Monday 31 March 2014

Kweli Serikali itadhibiti ada kubwa vyuoni?

Kwa muda mrefu wananchi wa kada mbalimbali wamekuwa wakilalamika kuhusu karo kubwa zinatozwa shuleni na katika vyuo vya elimu ya juu.
Kuna shule hapa nchini ambazo ada yake kwa mwaka inazidi kiwango kinachotozwa katika baadhi ya vyuo vikuu.
Hata hivyo, tatizo linatajwa kuwa kubwa zaidi kwenye vyuo vikuu. Kwa mfumo ulivyo nchini wanafunzi wanapoomba nafasi vyuoni, wanaweza kupangiwa chuo chohote.
Hali hii imekuwa ikiwaathiri wanafunzi wanaotoka katika familia masikini, kwa sababu wanajikuta wamepangiwa chuo kinachotoza karo kwa kiwango kikubwa.
Vyuo ni tofauti na shule kwa sababu mzazi ndiye anayeamua wapi ampeleke mwanawe kulingana na uwezo wa fedha alionao.
Inawezekana hili linalotokea katika taasisi za elimu ya juu ndilo lililoisukuma Serikali kuanzisha kile ilichokiita kama mfumo mpya wa upangaji ada kwa vyuo vikuu.
Akizindua mfumo huo hivi karibuni, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alisema utasaidia kudhibiti viwango vya ada vinavyotozwa kwa wanafunzi.
Alisema Serikali imeanzisha mfumo huo utakaoanza kutumika mwaka huu katika vyuo vyote, kwa lengo la kudhibiti ada kulingana na fani zinazotolewa.
Kwa mujibu wa Dk. Kawambwa, mfumo huu ambao baadaye utaendelea hadi shule za sekondari na msingi, umepatikana kupitia kikosi kazi cha wataalamu ambacho pamoja na majukumu mengine kilipewa kazi ya kutathmini gharama.
Dk. Kawambwa alisema moja ya faida ya utaratibu huo mpya ni kudhibiti taasisi zinazotoza ada kubwa kwa sababu za binafsi ikiwamo biashara.
Itakumbukwa pia kuwa, Aprili 2013 akifungua mkutano mkuu maalumu wa Chama cha Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo Visivyokuwa vya Serikali (Tamongsco) uliofanyika mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete alisema: “Elimu ni huduma muhimu na haki kwa mtoto kwa hiyo si vyema kugeuzwa kuwa biashara ya faida kubwa.’’
Pamoja na nia njema ya Serikali, nina shaka na utekelezaji wa mfumo huu. Kila ninapoutazama kwa jicho la ndani sioni zaidi ya ugumu katika kuutekeleza.

 

Sasa tuseme ajali za mabasi zimetosha ajali hizi basi

Pamoja na ubora huo, pia mafunzo ya madereva yaangaliwe upya ili kabla ya mtu kupewa leseni awe ameiva, leseni pia tunashauri zidhibitiwe.

Kwa mara nyingine, nchi yetu imepata janga jingine kubwa baada ya ajali mbili kutokea katika mikoa ya Pwani na Kilimanjaro mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vifo kwa watu zaidi ya 30.
Ajali ya kwanza ilitokea Hedaru wilayani Same, Kilimanjaro ambayo imesababisha vifo vya waombolezaji 12. Nyingine ni ile iliyotokea Rufiji mkoani Pwani ambayo imeua watu 22 na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Tunachukua nafasi hii kipekee kuwapa pole majeruhi wa ajali hizi, tukiwaombea ili wapate nafuu haraka na kuendelea na majukumu yao.
Aidha, tunawapa pole waliofiwa na ndugu, jamaa na marafiki zao katika ajali hizi, hasa kipindi hiki kigumu cha majonzi. Hakuna shaka, ajali hizi ni mfululizo wa matukio ya kusikitisha yanayoendelea kutokea katika barabara nyingi nchini.
Ajali hizi hazitokani na uzembe wa madereva pekee, bali matumizi duni ya barabara zetu ikiwamo nyakati wa mvua za masika au hata kiangazi kutokana na vumbi. Tunashauri kila mtumiaji wa barabara awe makini, atimize wajibu wake ipasavyo.
Tukitumia mfano wa ajali za Same na Rufiji, jambo linalofanana ni magari yaliyohusika katika ajali hizo kugongwa na mengine kwa nyuma. Haya yametokea wakati kuna madai kuwa magari yamekuwa yakiachwa barabarani kwa muda mrefu yakiharibika bila kuondolewa.
Hii, tunasema inaweza kuwa sababu ya magari kugongana na kuuua abiria. Huu, bila shaka ni ushahidi wa jinsi ambavyo madereva, baadhi yao wasivyokuwa makini katika kuendesha vyombo vya moto. Tunashauri, wasimamizi wa uchunguzi wa magari, usalama wake wawe makini ili magari yanayoruhusiwa kuingia barabarani, kubeba abiria yawe kwenye ubora na viwango vinavyostahili.
Pamoja na ubora huo, pia mafunzo ya madereva yaangaliwe upya ili kabla ya mtu kupewa leseni awe ameiva, leseni pia tunashauri zidhibitiwe.
Ni wazi, kuruhusu magari yakiwamo malori madogo maarufu kama kirikuu kubeba abiria jioni au usiku ni mambo ambayo hayakubaliki na ni hatari. Hali hii inatokea katika maeneo mengi nchini ikiwamo Dar es Salaam, ambako askari wapo barabarani mchana kutwa.
Tunasema, udhaifu huu umekuwa sababu ya vifo, nasi kama jamii tunabaki kimya.
Tunashangazwa, kwa mfano, na ruhusa nyingine kwa magari madogo ya mizigo (pick-up), ya familia kama Toyota Noah na mengi yakiwa chakavu kuruhusiwa kubeba abiria.
Tunasema hivyo kwa muwa ndivyo ilivyotokea Same. Ni jambo linalosikitisha kwa kuachwa liendelee huku askari wa usalama barabarani wakishuhudia kana kwamba ni jambo la kawaida. Ruhusa hizi kwa malori madogo kubeba abiria ni jambo linalofanyika Dar es Salaam, mahali ambako kuna askari wengi wa usalama barabarani, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa. Ukimya huu katika roho za watu ni wa nini?

 

Mvua zaleta maafa makubwa Dar, mikoani

Mkazi wa Kijiji cha Bulembo mkoani Kagera, Godena Joseph akitafakari baada ya shamba lake la migomba kuharibiwa na mvua iliyoambatana na upepo. Picha na Issa Ibrahim.  

ar/Pwani/Kagera. Mvua zilizonyesha maeneo mbalimbali nchini tangu wiki iliyopita, zimesababisha maafa, uharibifu wa mali, miundombinu na kuacha zaidi ya familia 150 bila makazi.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa athari za kifamilia zimeukumba zaidi Mkoa wa Kagera ambako familia zaidi ya 125 zinahitaji msaada baada ya nyumba zao kuezuliwa paa na mashamba ya migomba kuharibiwa.
Ingawa maeneo mengi ya nchi yameathirika, hali inaonekana ni ya kiwango cha juu zaidi katika mikoa ya Dar es Salaam, Bukoba, Lindi na Mtwara.
Jijini Dar es Salaam, maeneo kadhaa yamejaa maji na hata kusababisha watu kuyakimbia makazi yao kama vile Jangwani, Bonde la Mto Msimbazi na Mbweni ambako Serikali ilipima viwanja na kuvigawa kwa wananchi.
Mkoani Kagera, maeneo yaliyoathirika zaidi ni ya vijiji vya Bulembo, Kata ya Kamachumu wilayani Muleba.
Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage alisema: “Hali siyo nzuri na timu ya watalaamu ipo eneo la tukio ili kufanya tathmini zaidi kuhusu kadhia hiyo.
“Watu wa Msalaba Mwekundu wanajaribu kurejesha paa upya katika baadhi ya nyumba zilizoezuliwa.”
Mkazi wa Kijiji cha Bulembo, Richard Kichabeba alisema familia zilizokumbwa na tatizo la nyumba zao kuezuliwa paa, zinaishi nje na mbaya zaidi nyumba zinazidi kuporomoka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
“Hakuna muhogo wala mgomba. Mawe na upepo vimevuruga kila kitu,” alisema mkazi huyo na kuongeza kuwa mbaya zaidi hata hizo paa zao hazijulikani zimeangukia wapi.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi alisema kuwa uongozi wa wilaya hiyo umelazimika kuifunga kwa muda usiojulikana Barabara ya Msata – Bagamoyo baada ya maji kuifunika.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Halima Kihemba alisema kuwa hivi sasa Kata mbili za Ruvu na Kwala hazifikiki baada ya madaraja kubomoka.
Alisema kuwa madaraja mawili ya Mto Ndwati na Msua yamefurika maji hali iliyosababisha mafuriko makubwa, hivyo aliwataka wakazi wa vijiji hivyo kuchukua tahadhari.

 

Sitta ampa barua Mtikila aende kwa JK

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba,Samuel Sitta.

