake na watoto.
Katika hospitali ya mji wa Nimule kwenye mpaka wa Sudan Kusini na Uganda Kuna vitanda 174 pekee hospitalini idadi ambayo haiafikiana kamwe
na maelfu ya wagonjwa na wahasiriwa wa vita .
Save the children inasema kuwa vita vinawaathiri zaidi watoto huko Syria, Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la Save the Children linasema kuwa vifo hivi vingi vinaweza kuzuiliwa.


WAZIRI MKUU AKIWA NA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOMA LEO


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. Kulia ni mbunge wa Sumve Richard Ndassa.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014.

  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Singida Magharibi Mohamed Bissanga na Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa ,wote wakiwa ni wabunge wa Bunge Maalum la Katiba, nje ya ukumbi wa Bunge Mjiji Dodoama Februari 24, 2014.

 

 Waziri Mkuu, Mizengo, Pinda akizungumza na Katibu wa Bunge, Thomas Kashilillah, nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Februari 24, 2014. (Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)

SIKU TATU ZA CHADEMA WALIZOMPA RAIS KIKWETE ZIMEISHIA WAPI ?

 

Chadema kupitia kigaila walitoa siku tatu kwa rais afute kauli yake kuwa uvumilivu kwa wanaccm sasa basi. Leo ni zaidi ya wiki moja, aona kimya. Vipi, wamesahau? Hawana la kumfanya? Wamesalimu amri? Wamemuogopa? Tunaomba mrejesho wa kinachoendelea.

 

Monday 24 February 2014

Ajali mbaya Yatokea eneo la Mikese, Morogoro, leo Asubuhi

 

 

Ankle habari. Leo asubuhi eneo la Mikese, Morogoro, tumekutana na na ajali  mbaya sana ya magari mawili, moja la mafuta, kugongana uso kwa uso na kutumbukia mtaroni na yote kushika moto. Inasadikiwa mtu mmoja ambaye ni dereva wa magari hayo kateketea kabisa kwa moto. 


 

Hakuna cha kufanyika kutokana na moto mkubwa na moshi mwingi wakati magari hayo yakiteketea

 

 

Mlipuko mkubwa wakati matenki ya mafuta yakilipuka

Askari wa kikosi cha zimamoto wakijaribu kuuzima moto huo.Picha na Mdau Sixmund

TANZANIA KUPELEKA MAJESHI SUDAN KUSINI 

 Mzinga 3c649

Serikali inatarajia kupeleka kikosi kimoja cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) huko Sudan Kusini kwa ajili ya kulinda amani kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe anasema Dar es Salaam jana kwamba Serikali imekubali kupeleka batalioni moja baada ya kuombwa na Umoja wa Mataifa (UN).
Sudan ya Kusini imekuwa katika machafuko ambayo yamesababisha vifo vya mamia ya raia na wengine kujeruhiwa.
"Tumefanya uamuzi wa kupeleka majeshi yetu Sudan Kusini, tumefanya hivyo baada ya kuombwa na Umoja wa Mataifa kwa sababu ya ubora wa jeshi letu," Membe aliwaambia waandishi wa habari.
Anasema jukumu la kulinda amani katika Bara la Afrika ni la Waafrika wenyewe na kwamba Tanzania inajiona kwamba ina jukumu la kusaidia kupatikana kwa amani.
Anasema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon alimwomba Rais Jakaya Kikwete kusaidia kupeleka majeshi yake Sudan Kusini kusaidia kulinda amani. "Rais alikubali, sasa tuko kwenye maandalizi, nadhani Aprili jeshi letu litaondoka kuelekea Sudan Kusini," alisema Membe.

Kwa sasa Tanzania ina vikosi vya wanajeshi wa kulinda amani katika nchi za DRC, Darfur (Sudan) na Lebanon. Chanzo: mwananchi


MKUU WA MKOA WA NJOMBE ACHEFULIWA NA VYOO VYA MAKETE 

 

Tabia ya wakazi wengi wa wilaya ya Makete mkoani Njombe kujenga vyoo vidogo kiasi cha watumiaji kupata shida kuingia kujisaidia, imemchefua mkuu wa mkoa huo wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo hivi karibuni

Akizungumza wilayani hapa mkuu wa mkoa wa Njombe Kapt. Aseri Msangi amesema anakerwa na tabia ya wananchi wa makete wanaojenga vyoo vidogo hali inayosababisha kero kwa watumiaji kutokana na kupata shida tangu anapoingia hadi kutoka

