Kweli Serikali itadhibiti ada kubwa vyuoni?
Kwa muda mrefu wananchi wa kada mbalimbali wamekuwa wakilalamika
kuhusu karo kubwa zinatozwa shuleni na katika vyuo vya elimu ya juu.
Kuna shule hapa nchini ambazo ada yake kwa mwaka inazidi kiwango kinachotozwa katika baadhi ya vyuo vikuu.
Hata hivyo, tatizo linatajwa kuwa kubwa zaidi
kwenye vyuo vikuu. Kwa mfumo ulivyo nchini wanafunzi wanapoomba nafasi
vyuoni, wanaweza kupangiwa chuo chohote.
Hali hii imekuwa ikiwaathiri wanafunzi wanaotoka
katika familia masikini, kwa sababu wanajikuta wamepangiwa chuo
kinachotoza karo kwa kiwango kikubwa.
Vyuo ni tofauti na shule kwa sababu mzazi ndiye anayeamua wapi ampeleke mwanawe kulingana na uwezo wa fedha alionao.
Inawezekana hili linalotokea katika taasisi za
elimu ya juu ndilo lililoisukuma Serikali kuanzisha kile ilichokiita
kama mfumo mpya wa upangaji ada kwa vyuo vikuu.
Akizindua mfumo huo hivi karibuni, Waziri wa Elimu
na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema utasaidia kudhibiti
viwango vya ada vinavyotozwa kwa wanafunzi.
Alisema Serikali imeanzisha mfumo huo utakaoanza
kutumika mwaka huu katika vyuo vyote, kwa lengo la kudhibiti ada
kulingana na fani zinazotolewa.
Kwa mujibu wa Dk. Kawambwa, mfumo huu ambao
baadaye utaendelea hadi shule za sekondari na msingi, umepatikana
kupitia kikosi kazi cha wataalamu ambacho pamoja na majukumu mengine
kilipewa kazi ya kutathmini gharama.
Dk. Kawambwa alisema moja ya faida ya utaratibu
huo mpya ni kudhibiti taasisi zinazotoza ada kubwa kwa sababu za binafsi
ikiwamo biashara.
Itakumbukwa pia kuwa, Aprili 2013 akifungua
mkutano mkuu maalumu wa Chama cha Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo
Visivyokuwa vya Serikali (Tamongsco) uliofanyika mkoani Mbeya, Rais
Jakaya Kikwete alisema: “Elimu ni huduma muhimu na haki kwa mtoto kwa
hiyo si vyema kugeuzwa kuwa biashara ya faida kubwa.’’
Pamoja na nia njema ya Serikali, nina shaka na
utekelezaji wa mfumo huu. Kila ninapoutazama kwa jicho la ndani sioni
zaidi ya ugumu katika kuutekeleza.
No comments:
Post a Comment