Dodoma. Ombi la Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mchungaji Christopher la kutaka Bunge hilo livunjwe, limekuwa zito kwa Mwenyekiti Samuel Sitta.
Kutokana na ugumu huo, Sitta amelazimika kumpatia barua Mtikila ili awasilishe hoja yake kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye kisheria ana mamlaka hayo ya kuvunja Bunge la Katiba, ambalo limekuwa likionekana kwenda mrama.
Mtikila, ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia na mjumbe wa Bunge la Katiba aliwasilisha barua yenye hoja binafsi akitaka bunge hilo livunjwe na wajumbe warejee makwao kwa madai kuwa chombo hicho cha kutunga Katiba mpya hakijali maslahi ya umma na uongozi umekuwa haumtendei haki.
Majibu ya barua hiyo yalikuwa hivi: “Nimeagizwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu nikujulishe kwamba Bunge Maalumu halina uwezo wala mamlaka ya kujitangaza kwamba ni haramu na hivyo livunjwe ; na kwamba hoja hiyo haistahili kuwa hoja ya Bunge Maalumu,” inasomeka barua hiyo iliyoandikwa na katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamad.
Akizungumza na Mwananchi jana, Sitta alikiri kumpatia barua hiyo Mtikila ili aende kwa Rais Kikwete kwa sababu hoja yake kutaka kuvunjwa Bunge haiwezi kusikilizwa na chombo hicho kwa kuwa mwenye madaraka ya kuvunja Bunge ni Rais pekee.
“Ni kweli ametuletea hoja ya kuvunja Bunge. Ameandika mambo mengi, akitumia lugha ya uchochezi, kama kudai kwamba ‘Tanganyika imekuwa koloni la Zanzibar kwa muda mrefu’, lugha ya namna hii hatuwezi kuikubali,” alisema Sitta.
Sitta alisema siyo kila kitu ambacho mjumbe anasema, ni lazima kifuatwe katika mchakato huu wa kuandika Katiba Mpya.
“Mtu akija anasema anataka Bunge livunjwe amfuate aliyetuteua, siyo sisi wenyewe kujivunja,” alisema Sitta.
Alisema hoja ya Mtikila, ambaye alitishia kufungua kesi ya kuzuia Bunge la Katiba kufanya kazi, ya kutaka Bunge kuvunjwa imekwenda kinyume kabisa na taratibu za Bunge.
“Hoja hii imekwenda nyuzi 180 kwa sababu aliyetuteua alitaka sisi tutunge katiba kutokana na rasimu, ili sisi tupeleke kwa wananchi rasimu iliyopendekezwa,” alisema.
Mchungaji Mtikila alikiri kupokea barua kutoka Ofisi ya Bunge ikimweleza jambo moja; apeleke hoja yake kwa Rais Kikwete aliyeteua Bunge la Katiba.
Hata hivyo, alisema hakusudii kwenda kumuona Rais Kikwete baada ya kushauriwa kupitia barua ya Bunge kutokana na kutoa hoja ya kutaka kuvunjwa kwa bunge hilo.

Ukawa waanza mapambano nje ya Bunge

Mjumbe wa Bunge la Katiba wa kundi la Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (Ukawa), Ismail Jussa akionyesha moja ya nukuu za kitabu cha Profesa Issa Shivji wakati wa mkutano na waandishi Dodoma jana. Kushoto ni mjumbe mwenzake, Tundu Lissu. Picha na Salima Shao

Dar /Dodoma/Mwanza. Ni dhahiri kwamba mjadala wa msomi wa Sheria, Profesa Issa Shivji umewavuruga wanasiasa waumini wa serikali mbili ambao baadhi yao jana walimshukia wakidai kuwa “mzee huyu ni ndumila kuwili na kigeugeu.”
Shivji juzi alitoa mjadala kuhusu muundo wa Muungano na kuishutumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyopendekeza serikali tatu, kuwa ilipotosha maoni ya wananchi. Alipotakiwa kuzungumzia madai dhidi yake, Profesa Shivji alisema: “Nyie ni waandishi wa habari someni, angalieni wapi mimi nilisema Serikali tatu, wanaosema ninatumiwa na CCM hayo ni maoni yao siwakatazi kuzungumza wanachofikiria.”
Jana Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kampeni yake nje ya Bunge la Katiba, ulimtaka Profesa Shivji kuwaomba radhi wananchi kwa kile wanachodai kwamba amekuwa kigeugeu kwenye maandishi na matamshi yake kuhusu muundo wa Muungano.
Katika mkutano wake wa kuelimisha wananchi kuhusu Katiba Mpya mjini Mwanza uliojaa polisi kila kona, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa alisema wanamshangaa Profesa Shivji kwa mawazo yake yasiyoeleweka kuhusu muundo wa Muungano.
“Kwa kweli tunaamini watu ambao ni wasomi kama Profesa Shivji wanaweza kuwasaidia wananchi kupata katiba nzuri, lakini anachokifanya sasa ni siasa, jambo ambalo siyo jema,” alisema Dk. Slaa na kuongeza:
“Ukawa tunamtaka awaombe radhi wananchi, kwani amewadhalilisha kwa kuwa kigeugeu. Mara ya kwanza tunakumbuka alikuwa muumini wa Serikali tatu leo anageuka na kuanza kuhubiri serikali mbili, huu ni upuuzi kwa msomi kama yeye kufanya hivyo.”
Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema CCM wanaogopa Rasimu ya Katiba kwa sababu wamezoea uchakachuaji.
Naye Kaimu Katibu Mkuu wa CUF, Abdulkarim Kambaya alisema Rais Kikwete amewachezea akili wananchi, kwani awali alikuwa anaonyesha yupo upande wao lakini kupitia hotuba yake bungeni amewakana na kuibeba CCM.
Lissu, Jussa nao wanena
Pia baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana walimshambulia kwa maneno Profesa Isa Shivji kuwa ni ‘ndumilakuwili’.
Kwa nyakati tofauti, wajumbe Tundu Lissu na Ismail Jussa walisema kuwa Profesa Shivji “alibebwa na CCM na kulishwa maneno kwa masilahi ambayo hayajulikani.”
Akizungumzia hotuba hiyo, Jussa aliyeweka wazi masilahi yake kuwa ni mwanafunzi wa Profesa Shivji, alisema msomi huyo aliyekuwa tegemeo la wanyonge, alifanya upotoshaji mkubwa ambao umetoa vitisho kwa wananchi.

 

Ripoti ya CAG yaibua utata kisheria

“Tangu uhuru, taarifa ya CAG inawasilishwa katika mkutano wa Bunge wa Aprili kila mwaka. Kwa hali ya sasa, Rais atakaa na taarifa hiyo kwa zaidi ya miezi miwili akisubiri Bunge kukutana.”PICHA|MAKTABA

Dar es Salaam. Siku chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kupokea taarifa kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, utata wa kisheria umegubika suala hilo kutokana na ukweli kuwa ibara ya 143 (4) ya Katiba inataka Rais aiwasilishe bungeni taarifa hiyo ndani ya siku saba.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe alisema jana kuwa suala hilo lina madhara katika utendaji wa Serikali.
“Kuna madhara makubwa katika mzunguko wa uwajibikaji, kwani ni rahisi Serikali kuichezea taarifa ya CAG kabla haijawa ya umma. CAG anakagua fedha za Serikali kwa niaba ya wananchi kupitia Bunge. Hivyo ni lazima Bunge la Katiba lipishe Bunge la Muungano ili kupokea taarifa ya CAG,” alisema Zitto.
Aliongeza: “Tangu uhuru, taarifa ya CAG inawasilishwa katika mkutano wa Bunge wa Aprili kila mwaka. Kwa hali ya sasa, Rais atakaa na taarifa hiyo kwa zaidi ya miezi miwili akisubiri Bunge kukutana.”
Hata hivyo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema siku hizo saba ni baada ya Bunge kuanza.
“Hakuna utata wowote hapo, ukisoma vizuri kifungu hicho kinasema, Rais atamuagiza waziri anayehusika kupeleka taarifa hiyo bungeni siku saba baada ya Bunge kuanza, siyo siku aliyokabidhiwa. Kitu muhimu hapo ni pale kikao cha Bunge kinapoanza bila kujali kinaanza lini,” alisema Balozi Sefue.
“Katika hali ya kawaida, Bunge la Bajeti lilipaswa kuanza Aprili 8. Bunge la Katiba linahitaji pesa kutoka kwenye bajeti. Sioni namna Bunge la Katiba kuendelea kwa sasa. Itabidi liahirishwe mpaka Agosti,” alisema.
Suala la kuahirisha vikao vya Bunge la Katiba kupisha Bunge la Bajeti lilielezwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliyesema atamshauri Rais Kikwete kuangalia uwezekano huo.
Hata hivyo, Katibu wa Bunge, Thomas Kashilila akizungumzia uwezekano huo, alisema Bunge hilo litasubiri ratiba ya shughuli za Bunge la Katiba.
Dk Kashilila alisema Kamati ya Uongozi wa Bunge la Katiba inatarajiwa kutoa ratiba ya shughuli zake kuelekea Bunge la Bajeti.
“Inapofika Juni, Serikali inatakiwa kuidhinishiwa fedha kwa ajili ya matumizi yake, kwa hiyo mpango uliopo ni kuhakikisha kabla ya Juni 30, Bunge la Bajeti liwe limeanza kazi zake,” alisema.

TZ, Kenya lawamani kwa kukwamisha biashara A.Mashariki

Kilimanjaro. Tanzania na Kenya zinakwamisha kuanza kazi kwa Kituo cha pamoja cha Mpakani (OSBP) cha Holili wilayani Rombo, ambapo ujenzi wake ulikamilika tangu Desemba mwaka jana.
Kituo hicho ni kwa ajili ya ukaguzi wakati wa kuvuka mpaka wa Tanzania na Kenya, ambapo wananchi wa nchi hizo mbili watakaguliwa katika kituo kimoja badala ya viwili kama ilivyo sasa.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mipaka wa Taasisi ya Trademark East African (TMEA), Theo Lyimo alisema ujenzi wa kituo hicho umefadhiliwa na taasisi hiyo kwa Dola 5.7 milioni (Sh. 9.1 bilioni).
Lyimo aliwaeleza waandishi wa habari wa Tanzania na Kenya waliotembelea vituo vya Holili na Taveta. “Vituo hivi vikianza kazi kama mtu anatoka Tanzania kwenda Kenya atakaguliwa Taveta upande wa Kenya, ambako katika kituo hicho kutakuwa na maofisa wa nchi hizo mbili wa TRA, Uhamiaji na Afya ,” alisema.
Lyimo alisema jengo jingine linajengwa katika mpaka huo lipo katika eneo la Taveta upande wa Kenya litakalogharimu Dola 6.7 milioni (Sh.10.7 bilioni ) ambalo litakamilika katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.
Alisema pia kwa wasafiri wanaotoka Kenya kwenda Tanzania watakaguliwa katika eneo la Holili upande wa Tanzania ambako pia kutakuwa na maofisa wa nchi hizo mbili.

