Monday 31 March 2014

TZ, Kenya lawamani kwa kukwamisha biashara A.Mashariki

Kilimanjaro. Tanzania na Kenya zinakwamisha kuanza kazi kwa Kituo cha pamoja cha Mpakani (OSBP) cha Holili wilayani Rombo, ambapo ujenzi wake ulikamilika tangu Desemba mwaka jana.
Kituo hicho ni kwa ajili ya ukaguzi wakati wa kuvuka mpaka wa Tanzania na Kenya, ambapo wananchi wa nchi hizo mbili watakaguliwa katika kituo kimoja badala ya viwili kama ilivyo sasa.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mipaka wa Taasisi ya Trademark East African (TMEA), Theo Lyimo alisema ujenzi wa kituo hicho umefadhiliwa na taasisi hiyo kwa Dola 5.7 milioni (Sh. 9.1 bilioni).
Lyimo aliwaeleza waandishi wa habari wa Tanzania na Kenya waliotembelea vituo vya Holili na Taveta. “Vituo hivi vikianza kazi kama mtu anatoka Tanzania kwenda Kenya atakaguliwa Taveta upande wa Kenya, ambako katika kituo hicho kutakuwa na maofisa wa nchi hizo mbili wa TRA, Uhamiaji na Afya ,” alisema.
Lyimo alisema jengo jingine linajengwa katika mpaka huo lipo katika eneo la Taveta upande wa Kenya litakalogharimu Dola 6.7 milioni (Sh.10.7 bilioni ) ambalo litakamilika katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.
Alisema pia kwa wasafiri wanaotoka Kenya kwenda Tanzania watakaguliwa katika eneo la Holili upande wa Tanzania ambako pia kutakuwa na maofisa wa nchi hizo mbili.

 

No comments:

Post a Comment