 Mimi nashangaa kabisa badala ya mtu kujenga choo kikubwa kitakachopelekea mtu kujisikia nafuu anapoingia kujisaidia nyie mnajenga choo ambacho mtu akiingia kwanza anainama, na pili hawezi kugeuka akiingia, yaani akiingia kwa mbele anarudi kinyume nyume" alisema Msangi


Ametoa wito kwa wananchi hao kujenga vyoo vikubwa na vyenye ubora kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza magonjwa ya matumbo ambayo yanawakumba wananchi wengi na uchunguzi kubaini kuwa ni kutokana na kukosekana kwa vyoo bora vinavyotunzwa vizuri

Taswira,Bomoabomoa Inayoendelea Jiji la Arusha

 

 

 

 

Halmashauri aya Jiji la Arusha imevunja nyumba zake338 baada ya kushinda kesi iliyofunguliwa na wapangaji Sangito Sumari na wenzake 216 katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Arusha.

Operesheni hiyo inayojulikana kama “Operesheni Mongela”ilianza saa 12 asubuhi jana kwa kuvunja nyumba 56 eneo la Kilombero, nyumba 198 eneo la Kaloleni na nyumba 84 katika eneo la Themi.

Wengi walitegemea kuibuka vurugu wakati wa uvunjaji nyumba lakini hadi mchana hapakuwa na pingamizi kwa wapangaji badala yake wenyewe walihamisha vitu vyao mapema jana asubuhi kabla ya zoezi la kuvunja kuanza.

Hata hivyo kuvunjwa kwa nyumba hizo kumeleta neema kwa baadhi ya watu wakiwamo vijana wanaokusanya vyuma chakavu kuvamia maeneo hayo na kuokota kila aina ya chuma au kitu ambacho waliamini kinaweza kuuzwa na kuwapatia fedha.

Akiwa eneo la Kaloleni baada ya kukamiliza kuvunjwa nyumba za Kilombero, Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mongela alisema, ‘Operesheni Mongela’ ilipata baraka zote za viongozi wa Serikali wanasiasa wakiwamo madiwani wote Mbunge na Meya wa Jiji.

 

Friday 21 February 2014

Ukraine:Hatimaye makubaliano yapatikana

 

Habari za hivi punde zinaarifu kuwa ofisi ya rais Yanukovych nchini Ukrain imetoa taarifa inayosema kwamba mwafaka umefikiwa katika mazungumzo ya usiku kucha kati ya serikali, upinzani na waakilishi wa Muungano wa Ulaya na Urusi.
Taarifa hiyo hata hivyo haikutoa maelezo zaidi kuhusu makubaliano hayo ingawa ilisema kuwa pande zote zitatia saini makubaliano yenyewe.
Duru zinasema kuwa Rais Yanukovych amekuwa akikabiliwa na shinikizo apange uchaguzi wa mapema pamoja na mageuzi ya kikatiba.
Umoja wa Ulaya umekubali kuwawekea vikwazo viongozi waliopanga ghasia zinazoikabili Ukraine kwa sasa.
Uamuzi huo uliofanyika mjini Brussels, Ubelgiji umejiri baada ya watu kadhaa kuuawa mjini Kiev, katika siku ambayo ilishuhudia umwagikaji mkubwa zaidi wa damu tangu uhuru wa Ukraine zaidi ya miaka ishirini iliyopita.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Italia, Emma Bonino, amesema vikwazo hivyo vinavyojumuisha vya usafiri na kupiga tanji mali za wahusika na kwamba vinawalenga wale waliohusika na mauaji ya waandamanaji.
Ujumbe wa Umoja wa Ulaya mjini Kiev unajaribu kuwapatanisha viongozi wa upinzani na rais Victor Yanukovych ili kuleta amani na pia kushawishi taifa hilo kuandaa mapema uchaguzi uliopangiwa kufanyika mwaka ujao.
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa, Ban Ki-moon amesema hali nchini Ukraine ni ya kutamausha:
Wito huo umetolewa vile vile na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry ambaye ametaka vurugu kusitishwa nchini Ukraine akisema kuwa watu wa taifa hilo wanastahili kuwa na hali bora kuliko kile alichokitaja kuwa maafa na mateso yasiyofaa ambayo yameshuhudiwa katika barabara za mji mkuu, Kiev.
Haijabainika ni watu wangapi waliouwawa katika vurugu za Alhamisi lakini wizara ya Afya inasema tangu Jumanne, watu sabini wameuawa na zaidi ya 570 wamejeruhiwa.