 

Wafanyabiashara Mwika walalamikia ushuru magari

Moshi. Wafanyabiashara wa mazao ya ndizi na maparachichi katika Soko la Mwika lililopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro wamelalamikia ongezeko la ushuru wa magari makubwa katika soko hilo.
Hali hiyo imesababisha wenye magari kuhamisha magari yao na kuyapeleka Soko la Mamsera wilayani Rombo na kuwaacha wananchi wa Mwika wakishindwa kuuza bidhaa zao.
Wafanyabiashara hao walikuwa wakiuza bidhaa hizo kwa wafanyabiashara wakubwa wa jijini Dar es Salaam, Kenya na mikoa ya jirani, lakini kwa sasa bidhaa hizo haziuziki baada ya wafanyabiashara wakubwa kukimbia ushuru ulioongezwa na wakala kutoka Sh 40,000 hadi Sh 60,000
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, Dk. Agustino Mrema alikiri kupokea malalamiko hayo na tayari amewasiliana na mkurugenzi wa halmashauri hiyo kufuatilia malalamiko.
Mrema alimuomba mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi kuingilia kati na kukaa na wakala pamoja na wafanyabiashara, ili kutoharibu biashara katika soko la kimataifa ambalo linawaleta wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya nchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Fulgence Mponji hakuweza kupatikana kuzungumzia malalamiko hayo. baada ya simu yake ya mkononi kutopatikana.

 

Programu ya kompyuta kuvuruga ATM wiki ijayo

Kwa mujibu wa Microsoft asilimia kubwa ya benki katika nchi zinazoendelea zinatumia programu ya Windows XP katika kuendesha ATM, hivyo kuwa moja ya waathirika wa mpango huo.

Dar es Salaam. Wiki moja kabla ya kusitishwa huduma za programu ya kompyuta (OS) ya Windows Xp, imefahamika kuwa waathirika wakubwa watakuwa ni benki na taasisi za fedha ambazo hutumia mfumo huo katika mashine za kutolea fedha (ATMs)
Shirika la Microsoft limethibitisha kuwa benki ni miongoni mwa taasisi nyingi zitakazoathirika na mabadiliko hayo.
Baadhi zimeanza kufanyia kazi tatizo hilo, ikiwamo benki moja ambayo jana alasiri ilituma ujumbe kwa wateja wake kuwa, “Ndugu mteja, kuanzia Jumamosi saa 2:00 usiku Aprili 5, mpaka Jumapili saa 12:00 asubuhi tutakuwa tunaboresha mashine zetu za ATM, hivyo kadi yako haitafanya kazi kwa kipindi hiki. Asante.”
Kwa mujibu wa Microsoft asilimia kubwa ya benki katika nchi zinazoendelea zinatumia programu ya Windows XP katika kuendesha ATM, hivyo kuwa moja ya waathirika wa mpango huo.
Katikati ya Machi, Microsoft ilitangaza kusitisha huduma zote zinazohusiana na bidhaa zake za Windows Xp kufikia Aprili 8, mwaka huu. Pia shirika hilo litasitisha ufanisi wa programu ya kuzuia na kupambana na virusi ya Microsft Security Essentials katika mfumo wa Windows Xp, hivyo kufanya urahisi wa kompyuta zinazoitumia kukosa ulinzi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Twiga Hosting, Jacob Urassa alisema Watanzania hawatakiwi kupuuza onyo hilo kwa kuwa ikifika Aprili 9 usalama wa taarifa zao utakuwa hatarini.
“Windows XP ni dhaifu mara tano zaidi ya Windows 7 na 8, kwa hiyo Microsoft wameona ni bora wakaitoa sokoni. Kwa maana hiyo ATM na kompyuta zote zinazotumia programu hizo hazitakuwa na ulinzi wa uhakika,” alisema Urassa ambaye ni mtaalamu wa masuala ya Teknolojia ya Mawasiliano (IT).
Alisema kuwa kuna idadi kubwa sana ya Watanzania wanaoendelea kutumia bidhaa hizo zikiwemo taasisi kubwa nchini hivyo kuna haja kubwa ya kuchukua hatua za kubadilika na teknolojia.
Naye, Ofisa Uhusiano wa Benki ya Posta, Noves Moses aliwatoa wasiwasi wateja wake kuwa licha ya kusitishwa kwa matumizi ya Windows XP, bado benki hiyo itaendelea kutoa huduma zenye kiwango kile kile.

 

Magaidi waua watu 6 Kenya 

Watu sita wameuawa na wengine 25 kujeruhiwa vibaya katika shambulizi la kigaidi katika eneo la California mtaa wa Eastleigh, viungani mwa mji wa Nairobi.

Waathiriwa wa shambulizi wakipelekwa hospitalini 

Kamanda wa Polisi mjini Nairobi Benson Kibue amesema kuwa milipuko miwili ilitokea wakati magaidi waliporusha vilipuzi katika mikahawa miwili midogo.
Mlipuko wa tatu ulitokea katika kituo cha mabasi ya uchukuzi kilichoko karibu na zahanati za afya ya mama na mtoto.
Miongoni mwa waliojeruhiwa walikuwa ni wanawake waliokuwa wanauza mboga na bidhaa zingine za rejareja.
Kwa mujibu wa polisi wale waliouawa walikuwa wamekwama ndani ya mkahawa huo baada ya mlango kufungwa kutoka nje na washambulizi waliorusha bomu ndani .
Waathiriwa walikuwa wameenda kununua chakula cha jioni.
Idadi kubwa ya wakimbizi wa kisomali wanaishi katika mtaa wa Eastleigh.
Inaarifiwa washambuliaji walitumia maguruneti au mabomu ya kutengezwa nyumbani kufanya mashambulizi hayo
Mashambulizi haya yanawadia siku moja tu baada ya mtu anayeshukiwa kuwa gaidi kufa kilipuzi alichokuwa akikiunganisha kilipolipuka .
Isitoshe wakenya bado wanaomboleza vifo vya waumini 6 waliouawa katika kanisa moja mjini likoni Mombasa majuma mawili yaliyopita.
Mtaa wa Eastleigh unafahamika kama ''Mogadishu ndogo'' kutokana na idadi kubwa ya wasomali wanoishi hapo wengi wakiwa ni wakimbizi.
Mtaa huu ambao ni kitovu cha biashara umepigwa darubini na serikali ya Kenya haswa baada ya visa vingi vya ugaidi kuhusishwa na kundi la wapiganaji wa kiisalmu la Al Shaabab ambao wamepinga vikali kuweko kwa majeshi ya Kenya nchini Somalia kama sehemu ya AMISOM.

Kesi dhidi ya Rais Kenyatta yaahirishwa

Rais Uhuru Kenyatta 

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imehairisha kesi dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta hadi tarehe saba Oktoba mwaka huu.
Rais Kenyatta anatuhumiwa kwa makosa ya jinai kufuatia machafuko ya baada ya uchaguzi wa mkwaka 2007 - 2008, madai ambayo ameyakanusha.
Mahakama kuu ya ICC, kupitia mwendesha mashitaka Fatou Bensouda, imekuwa ikiitaka serikali ya Kenya kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuendesha kesi zinazowakabili Rais Kenyatta na naibu wake bwana Ruto.
Hii ni mojawapo ya sababu kuu ya kubadili tarehe ya kusikizwa kwa kesi hii.
Upande wa mashitaka umesema kuwa unaipa Kenya muda wa ziada ili kutafuta na kuwasilisha baadhi ya stakabadhi za benki zinazohitajika katika kesi hiyo.
Kumekuwa na malalamishi kutoka kwa upande wa mashitaka kuwa serikali ya Kenya inalenga kuzuia stakabadhi hizo kufikishwa mahakamani jambo ambalo mawakili wa bwana Kenyatta wamekanusha.
Miongoni mwa yale yanayohitajika kotini ni pamoja na taarifa ya maelezo ya fedha anazomiliki bwana Kenyatta.
Kesi hii imekumbwa na matatizo ya mashahidi kujiondoa na shutuma za mahakama hii kuonea viongozi wa bara Afrika.

 

 

 

Thursday 27 March 2014

ANGALIA PICHA ZA KUTISHA WATU WANAVYOJICHUKULIA SHERIA MKONONI


 KUMRADH kwa picha mbaya na za kutisha.Tunaungana na Jeshi la Polisi nchini kupinga unyama huu wanaofanyiwa binadamu wenzetu licha ya kwamba wanakuwa waharifu hii ni kosa kisheria.


I

Bei ya gesi kupanda maradufu Ukraine

Serikali ya mpito ya Ukraine imesema itaongeza bei ya gesi kwa watumiaji wa ndani kwa asilimia 50 zikiwa jitihada za kuhakikisha kuwa wanafanikiwa kupata mkopo kutoka Shirika la fedha duniani, IMF

 

Shirika la taifa la nishati ya gesi, Naftogas limetangaza nyongeza ya gharama hizo kuanza kutekelezwa tarehe mosi mwezi Mei.
Ukraine hununua gesi nusu ya gesi yake ya asili kutoka kampuni ya Gazprom ya Urusi, kisha huiuza kwa watumiaji wake kwa gharama nafuu.
IMF halikadhalika inaitaka Ukraine kupambana na vitendo vya rushwa na kusitisha mchakato wa Benki kuu ya Ukraine kusaidia fedha ya nchi hiyo.
Siku ya jumanne, waziri wa fedha wa nchi hiyo Olexander Shlapak alisema Ukraine inahitaji kiasi cha Pauni bilioni 9-12 kutoka kwa IMF.
Jarida la Financial Times limeripoti kuwa uamuzi uko mbioni kufikiwa kuhusu kiasi cha fedha cha takriban dola za kimarekani bilioni 15
ambacho Ukraine inatakiwa kujiokoa na kwamba maamuzi hayo yatatangazwa rasmi Alhamisi.
Makubaliano kati ya Ukraine na IMF ni muhimu wakati huu ili kuweza kupata misaada zaidi kutoka kwa Jumuia ya Ulaya na Marekani.
Msaada wa kifedha unahitajika haraka wakati nchi hiyo ikiwa imelazimika kutumia hifadhi ya fedha za kigeni,huku uchumi nao ukitarajiwa kuanguka kwa 3% mwaka huu.
Wizara ya fedha nchini humo pia inatarajia msaada kutoka kwa Marekani japo kiasi kamili kinasubiri mjadala na bunge la Congress.

 

Rais Uhuru na naibu wake walipoamua kusimamisha msafara ili kula.

 Screen Shot 2014-03-27 at 12.06.56 PM 

Ni picha ambayo nimetumiwa na Mwandishi wa habari wa Kenya ikimuonyesha Uhuru Kenyatta ambae ni Rais wa nchi hiyo akiwa na naibu wake William Ruto baada ya kuamua kusimama njiani wakitokea Arusha kwa gari na kula chakula chini ya mti Kajiado.

Rais Uhuru ameripotiwa kufanya mambo kadhaa ambayo hayajawahi kufanywa na Marais wengine wa nchi hiyo likiwemo la kutembea Nairobi bila msafara ambapo hivi juzi kuna video ilitoka ikidaiwa kumuonyesha Rais huyo akinunua karanga kutoka kwa watoto barabarani Nairobi.
Hii picha ya leo hapo juu inadaiwa ni msafara wake uliosimama na kula chakula wakati akitokea Arusha Tanzania kwenye mkutano ambapo alitumia usafiri wa gharama nafuu (gari) na kuendeshwa kutoka Nairobi, siku kadhaa tu baada ya nchi hiyo kutangaza kuvunja safari za nje ya nchi za viongozi wa serikali zisizo za lazima ili kuokoa matumizi makubwa ya fedha.
Ni siku kadhaa pia baada ya Rais huyu kutangaza maamuzi ya kupunguza mshahara wake, naibu wake, Mawaziri na hata wakuu wa mashirika ya umma nchini humo.
Screen Shot 2014-03-27 at 12.52.17 PM

 

Tazama jinsi fundi alivyookolewa dakika za mwisho kwenye jengo lililowaka moto

Screen Shot 2014-03-27 at 12.14.25 PM 

Ni moto ambao umetokea kwenye gorofa ya tano ya jengo moja huko Houston Texas Marekani ambapo kikosi cha zimamoto kilifanya pia jitihada za kumuokoa fundi ujenzi mmoja aliekua kwenye gorofa hilo dakika za mwisho wakati moto umeshashika.

Screen Shot 2014-03-27 at 12.14.39 PM

 

Kuna njama kuvuruga Bunge

a Uvumilivu una mwisho wake, ukifika wakati huo tutawaambia Watanzania nini kinachoendelea na sisi tunakusudia kufanya kitu gani.

Dodoma/Dar. Kuna njama. Maneno haya mawili ndiyo yametumiwa na pande mbili zinazopingana ndani ya Bunge Maalumu la Katiba, kuelezea hali iliyojitokeza jana wakati wa kikao cha Bunge hilo kuhusu mvutano wa mabadiliko ya kanuni.
Njama zinazoelezwa na pande hizo ni za kuvuruga mchakato wa Katiba Mpya, zikirejea yaliyotokea jana jioni ikiwamo zomeazomea hali iliyomlazimu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta kuliahirisha Bunge hadi leo jioni.
Baada ya kuahirisha Bunge hilo, Sitta alikutana na waandishi wa habari na kusema kwamba kuna njama za baadhi ya wanasiasa kutumia vurugu kuhujumu mchakato wa upatikanaji wa Katiba, badala ya kujenga hoja.
Bila kuwataja wanasiasa hao, Sitta alisema ikiwa hawataki kuendelea na mchakato huo, basi waondoke na kuwaacha wenye nia njema.
“Wanasiasa hawa wamedhamiria kuvuruga mchakato wa Katiba, tuhuma ambazo tumetuhumiwa leo na Lissu (Tundu) ni uongo na uzushi, mimi sihusiki na kupeleka marekebisho ya kanuni kwenye Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge,” alisema Sitta.
Sitta alikuwa anajibu mchango wa mjumbe wa Bunge, Tundu Lissu alioutoa mapema kwenye kikao cha jioni, akipinga kilichoelezwa ni njama za kutaka kubadili kanuni kinyemela ili kumsaidia mwenyekiti kulidhibiti Bunge.
Sitta alisema kwa kuzingatia kanuni ya 59 (1), Kamati ya Uongozi ina mamlaka ya kupeleka marekebisho ya kanuni ili kuliwezesha Bunge kufanya kazi vizuri.
Alisema hoja kwamba haiwezekani kufanyika mabadiliko hata kabla ya kuanza kutumika kanuni, siyo ya msingi kwani kila kitu kinabadilika kutokana na mazingira yake.
“Kamati ya Uongozi ndiyo ilipeleka waraka wa mabadiliko ya kanuni kwa Kamati ya Kanuni na Haki kwa kuzingatia kanuni, lakini hata kabla ya kujadiliwa na kamati husika inaonekana kuna wajumbe ndiyo wameichukua na kuifikisha bungeni,” alisema Sitta.
Alisema kwa kiasi kikubwa marekebisho ambayo yangesomwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Pandu Ameir Kificho, yalilenga kutoa ufumbuzi wa kanuni ya 37 na 38 juu ya upigaji kura ama uwe wa wazi au siri.
Sitta alisema pamoja na hilo, kulikuwa na marekebisho ya msingi kama kuweka utaratibu mzuri wa majadiliano katika kamati pia kuweka utaratibu wa vikao vya Bunge kuanzia Jumatatu hadi Jumapili.
“Mengi ambayo alikuwa anayasema Lissu kama ni takataka hayakuwapo katika taarifa ya Kificho,” alisema Sitta.

 

 

Rais akistaafu afutiwe kinga’

 

Dar es Salaam. Wakati Bunge la Katiba likiwa bado halijaanza kujadili Rasimu ya Katiba, taasisi moja ya viongozi wa dini imetoa maoni mapya ikitaka Rais wa nchi awe tu na kinga anapokuwa madarakani, akiondoka awajibike kwa matendo yake.
Mapendekezo hayo yalitolewa Dar es Salaam jana na Baraza la Wadhamini la Taasisi ya Viongozi wa Dini Tanzania (IRCPT), lilipokutana kwa ajili ya kutafakari kwa pamoja juu ya mchakato wa Katiba Mpya.
Mkutano wa Baraza hilo linalojumuisha Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Titus Mdoe, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Musa Salum na Padri John Solomon, uliongozwa na kaulimbiu ya ‘Katiba Moja Kwa Watanzania Wote, Pamoja Tutafika’.
Mwenyekiti wa IRCPT, Jaji Mstaafu Raymond Mwaikasu alisema tafakari inahitajika kuhusu kinga ya Rais na kwamba wao wanapendekeza awe nayo anapokuwa madarakani, lakini kinga hiyo iondolewe anapoachia madaraka, ili awajibishwe pale alipokosea.
Jaji Mwaikasu alisema pamoja na kwamba waliwasilisha maoni kwa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, hatua ya sasa inawalenga watu wenye lengo la kuingia Ikulu wakiwa na mawazo ya kujinufaisha wao, ndugu, jamaa na marafiki zao badala ya kuwatumikia wananchi.
“Hili linapaswa kutazamwa kwenye Katiba yetu mpya na sisi hatutakuwa wa kwanza kufanya hivyo, ila itasaidia kuwafanya viongozi kufuata maadili na iwapo itatokea Rais kuvunja Katiba, apelekwe mahakamani na akikutwa na hatia, awajibike hata kwa kujiuzulu,” alisema Jaji Mwaikasu. Naye Sheikh Salum alisema mali zote ni miliki ya Mungu, hivyo zinapaswa kugawanywa kwa usawa na ikitokea mtu akajimilikisha ni jambo lisilokubalika, hivyo ziwepo sheria za kuwabana viongozi wa aina hiyo.
Askofu Mdoe alisema Rasimu ya Katiba ni nzuri ingawa hakuna kitu kinachokamilika kwa asilimia 100, hivyo mazuri yaboreshwe, upungufu usahihishwe na yaliyokosekana yapatiwe fursa.
Alisema malumbano yanayoendelea kwenye Bunge la Katiba hayana tija kwani yana mwelekeo wa masilahi ya kisiasa badala ya masilahi ya umma.
“Wamebadilisha hali waliyotakiwa kuwa nayo, wanarudi katika makundi hasa ya kisiasa na mijadala kuwa ya kichama zaidi, wakifika bungeni wawe wazalendo wajadili na kuacha ushabiki,” alisema Askofu Mdoe.
Muundo wa Muungano
Kuhusu mjadala wa serikali mbili au tatu, Jaji Mwaikasu alisema hauna tija isipokuwa jambo muhimu ni kujenga msingi imara wa kuheshimiwa kwa Katiba itakayopitishwa. “Tunaambiwa Katiba imevunjwa, tunafanya nini? muhimu ni kuangalia viongozi wanaohusika wanadhibitiwa vipi, vinginevyo itakuwa ni bure,” alisema.
Alibainisha kuwa tatizo Bunge la Jamhuri ya Muungano limelala na walioteuliwa kutetea wanatetea mikate yao, hivyo akapendekeza kuwapo haja ya wananchi nao kupewa meno ya kuhakikisha Katiba inalindwa, ili pale itakapothibitika Rais amevunja Katiba wachukue hatua.

 

Seif: Hatuko tayari kujadili serikali mbili

Zanzibar. Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake cha CUF hakiko tayari kujadili mfumo wa Muungano wa serikali mbili kama inavyotetewa na wabunge wa CCM na Rais Jakaya Kikwete.
Amesema tayari amewaandikia barua Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwaeleza juu ya msimamo huo.
Maalim Seif alitoa msimamo huo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.
Isitoshe, alisema CUF imebaini kuwa kuna njama za kufuta kipengele katika Katiba ya Zanzibar kinachosema; “Zanzibar ni nchi” na kwamba hiyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa kuwa Wazanzibari kamwe hawatakubali kufanya hivyo.
Maalim Seif alisema haikuwa mwafaka kwa Rais Kikwete kukosoa mapendekezo ya Rasimu ya Katiba yanayotaka mfumo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.
Alisema Jaji Warioba aliweka kando itikadi yake ya CCM katika utendaji wake kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuja na uamuzi huo kwa vile ndiyo tiba ya kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Mapendekezo yaliyowasilishwa na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya wananchi, Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili kujenga mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali tatu,” alisema Maalim Seif.
Alisema Muungano wa serikali mbili hauvumiliki na kama kuna watu wanaendelea kuutetea mfumo huo, Zanzibar inaweza kutumia sheria yake ya kura ya maoni kuwauliza wananchi wanaotaka na wasiotaka jambo hilo.
“Nimemwandikia barua Rais Kikwete, nakala nimempelekea Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, Tanzania Bara wanataka Zanzibar iondoe kifungu cha Katiba kinachosema Zanzibar ni nchi, jambo hilo halitapita...tutafanya kampeni wananchi walikatae,” alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Alisema ni jambo la kusikitisha katika hotuba yake alijisahau kama ni mkuu wa nchi na analihutubia Bunge Maalumu badala yake akaegemea kuwa mwenyekiti wa CCM.
Alisema haikuwa sahihi kutoa vitisho na kutaja ikiwa Serikali ya Muungano chini ya Serikali tatu italegalega, jeshi litachukua madaraka ya nchi.
“Rafiki na ndugu yangu Kikwete, usifikiri huu ni wakati ule wa Julius Nyerere, akisema yeye hakuna wa kumpinga. Mambo yamebadilika, usijifanye ni Nyerere mpya, hakuna atakayekusikiliza na kubabaika,” alisisitiza Maalim Seif.

Rwanda na A.Kusini kusuluhisha mgogoro

Rais Jacob Zuma wa Afrika-Kusini na Paul Kagame wa Rwanda wamekubaliana mjini Luanda Angola, kuanzisha mazungumzo ya pamoja ya kumaliza mzozo wao wa kidiplomasia

Jaribio la kumuua Kayumba Nyamwasa lilitibuka Afrika Kusini
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulianza kuzorota pale Rwanda ilipowafukuza maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini, saa chache baada ya Afrika Kusini kuwatimua wanadiplomasia watatu wa Rwanda kuondoka nchini humo karibu wiki tatu zilizopita.
Afrika Kusini ilichukua hatua hiyo baada ya nyumba ya mpinzani mmoja wa Rwanda anayeishi Afrika Kusini Kayumba Nyamwasa kushambiliwa.
Lakini Serikali ya Rwanda ilisema hatua ya kuwatimua maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini mjini Kigali ni ya haki na ilizingatia uchokozi ambao ulianzishwa na serikali ya Afrika Kusini yenyewe kwa kufukuza maafisa watatu wa ubalozi wa Rwanda.
Rwanda ilisema kuwa Afrika Kusini ndio ilianza uchokozi kwa kuwatimua mabalozi wake watatu 

Jenerali Kayumba Nyamwasa, ambaye aliwahi kuwa mkuu wa majeshi nchini Rwanda, hakuwa nyumbani wakati wa shambulio hilo.
Nyumba yake iliharibiwa huku komputa na baadhi ya nyaraka zilichukuliwa.
Mkutano wa usalama uliofanyika mjini Luanda ulijadili hali kati ya nchi hizo mbili huku viongozi hao wawili wakikikutana ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mzozo huo kutokea.
Rais Zuma alisema kuwa wamekubaliana kusuluhisha mgogoro huo na pia kupata taarifa ya pamoja ili kuweza kusuluhisha tofauti kati yao.
Kadhalika Rais Zuma aliongeza kwamba serikali yake inatekeleza wajibu wake wa kimataifa kwa kuwapa hifadhi watu wanaoomba. Viongozi hao wawili wamekubaliana kukutana kwa ajili ya kuzungumzia swala hilo baadaye.

Obama kukutana na Papa Francis


Obama Kukutana na Papa Francis

Rais Barrack Obama wa Marekani anatarajiwa kukutana na kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, katika makao yake makuu huko Vatican.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Obama kukutana na papa Francis.
Wawili hao wanatarajiwa kujadili namna ya kupunguza tofauti iliyopo kati yao katika maswala mengi mbali na kujaribu kuinua maisha ya watu maskini duniani baada ya takwimu kuonyesha kuwa tofauti ya mapato kati ya matajiri na Masiki inaendelea kupanuka .
Aidha viongozi hao wawili wanatazamiwa kujadili hali ilivyo Nchini Ukraine, na swala la upatikanaji wa amani mashariki ya kati.
Mwafaka baina ya mitazamo tata kuhusiana na maswala ya uavyaji mimba, matumizi ya dawa za kupanga uzazi na ndoa ya jinsia moja pia inatarajiwa kuwa kati ya mada itakayojadiliwa .

 

Mkuu wa Jeshi kugombea Urais Misri

 Mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi Misri, Abdul Fattah al-Sisi, ametangaza kujiuzulu jeshini ili kugombea katika uchaguzi wa urais mwezi ujao.Wagombea wote wanapaswa kuwa raia.

Akizungumza Kwenye hotuba ya Televisheni huku akiwa amevalia sare ya kijeshi Abdel Fattah El Sissi amesema yeye sio mwanajeshi tena baada ya miaka 44 na kwamba amechukua hatua hiyo ili aweze kutimiza jukumu lingine muhimu.
Ni Bayana kwana Sisi hatakua na kibarua kigumu kujipatia ushindi katika uchaguzi wa Urais. Anaungwa mkono na idadi kubwa ya raia wa Misri na hadi sasa hana wapinzani wowote.
Baadhi ya waliotaka kugombea urais wamejiondoa wakidai kwamba hawataweza kuendesha kampeni zao kwa njia huru.
Wafuasi wake Sisi wanamuona kama kiongozi imara ambaye anaweza kurejesha amani na udhabiti nchini Misri baada ya miaka mingi ya machafuko.
Wakosoaji wake wanasema ana msimamo mkali na amechangia pakubwa katika kusambaratisha na kuhujumu upinzani nchini Misri.
Mkuu huyo wa jeshi atakabiliwa na majukumu mazito ya kufufua uchumi uliofifia , kupambana na uasi na kuileta pamoja nchi iliyogawanyika. Ameahidi kutekeleza mabadiliko makubwa lakini akaonya kuwa hawezi kufanya miujiza.

Tuesday 25 March 2014

Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Home » General News » Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Kuhusu shambulizi la Kanisa Mombasa na mtoto ambae mpaka sasa ana risasi kichwani

Screen Shot 2014-03-25 at 8.53.23 AM
Idadi ya waliofariki kutokana na shambulizi la Kanisa Mombasa Kenya March 23 2014 imefikia sita ambapo wote hao vifo vyao vimetokana na majereha ya risasi huku wengine tisa waliokua wakipata matibabu hospitali wakiruhusiwa kwenda nyumbani.
Mkuu wa Polisi Kenya amesema bado hawajafutilia mbali kwamba lilikua shambulio la kigaidi ambapo kwa mujibu wa Erick Ponda ambae ni mwandishi wa habari wa DW Mombasa alieongea na millardayo.com akisema mpaka March 24 2014 jioni watu 59 walikua wamekamatwa na Polisi kwenye msako wakituhumiwa kuhusika na shambulio hilo.
Wakati huohuo, mtoto ambae bado kichwani kwake kuna risasi aliyopigwa kwenye shambulio hilo amepelekwa kwenye hospitali ya binafsi kwa matibabu maalum kwa sababu anahitaji kufanyiwa upasuaji ili kuokoa maisha yake.
Mama mzazi wa mtoto huyu alifariki kwenye hili shambulio hivyo kwa sasa mtoto yuko na ndugu wa mama yake ambae namkariri akisema ‘haendelei vizuri manake amekua akinisumbua hawezi kulala, ana maumivu makali sana kichwani kutokana na hiyo risasi ndani ya kichwa’
Viongozi wa kidini wakiongozwa na Askofu Julius Atsango wamewataka wenzao wa dini ya kiislamu kuisaidia serikali kuwakamata wanaosingizia dini kutekeleza mashambulizi

 

Monday 24 March 2014

Zanzibar yashauriwa kurekebisha Katiba

 

 Alisema wakati Katiba ya Zanzibar ikieleza hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sura ya 1 inaelezaa kuwa Tanzania ni nchi moja na eneo lake la mipaka ni kuanzia Tanzania Bara hadi Visiwani

Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeshauriwa kufanya marekebisho ya Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu Mwaka 2015 ili kuondoa vifungu vinavyogongana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ushauri huo umetolewa na mwanasiasa mkongwe wa Zanzibar, Ali Hassan Khamis wakati akiwasilisha mada juu ya hali ya kisiasa na mchakato wa Katiba ya Muungano katika kongamano lililoandaliwa na Jumuiya za CCM, lililofanyika kwenye Ukumbi wa Tawi la Kiembesamaki Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Alisema migongano inayojitokeza katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imetokana na marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 iliyogongana na Katiba ya Muungano na kusababisha mjadala mkubwa katika mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea.
Alisema marekebisho hayo ya Katiba ya Zanzibar yameongeza migongano hasa sura ya 1(1) inayoeleza kuwa Zanzibar ni nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vilivyozungukwa na bahari yake, ambayo kabla ya Muungano wa Tangayika na Zanzibar ilikuwa ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Alisema wakati Katiba ya Zanzibar ikieleza hivyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sura ya 1 inaelezaa kuwa Tanzania ni nchi moja na eneo lake la mipaka ni kuanzia Tanzania Bara hadi Visiwani.
Aliwaeleza washiriki hao kuwa kifungu cha 2(a) cha Katiba ya Zanzibar kimempa uwezo Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar katika mikoa na wilaya kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
Alisema marekebisho hayo ya 10 yamechangia kwa kiwango kikubwa kuibua migogoro ndani ya Muungano na kutaka Katiba ya Zanzibar iandikwe upya na wananchi wapewe nafasi ya kuijadili na kuamua.
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Vilevile alieleza katika marekebisho hayo ya 10 kuna vitu viliondolewa lakini havikuwa na ulazima kama wakuu wa mikoa kuwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi (BLW), wakati ni watendaji wakuu wa shughuli za Serikali katika kuwahudumia wananchi kwenye maeneo yao.
“Wakati umefika katiba yetu ya Zanzibar iangaliwe upya iendane na Katiba ya Jamhuri ya Muungano vinginevyo tutaendelea kuendeleza migogoro na kuathiri msingi mzima wa Muungano na Mapinduzi ya Zanzibar,” alisema Ali Hassan Mkuu wa Wilaya ya Kati wa zamani visiwani humo.
Akifafanua zaidi alisema hata muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), una kasoro Zanzibar kutokana na sera ya CCM kuwa ni moja kati ya Zanzibar na Tanzania Bara lakini mfumo huo wa Serikali umezingatiwa upande marekebisho hayo ya kati mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Chama chetu ni kimoja, ni sehemu gani sera yetu imesema CCM ikishinda itaunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa wakati hilo Tanzania Bara halipo,” alisema.

 

Ikulu: Kujadili hotuba ya JK kupoteza muda

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salva Rweyemamu

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salva Rweyemamu amesema kuendelea kuijadili hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyotoa kwenye Bunge la Katiba mwishoni mwa wiki ni kupoteza muda.
Akizungumza na gazeti hili jana, Rweyemamu aliushangaa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuendelea kutoa matamko yanayoipinga hotuba hiyo, akisema haumtendei haki mkuu huyo wa nchi na Watanzania wote kwa ujumla. Alisema kama Mtanzania, Rais alitoa maoni yake na amekuwa muungwana kwa kuwaambia kwamba bado wana fursa ya kujadili na kuleta mapendekezo yao, lakini wajali zaidi masilahi ya taifa.
“Hiyo ni propaganda isiyokuwa na maana kwa taifa na hata hatima ya Katiba yenyewe. Ningependa kuwakumbusha kwamba Watanzania wamewapeleka Dodoma wakajadili Katiba na siyo kufanya propaganda, tunawataka wafanye kazi,” alisema Rweyemamu.
Kwa mujibu wa Rweyemamu, umoja huo wenye viongozi kutoka vyama vya upinzani haumtendei haki Rais kwani kama Mtanzania, mkuu huyo wa nchi ana fursa ya kutoa maoni yake.
“Wasifikiri kwa kumjibu hivyo Rais wanajibizana na CCM. Rais ni mkuu wa nchi ana maoni yake, lakini zaidi ya yote, Bunge la Katiba siyo mahali pa kufanya siasa. Kama wanataka siasa tunawaomba warudi maofisini mwao wakafanye siasa, pale tumewatuma kazi,” alisisitiza.
Rweyemamu alibainisha kuwa mchakato wa kutunga Katiba unahitaji busara na busara hiyo haiwezi kupatikana kama watu waliotumwa kuwawakilisha wananchi wameamua kufanya siasa.
“Tunahitaji watu wote wawe CCM, CUF, Chadema na vyama vingine waache siasa,” alisema.
Wakati huohuo, bungeni Dodoma limeibuka kundi la wajumbe, wengi wao kutoka CCM wakiipongeza hotuba hiyo ya Rais Jakaya Kikwete na kuwakosoa watu wanaotishia kumpeleka Rais mahakamani kwa madai ya kuvunja kanuni na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuingilia mchakato wa maoni.
Mjumbe wa kundi hilo linalojiita Tanzania Kwanza, Evod Mmanda alisema siyo kweli kuwa Rais amevunja sheria kwani alihutubia Bunge baada ya kupitishwa kwenye kanuni za Bunge kifungu cha 75(1) ambacho kinaeleza mwenyekiti anaweza kumwalika mgeni rasmi kulihutubia Bunge.
Walioambatana na Mmanda ni Dk Emmanuel Nchimbi, Said Nkumba, Mohamed Thabit Kombo, Waride Jabu, Seleman Jafo na Charles Mwijage.

Bunge la Katiba Njiapanda

“Kama tunataka serikali ya tatu lazima tuitengenezee misingi ya uhakika na kuhoji nani atayeidhamini serikali ya tatu virungu, pingu, magari ya kuwasha, majeshi au bunduki.”
Dar es Salaam. Kwa neno moja unaweza kusema kwamba wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na wananchi kwa ujumla wako “njiapanda”.
Hii ni baada ya hotuba ya ufunguzi wa Bunge hilo iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete kuibua mambo mazito ambayo kimsingi yanatofautiana na mapendekezo yaliyomo katika Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Huku wananchi wakijiuliza nini hatima ya Bunge hilo baada ya hotuba hiyo, baadhi ya wajumbe ambao wiki hii ndiyo wanaanza kujadili rasimu hiyo, watakuwa katika wakati mgumu wa kuamua wafuate maoni ya nani, kati ya viongozi hao wawili.
Ingawa Rais Kikwete amesema mara kadhaa kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba ndiyo waamuzi. Mambo mengi aliyoibua yanaonyesha kutokubaliana kwake na baadhi ya maoni ya wananchi yaliyomo katika rasimu, ambayo Jaji Warioba amewahi kusema kuwa yanatakiwa kuheshimiwa.
Wakizungumzia tofauti hizo, mjumbe wa Bunge la Katiba, Ezekiah Oluoch alisema kauli za Rais Kikwete na Jaji Warioba zimezidi kuwagawa wajumbe wa Bunge hilo kwa maelezo kuwa tangu awali wajumbe hao walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili; ya wanaotaka muundo wa Muungano uwe wa serikali tatu na wale wanaotaka serikali mbili.
Alisema kama suala la muundo wa Serikali likishindikana kupatiwa mwafaka ni vyema likarudishwa kwa wananchi ili wapige kura ya maoni kuchagua aina wanayoitaka, kisha suala hilo lirejeshwe tena katika Bunge la Katiba kwa ajili ya kuboreshwa.
“Rais alipoanza kuzungumza alikuwa kama mkuu wa nchi lakini mwisho wa hotuba yake aligeuka kuwa mwenyekiti wa CCM. Kifupi alichokizungumza kimekwenda tofauti na wadhifa wake,” alisema.
Naye Deo Filikunjombe alisema: “Nadhani kwa hotuba hizi mbili, kazi ya wajumbe wa Bunge la Katiba itakuwa rahisi. Maana sasa wameshajua uzuri na ubaya wa serikali tatu na mbili.
“Hata kama kutakuwa na tofauti, wananchi ndiyo watakuwa wa mwisho kuamua kama Katiba hii ipite au isipite. Tunachotakiwa wajumbe ni kuwa makini na uamuzi wetu.”
Naye Yusuf Manyanga alisema: “Bunge la Katiba limejaa watu wenye busara. Sidhani kama tutashindwa kuelewana maana hata katika biashara ya utumbo inzi ni wengi lakini utumbo unauzika.”
Katika hotuba yake aliyoitoa Ijumaa iliyopita Rais Kikwete aligusia mambo saba ya msingi yaliyomo katika rasimu ya Katiba na kutaka yatazamwe kwa kina, huku akibainisha kuwa mengine hayawezekani kutekelezeka.

 

Sitta ‘amkataa’ Warioba bungeni

Mwenyekiti wa Bunge maalumu la katiba, Samuel Sitta 

Dodoma. Jaribio la kutaka kumrejesha bungeni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba ili ajibu masuala yaliyoibuliwa na Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake ya kufungua Bunge limegonga mwamba.
Uamuzi wa kukataa ombi hilo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta wakati akijibu mwongozo ulioombwa na Mjumbe wa Bunge, Julius Mtatiro, akisema hadhani kama ni sahihi ombi hilo kutekelezwa.
Awali Mtatiro aliomba mwongozo kwa mwenyekiti, akitaka kujua iwapo kuna haja ya kumrejesha Jaji Warioba kutoa ufafanuzi juu ya baadhi ya hoja za Rais Kikwete ambazo zimekinzana na maoni ya wananchi yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba.
Mtatiro alisema: “Mtoa hoja mahususi alikuwa ni Jaji Warioba na Rais Kikwete alialikwa kama mgeni rasmi kufungua Bunge, lakini badala yake alikuja kujibu hotuba ya Warioba.
“Kwa sababu Rais alikaribishwa kama mgeni rasmi, lakini  alijibu  hoja za Warioba, je, hatuoni kama kuna haja ya kumrejesha mtoa hoja mahususi aje kujenga hoja  kutokana na alichosema Rais Kikwete?” alihoji Mtatiro ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF.
Katika ufafanuzi wake, Sitta alisema tayari amepokea kwa maandishi kutoka kwa baadhi ya wajumbe kuzungumzia suala hilo, jambo ambalo litafanyika lakini si kwa kumwita tena Jaji Warioba. Tunapenda kupata muda wa kuzungumzia  suala hili ili kuliweka sawa, hotuba zote mbili ambazo ni muhimu zitaandaliwa ili kupitiwa kuona kama malalamiko yanayotolewa yana hoja,” alisema Sitta.
Tangu Rais Kikwete ahutubie Bunge Ijumaa na kutoa hoja kinyume na mapendekezo ya Rasimu ya Katiba, hasa muundo wa Muungano, kumeibuka mijadala ya ama kuipinga au kuiunga mkono, huku wengine wakieleza kuwa imekiuka sheria.

 

 

 

Marekani kusaidia UG kupambana na Kony


Kiongozi wa waasi wa LRA Joseph Kony

 Serikali ya Marekani inatuma ndege ya kivita na kikosii maalum cha jeshi kusaidia Uganda katika juhudi za kumsaka kiongozi wa kundi la waasi la Lord's Resistance Army, Joseph Kony.Msemaji wa baraza la usalama la Marekani, Caitlin Hayden, amesema kuwa wanajeshi wa Afrika wataendelea kuongoza operesheni hiyo, ingawa watapata ushauri kutoka kwa vikosi vya Marekani.Alisema kuwa ndege hiyo itawekwa nchini Uganda ingawa itatumika katika nchi zingine ambako waasi wa LRA wamekuwa wakijificha.Marekani ilituma vikosi vyake mara ya kwanza nchini Uganda mwaka 2011 kusaidia Uganda katika harakati za kumtafuta Joseph Kony.

 

529 wahukumiwa kifo Misri

Mahakama nchini Misri imewahukumu kifo watu 529 ambao wanasemekana kuwa wafuasi wa Rais aliyeng'olewa mamlakani Mohammed Morsi.
Watu hao walikabiliwa ma mashitika mbali mbali yakiwemo mauaji ya polisi na kuwavamia polisi.
Wafuasi hao wa chama kilichopigwa marufuku, cha Muslim Brotherhood, ni sehemu ya kundi lengine kubwa la watu zaidi ya 1,200 wanaoaminika kuwa wafuasi wa Morsi.
Maafisa wa utawala nchini Misri wamekuwa wakiendesha msako mkubwa dhidi ya wafuasi wa vuguvugu hilo, tangu Morsi kuondolewa mamlakani mwezi Julai mwaka jana.
Maelfu wamekamatwa huku mamia wakiuawa.
Mahakama hiyo ilitoa hukumu baada ya vikao viwili pekee ambapo mawakili wa watuhumiwa walilalamika kuwa hawakupewa muda wa kuwasilisha kesi yao vyema.
Mauaji wanayodaiwa kufanywa na watuhumiwa yalitokea Kusini mwa Misri, mwezi Agosti, baada ya vikosi vya usalama kuvunja kambi mbili za wafuasi wa Morsi waliokuwa wanataka arejeshwe mamlakani

 

Makahaba watumia Vibaya Hijab Kenya

Makahaba katika baadhi ya sehemu za mji mkuu wa Kenya , Nairobi, wametupilia Mbali vazi la 'Mini skirt na kuanza kutumia Hijab kama njia ya kuwavutia wateja wao, jambo ambalo limekashifiwa vikali na wakuu wa dini ya Kiislamu.
Hijab huvaliwa na wanawake wa Kiislamu kama ishara ya kumcha Mungu, lakini makahaba katika mtaa wa Eastleigh, viungani mwa Nairobi wanatumia Hijab ili kuwafanya wateja wao kudhania kua wanatoka sehemu za Pwani.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa shirika la habari la Nation mjini Nairobi.
Mwanamke mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake alisema kuwa yeye hupata wateja maradufu kwani huvalia vazi hilo la Hijab, wengi wa wateja wake wakimuona kama mwenye nidhamu.
Uchunguzi ulibaini kuwa wanawake wasio wa kiislamu wanavalia vazi hilo ili kuwavutia wanaume ambao wanaamini kuwa wao wana maadili zaidi ya wale wanaovalia nguo fupi au 'Mini Skirt'.
Nguo fupi ni mavazi yaliyozoeleka kwa makahaba sehemu nyingi duniani
Taarifa hiyo imemnukuu Imam mkuu wa msikiti wa Jamia mjini Nairobi, Mohamed Swalihu akisema kuwa ni jambo la kusikitisha sana kuwa Hijab inatumika kwa njia isiyopaswa na makahaba huku akiongeza kuwa pia wanaume wanalitumia vazi hilo kuendesha shughuli za uhalifu jambo ambalo amelitaja kuwa la kishetani linalostahili kukashifiwa vikali.
Hata hivyo chama cha makahaba nchini Kenya kimewatetea makahaba hao wanaotumia hijab huku likidai kwamba wanafanya hivyo ili kukidhi mahitaji ya wateja wao.
Mratibu wa muungano huo, Bi Phelister Abdalla, aliiomba serikali kuhalalisha ukahaba kwa madai ya viwango vya juu vya ukosefu wa ajira.
Mahojiano na makahaba katika mtaa wa Eastleigh yalibaini kwamba wanaume hawakuwa na haja ya wanawake wenye kuvalia nguo fupi badala yake wakipendelea wanawake wa kiislamu na wale wa kutoka Ethiopia.

Monday 17 March 2014


RIDHIWANI AANZA MBIO ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE‏


Meneja wa Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Saadani Wilayani Bagamoyo, wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.Baada ya kumaliza Mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Matipwili, Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete alifika katika Kijiji cha Gongo ndani ya Tarafa ya Saadani na kukutana na wananchi wa Kijiji hicho na kuzungumza nao kama aonekanavyo pichani.

Mbunge wa Arumeru Mshariki , Joshua Nassari aumbuka bungeni




Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Joshua Nassari, juzi alijikuta akiumbuka bungeni baada ya kushindwa kutaja kanuni aliyoitumia, kuomba mwongozo. 
 
Hali hiyo ilitokea muda mfupi kabla ya wajumbe kupiga kura za kumchagua Mwenyekiti wa Bunge hilo.
 
Kuumbuka kwa mjumbe huyo ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Mshariki, kulitokana na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo, Pandu Ameir Kificho, kumtaka kutaja kanuni aliyoitumia.
 
Hata hivyo, baada ya kusita kwa muda Nassari bila kutaja kanuni aliyoitumia, alisema wajumbe wengi hawajasikia utaratibu unaotumika katika upigaji kura kwa sababu walichelewa kwenye msongamano wa watu getini.
 
“Wengi wetu tumeingia tukiwa tumechelewa kwa sababu wengi tunapita katika geti moja. Ningependa ufafanuzi wako kuhusu aina ya kura tunayokwenda kupiga ni ya wazi au ya siri,”alisema.
 
Hata hivyo, kificho alimjibu kuwa kura zitakazopigwa kumchagua mwenyekiti zitakuwa ni za siri.
 
Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya Bunge hilo kupitisha kanuni za uendeshaji wake ambapo hata hivyo nyingine bado zimekuwa na mgongano wa maridhiano kwa baadhi ya wajumbe kutaka ufafanuzi zaidi.

Tuesday 11 March 2014

GARI LA KUBEBEA TAKA LILILOACHWA KITUO CHA GEREJI BARABARA YA MANDELA LAWA KERO KWA ABIRIA WANAOTUMIA KITUO HICHO 

 

 

Lori la kubeba taka likiwa eneo kituo cha gereji barabara ya mandela road,huku likiwa limebeba uchafu baada ya kuharibika na limekaa hapo siku mbili.

 

Huo unaonekana kwa juu ni uchafu uliooza na unatoa harufu kali kituoni hapo. eneo la kituo cha gereji mandela road 

 

Abiria wanaotumia kituo cha gereji barabara ya mandela kwa siku mbili mfululizo wamekuwa wakipata kero ya harufu kali inayosababishwa na gari ya kubebea taka iliyopaki kwenye kituo hiko.Wakiongea na mtandao wa wetu huu wa Dj sek abiria hao wamesema kwamba gari hiyo iliharibika ikiwa inaelekea kumwaga uchafu huo na wakaisogeza kituoni hapo ili waweze kuitengeneza, lakini badala yake dereva na wasaidizi wake wakaitelekeza gari iyo toka juzi.Wakiendeleaa kuongea na mtandao wetu wamesema eneo lote la kituoni hapo linatoa harufu kali ambayo ni kero kwa wao wanaosubilia usafiri eneo hilo.

Mwandishi wa blog hii nilishuhudia mwenyewe na kupiga picha pia kuonja adha ya harufu kali inayotoka kwenye gari hiyo.Manispaa ya kinondoni na wasimamizi wa usafi mnaombwa kufuatilia hili na kuweza kulitatua kwani ni kero kwa watumiaji wa kituo hiki. 

KAMPUNI YA GOOGLE YAKANUSHA PICHA YA GOOGLE MAP INAYOONESHA NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA 

KAMPUNI YA GOOGLE YAKANUSHA PICHA YA GOOGLE MAP INAYOONESHA NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA

Kampuni ya google imekanusha habari zilizotapakaa kwenye mitandao mbalimbali duniani kwa kuweka picha ya Google Map ambayo inaonesha ndege ya Malaysia Airline ikiwa imedondondoka ndani ya maji. Msemaji wa google nchini Malaysia amesema
"Yes, the images may be there, but it is not real time satellite images as the images may have provided to us several weeks or months ago," he said when contacted.
Hii imetokana na kutapakaa kwa picha inayoonesha ndege ya Malaysia Airline imedondoka kwenye maji.
Mpaka sasa meli zipatazo 40 na ndege 34 zinazunguka bahari inayizunguka maeneo ya Vietnam na Malysia wakitafuta ndege ya Malaysia Airline iliyopotea toka jumamosi.
Nchi zinazoshiriki kuitafuta ndege hiyo ni Australia, China, Thailand, Indonesia, Singapore, Vietnam, Philippines, New Zealand na Marekani.

 

Askofu Mtetemela awatuliza wananchi

Dodoma. Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Donald Mtetemela amewahakikishia Watanzania kuwa Katiba itapatikana kwa wakati.
Hata hivyo, amesema kuna haja kwa Watanzania wa dini zote kuliombea Bunge Maalumu la Katiba lifanye mambo kwa kumshirikisha Mwenyezi Mungu ili mchakato wa Katiba uende vizuri.
Askofu Mtetemela, ambaye ni mmoja wa mjumbe wa Bunge hilo, alitoa ushauri huo jana kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Alisema kuyumba kwa Bunge la Katiba kwa sasa kunatokana na misimamo ya vyama vya siasa na kwamba kitendo hicho kimesababisha kuchelewa kwa kazi ya msingi.
“Mambo ya misimamo hayawezi kuzuilika na wala si kosa kila kikundi kuwa na msimamo wake, lakini kinachotakiwa ni wajumbe kufuta mambo ya vyama vichwani mwao na hasa pale panapokuwa na hoja ya msingi,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.
“Watanzania waendelee kutuombea kwa nguvu zote. Sina shaka tutatoka hapa tukiwa wamoja kwa sababu tunaimba wimbo mmoja wa kutaka kitu kizuri mbele yetu,” alisisitiza Askofu Mtetemela.
Askofu Mtetemela alisema kuwa katika hatua za awali kulikuwa na misukosuko mikubwa ndani ya Bunge, lakini sasa kuna mwelekeo wa kuridhisha kutokana na wajumbe kuelewa wajibu wao katika mchakato huu.

 

Bunge Maalumu la Katiba sasa vululu vululu

 

Dodoma. Matarajio ya Bunge Maalumu la Katiba kukamilisha kanuni kwa maridhiano yaliyeyuka tena jana huku mambo ndani ya ukumbi yakionekana kuwa vululuvululu kwa baadhi ya wajumbe kuzungumza nje ya utaratibu na wengine kurushiana vijembe.
Baadhi ya wajumbe waliamua kutoleana lugha chafu na kuweka kando hoja za msingi zinazowafanya watofautiane na kuchelewesha kazi ya kuandika Katiba Mpya.
Hali ilichafuka mchana wakati wajumbe walipokutana kupitisha kanuni baada ya mmoja wao, Felix Mkosamali kuomba mwongozo kwa Mwenyekiti wa muda, Pandu Ameir Kificho. Hata hivyo, Kificho alimtaka kukaa chini kwa muda kwa maelezo kuwa wajumbe waliofika katika kikao hicho walikuwa wachache, hivyo mwongozo wake kama ulikuwa unahitaji majibu ingekuwa vigumu kutolewa.
Baada ya muda alisimama, James Mbatia na kuomba mwongozo, akihoji sababu za kutaka kuanza kikao cha kupitisha kanuni hizo wakati wajumbe hawajapewa vitabu vya rasimu ya kanuni zenyewe.
“Mwenyekiti ulitangaza asubuhi kuwa tutagawiwa kanuni kabla ya saa tisa lakini hadi sasa tunataka kusomewa kanuni wakati hatujagawiwa kanuni hizo,” alihoji Mbatia.
Kificho alitoa ufafanuzi kuwa kanuni hizo zilikuwa bado zinadurufiwa na kuwataka wajumbe wawe na nidhamu kwani anapotangaza wanapiga kelele.
Ghafla alisimama Mkosamali tena na kuwasha kipaza sauti na kuhoji kitendo cha mwenyekiti huyo kumpa Mbatia nafasi ya kutoa mwongozo wakati yeye amenyimwa... “Mwenyekiti hivi unaongozaje kikao, inakuwaje mimi nikuombe mwongozo uninyime na mwenzangu umpe? Mwenyekiti nakuheshimu sana, lakini sijui unatumia kanuni ipi kutoa nafasi kwa mjumbe wakati mimi ulinizuia nisiseme,” alihoji Mkosamali.
Baada ya kauli hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Hawa Ghasia aliwasha kipaza sauti na kwa sauti ya juu alisema “Mtoto mdogo hana adabu.” Kauli hiyo iliibua hasira za Mjumbe mwingine, Moses Machali ambaye naye aliwasha kipaza sauti na kumjibu: “Kubwa jinga halina adabu,” kauli iliyoibua miguno ndani ya Bunge.
Hata hivyo, licha ya Mwenyekiti kutoa onyo kwa kauli hizo kwamba hazifai, Mkosamali alisimama katika sehemu yake na kusema kuwa hakuna mtoto mdogo na kwamba tangu lini mtoto aliishinda CCM.
Chanzo cha tatizo
Chanzo cha mvurugano huo ambao wiki iliyopita kidogo usababishe ngumi kurushwa bungeni, ni mfumo wa upigaji kura katika kupitisha ibara za rasimu, ambao jana uliendelea kuwagawa wajumbe na kufanya ukumbi huo kuonekana kama eneo la mzaha.
Kauli za ‘ndiyoooo’, ‘hapanaaaa’ na vitendo vya kugonga meza viliongezeka katika kipindi cha asubuhi baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Kanuni, Profesa Costa Mahalu kuwaleza wajumbe kuwa kamati yake haijafikia mwafaka wa ama iwe kura za siri au wazi na kwamba suala hilo limerejeshwa kwa wajumbe wenyewe.

 

Meli ya Korea Kaskazini yanaswa Libya

Wakuu nchini Libya, wamesema kuwa wameikamata meli moja iliyokuwa na bendera ya Korea Kaskazini, ikiwa na shehena haramu ya mafuta katika bandari inayodhibitiwa na waasi.

 

Msemaji wa shirika la kitaifa la mafuta, amesema kuwa meli hiyo ilisimamishwa ilipokuwa ikijaribu kungoa nanga na kwa sasa inasindikizwa katika bandari inayodhibitiwa na serikali ya Libya.
Maafisa wa serikali ya Libya waliisimamisha Meli hiyo ya Korea Kaskazini ilipokuwa ikiondoka kutoka bandari inayodhibitiwa na waasi siku ya Jumatatu ikiwa imesheheni mzigo usio rasmi wa mafuta ghafi.
Jeshi la nchi hiyo limethibitisha tukio hilo.
Waasi wa zamani wanaotaka kuitenga eneo la Libya Mashariki, wamekuwa wakimiliki bandari ya Al-Sidra na vituo vingine muhimu vya kuuzia bidhaa nje katika eneo hilo tangu Julai mwaka uliopita.
Mnamo siku ya Jumamosi, walianza kupakia shehena ya mafuta yasiyosafishwa ndani ya meli hiyo ya Korea Kaskazini iitwayo Morning Glory, iliyokuwa imetia nanga katika bandari ya Al-Sidra.

Viongozi walaani wizi wa mafuta

Kiwanda cha mafuta nchini Libya
Siku ya Jumatatu jeshi la wanamaji lilizuilia meli hiyo ilipokuwa ikiondoka bandarini, huku amri ikitolewa ielekezwe hadi katika bandari inayodhibitiwa na serikali.
Chama kikuu cha kisiasa nchini humo cha General National Congress, GNC, kimethibitisha kuzuiliwa kwa meli hiyo.
Runinga ya taifa Nchini Libya Al-Nabaa pia imeripoti tukio hilo kwa undani.
Walid al-Tarhuni, ambaye ni msemaji wa zamani wa kundi la waasi ambalo limekuwa likidhibiti bandari hiyo, ameiambia runinga ya Al-Nabaa kuwa meli hiyo ya mizigo ilikuwa ikielekea katika bandari ya Zawiyah, kilomita 50, Magharibi mwa mji mkuu Tripoli, kupakua mafuta hayo.
Utawala wa Washington umesema kuwa umeshangazwa na tukio hilo na kukariri kuwa mafuta inayotoka Libya ni mali ya raia wa nchi hiyo na wala sio ya makundi fulani.

 

Malaysia yazidisha kasi kutafuta Ndege 

Zoezi la kutafuta ndege ya abiria ya Malaysia limeendelea kushika kasi baada ya kuwepo kwa hali ya sintofahamu na wasiwasi mwingi kutoka kwa ndugu za watu waliopotea wakiwa katika ndege hiyo.

 

Ndugu wa waliopotea wameelezwa kuwa wakae tayari kupata habari mbaya

 Mamlaka nchini Malaysia zinasema wameongeza mipaka ya eneo la utafutaji, mara mbili Zaidi, huku China ikiwa imepeleka mitambo 10 ya satelaiti kwa ajili ya kusaidia kutafuta ndege hiyo.

Mkuu wa Idara ya anga Azharuddin AbdulRahman amewaambia waandishi wa habari kuwa eneo la kusaka ndege hiyo limeongezeka mara mbili kutoka maili 50 za baharini kunakosemekana ndege ilipotelea mpaka maili 100.
Ndege iliyokua imebeba watu 239 ilipotea bila kutoa taarifa yeyote na hakuna dalili yeyote mpaka sasa ya kupatikana kwa mabaki ya ndege hiyo.